< Ester 3 >
1 Después de estas cosas, por orden del rey, Aman, hijo de Hamedata, Descendencia de Agag, lo promovió, le dio una posición de honor y un lugar más alto que todos los otros capitanes que estaban con él.
Baada ya matukio haya, Mfalme Ahasuero alimheshimu Hamani mwana wa Hamedatha, Mwagagi, akampandisha na kumpa kiti chake cha heshima cha juu sana kuliko wakuu wengine wote.
2 Y todos los siervos del rey que estaban en la casa del rey bajaron a la tierra antes de Amán y le dieron honor, porque así el rey había dado órdenes. Pero Mardoqueo no bajó ante él ni le dio honor.
Maafisa wote wa mfalme waliokaa langoni mwa mfalme walipiga magoti na kumpa Hamani heshima, kwa kuwa mfalme alikuwa ameamuru hili kuhusu Hamani. Lakini Mordekai hakumpigia magoti wala kumheshimu.
3 Entonces los siervos del rey que estaban en la casa del rey dijeron a Mardoqueo: ¿Por qué vas contra la orden del rey?
Kisha maafisa wa mfalme waliokuwa langoni mwa mfalme walimuuliza Mordekai, “Kwa nini hutii agizo la mfalme?”
4 Cuando le dijeron esto día tras día y él no prestó atención, dejaron que Hamán se enterara, para ver si se pasaba por alto el comportamiento de Mardoqueo, porque les había dicho que era judío.
Siku baada ya siku walizungumza naye lakini hakukubali. Kwa hiyo walimweleza Hamani kuona kama tabia ya Mordekai itaweza kuvumiliwa, kwa maana alikuwa amewaambia kuwa yeye ni Myahudi.
5 Y cuando Amán vio que Mardoqueo no se inclinaba delante de él y le daba honor, Amán se llenó de ira.
Wakati Hamani alipoona kuwa Mordekai hampigii magoti wala kumpa heshima alighadhibika.
6 Pero no fue suficiente para él atacar sólo a Mardoqueo; porque le habían dejado claro quién era el pueblo de Mardoqueo; así que Amán se propuso acabar con todos los judíos, incluso con el pueblo de Mardoqueo, a través de todo el reino de Asuero.
Hata hivyo baada ya kujulishwa watu wa Mordekai ni akina nani, alibadili wazo la kumuua Mordekai peke yake. Badala yake Hamani alitafuta njia ya kuwaangamiza watu wote wa Mordekai, yaani, Wayahudi, walio katika ufalme wote wa Ahasuero.
7 En el primer mes, el mes Nisán, en el duodécimo año del rey Asuero, día a día y mes a mes siguieron buscando un signo, echando él Pur, es decir la suerte, ante Amán, hasta que la señal salió el día trece del duodécimo mes, el mes de Adar.
Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Mfalme Ahasuero, katika mwezi wa kwanza uitwao Nisani, walipiga puri (yaani kura) mbele ya Hamani ili kuchagua siku na mwezi. Kura ikaangukia kwenye mwezi wa kumi na mbili, yaani Adari.
8 Y Amán dijo al rey Asuero: Hay una nación que vive aquí y allá en pequeños grupos entre la gente en todas las divisiones de tu reino; sus leyes son diferentes de las de cualquier otra nación, y no guardan las leyes del rey por esta razón, no es correcto que el rey los deje seguir viviendo en su reino.
Kisha Hamani akamwambia Mfalme Ahasuero, “Wako watu fulani wameenea na kutawanyika miongoni mwa watu katika majimbo yote ya ufalme wako, ambao desturi zao ni tofauti na zile za watu wengine wote, nao hawatii sheria za mfalme. Haifai mfalme kuwavumilia watu hawa.
9 Si es un placer del rey, que se ponga por escrito una declaración que ordene su destrucción y daré a los responsables del negocio del rey, diez mil talentos de plata para el tesoro del rey.
Kama inampendeza mfalme, itolewe amri kuwaangamiza, nami nitaweka talanta 10,000 za fedha katika hazina ya mfalme kwa ajili ya watu watakaoshughulikia jambo hili.”
10 Y el rey tomó su anillo de su mano y se lo dio a Amán, el hijo de Hamedata, de Agag, el enemigo de los judíos.
Basi mfalme alichukua pete yake ya muhuri kutoka kwenye kidole chake na kumpa Hamani mwana wa Hamedatha, Mwagagi, adui wa Wayahudi.
11 Y el rey dijo a Amán: El dinero es tuyo, y con él pueblo, para que hagas con ellos lo que te parezca correcto.
Mfalme akamwambia Hamani, “Baki na fedha yako na uwatendee hao watu utakavyo.”
12 A los trece días del primer mes, se envió a los escribas del rey, y pusieron por escrito las órdenes de Amán a todos los capitanes del rey y a los gobernantes de cada provincia de su reino y a los jefes de cada pueblo, a cada provincia del reino en la escritura comúnmente utilizada allí, y para cada pueblo en el idioma que era suyo; Fue firmado en nombre del rey Asuero y sellado con el anillo del rey.
Kisha siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kwanza waandishi wa mfalme waliitwa. Wakaandika barua kwa kila jimbo na katika kila lugha ya watu kama agizo la Hamani lilivyotoka kwa mfalme, kwa watawala wa majimbo mbalimbali, na wakuu wa watu mbalimbali. Hizi ziliandikwa kwa jina la Mfalme Ahasuero mwenyewe na kutiwa muhuri wa pete yake mwenyewe.
13 Y por medio de mensajeros enviaron cartas a todas las divisiones del reino ordenando la muerte y destrucción de todos los judíos, jóvenes y viejos, niños pequeños y mujeres, el mismo día, incluso el día trece del doceavo mes, el mes Adar, y la toma de todos sus bienes por la fuerza.
Barua zilipelekwa na tarishi katika majimbo yote ya mfalme zikiwa na amri ya kuharibu, kuua na kuangamiza Wayahudi wote, wadogo kwa wakubwa, wanawake na watoto wadogo, siku moja, yaani siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari, na pia kuteka nyara vitu vyao.
14 Una copia de la escritura, que se haría pública en cada parte del reino, fue enviada a todos los pueblos, para que pudieran estar listos cuando llegara ese día.
Nakala ya andiko la amri ilipaswa kutolewa kama sheria katika kila jimbo, na kufahamishwa kwa watu wa kila taifa ili waweze kuwa tayari kwa siku ile.
15 Los corredores salieron rápidamente por orden del rey, y se hizo una declaración pública en Susa: y el rey y Amán tomaron vino juntos, pero la ciudad de Susa estaba conmovida.
Kwa kuharakishwa na amri ya mfalme, matarishi walikwenda na andiko lilitolewa katika mji wa ngome ya Shushani. Mfalme na Hamani waliketi na kunywa, lakini mji wa Shushani ulifadhaika.