< Salmos 55 >

1 Escucha, o! Dios, mi oración; y no te escondas de mi suplicación.
Uyategee sikio maombi yangu, Mungu; nawe usijifiche mbali na kusihi kwangu.
2 Estáme atento, y respóndeme; que doy voces hablando, y estoy desasosegado,
Unitazame kwa makini na unijibu; Sina pumziko katika shida zangu
3 Por la voz del enemigo, por el aprieto del impío; porque echaron sobre mí iniquidad, y con furor me han amenazado.
kwa sababu ya sauti ya adui zangu, kwa sababu ya ukandamizaji wa waovu; maana wananiletea matatizo na kunitesa wakiwa na hasira.
4 Mi corazón está doloroso dentro de mí: y terrores de muerte han caído sobre mí.
Moyo wangu wasumbuka ndani yangu, na hofu ya kifo imeniangukia.
5 Temor y temblor vino sobre mí; y terror me ha cubierto.
Uwoga na kutetemeka kumenijia, nayo hofu imenielemea.
6 Y dije: ¿Quién me diese alas como de paloma? volaría, y descansaría.
Nikasema, “Oh, kama tu ningekuwa na mabawa kama njiwa! Ningelipaa mbali na kupata pumziko.
7 Ciertamente huiría lejos: moraría en el desierto. (Selah)
Tazama, ningeenda mbali; ningekaa jangwani. (Selah)
8 Apresuraríame a escapar del viento tempestuoso, de la tempestad.
Ningefanya haraka kuja mafichoni mwako kuzikimbia dhoruba na tufani.”
9 Deshace, o! Señor, divide la lengua de ellos: porque he visto violencia y rencilla en la ciudad.
Uwaangamize, Bwana, vuruga lugha zao! Kwa maana nimeona vurugu na ugomvi katika mji.
10 Día y noche la cercaron sobre sus muros: e iniquidad y trabajo hay en medio de ella.
Mchana na usiku wao huenda kwenye kuta zake; uchafu na ufisadi uko katikati yake.
11 Agravios hay en medio de ella; y nunca se aparta de sus plazas fraude y engaño.
Uovu uko katikati yake; ukandamizaji na uongo hauiachi mitaa yake.
12 Porque no me afrentó enemigo, que entonces suportára lo: ni el que me aborrecía se engrandeció contra mí, que entonces escondiérame de él.
Kwa maana hakuwa adui aliye nikemea, hivyo ningevumilia; wala ingekuwa ni yule aliye nichukia aliyejiinua mwenyewe dhidi yagu, hivyo ningejificha asinione.
13 Mas tú, hombre según mi estimación, mi señor, y mi familiar.
Lakini ulikuwa wewe, mtu sawa na mimi, mwenzangu na rafiki yangu.
14 Porque juntos comunicábamos suavemente los secretos: en la casa de Dios andábamos en compañía.
Tulikuwa na ushirika mtamu pamoja; tuliingia katika nyumba ya Mungu tukiwa na umati mkubwa.
15 Condenados sean a muerte, desciendan al infierno vivos: porque hay maldades en su compañía, entre ellos. (Sheol h7585)
Kifo na kiwapate ghafla; na washuke wakiwa hai kuzimuni, maana ndiko waishiko waovu, hapo hapo kati yao. (Sheol h7585)
16 Yo a Dios clamaré; y Jehová me salvará.
Lakini kwangu mimi, nitamwita Mungu, na Yahwe ataniokoa.
17 Tarde, y mañana, y a mediodía hablo y estoy gimiendo: y él oirá mi voz.
Wakati wa jioni, asubuhi na mchana ninalalamika na kuomboleza; yeye atasikia sauti yangu.
18 Redimió en paz mi alma de la guerra contra mí; porque muchos fueron contra mí.
Kwa usalama kabisa atayaokoa maisha yangu na vita dhidi yangu, kwa maana wale waliopigana nami walikuwa ni wengi.
19 Dios oirá, y los quebrantará, y el que permanece desde la antigüedad. (Selah) Por cuanto no se mudan, ni temen a Dios.
Mungu, yule unayetawala milele, atawasikia na kuwaaibisha wao. (Selah) Hawabadiliki, na hawamhofu Mungu.
20 Extendió sus manos contra sus pacíficos: violó su pacto.
Rafiki yangu ameinua mikono yake dhidi ya wale waliokuwa na amani naye; Hakuheshimu agano alilokuwa nalo.
21 Ablandan más que manteca las palabras de su boca, mas guerra en su corazón: enternecen sus palabras más que el aceite, mas ellas son espadas.
Mdomo wake ulikuwa laini kama siagi, lakini moyo wake ulikuwa adui; maneno yake yalikuwa laini kuliko mafuta, lakini yalikuwa ni panga zilizochomolewa.
22 Echa sobre Jehová tu carga, y él te sustentará: no dará para siempre resbalo al justo.
Umtwike mizigo yako Yahwe, naye atakusaidia; yeye hataruhusu mtu mwenye haki kuyumbayumba.
23 Y tú, o! Dios, les harás descender al pozo de la sepultura; los varones de sangre, y engañadores no llegarán a la mitad de sus días: mas yo confiaré en ti.
Bali wewe, Mungu, utawaleta waovu chini kwenye shimo la uharibifu; watu wenye kiu ya kumwaga damu na waongo hawataishi hata nusu ya maisha kama wengine, lakini mimi nitakuamini wewe.

< Salmos 55 >