< Job 29 >

1 Job retomó su parábola y dijo
Ayubu akaendelea na kusema,
2 “Oh, si yo fuera como en los meses de antaño, como en los días en que Dios velaba por mí;
Ee, ningekuwa kama nilivyokuwa miezi iliyopita wakati Mungu aliponiagalia,
3 cuando su lámpara brilló sobre mi cabeza, y con su luz atravesé las tinieblas,
taa yake ilipowaka kichwani pangu, na pale nilipotembea gizani kwa nuru yake.
4 como estaba en mi mejor momento, cuando la amistad de Dios estaba en mi tienda,
Ee, kwamba ningekuwa kama nilivyokuwa katika siku za ujana wangu uhusiano wangu na Mungu ulivyokuwa mzuri,
5 cuando el Todopoderoso aún estaba conmigo, y mis hijos estaban a mi alrededor,
wakati Mwenyezi alipokuwa pamoja nami, na wanangu walipokuwa karibu nami,
6 cuando mis pasos fueron lavados con mantequilla, y la roca derramó chorros de aceite para mí,
wakati maisha yangu yalipokuwa yamejawa na utele, na mwamba uliponichuruzishia chemichemi za mafuta.
7 cuando salí a la puerta de la ciudad, cuando preparé mi asiento en la calle.
Nilipokwenda langoni mwa mji, nilipokaa katika eneo la mji,
8 Los jóvenes me vieron y se escondieron. Los ancianos se levantaron y se pusieron de pie.
vijana waliniona na walikaa mbali kwa kuniheshimu, na wazee waliinuka na kusimama kwa ajili yangu.
9 Los príncipes se abstuvieron de hablar, y se puso la mano en la boca.
Wana wa mfalme waliacha kuongea nilipofika; wangeweka mkono wao katika vinywa vyao.
10 La voz de los nobles se acalló, y su lengua se pegó al paladar.
Sauti za waheshimiwa zililazimishwa, na ndimi zao hazikuweza kuongea vinywani mwao.
11 Porque cuando el oído me escuchó, entonces me bendijo, y cuando el ojo me vio, me elogió,
Kwani baada ya kunisikia, wangenibariki; waliponiona, wangeniona na kuniheshimu
12 porque liberé a los pobres que lloraban, y también al huérfano, que no tenía quien le ayudara,
kwa maana nilikuwa nikiwasaidia masikini waliokuwa wakiteseka, na yatima, asiye na msaada.
13 la bendición del que estaba dispuesto a perecer vino sobre mí, y he hecho que el corazón de la viuda cante de alegría.
Baraka zao waliokuwa karibu kuangamia zilinipata; niliufanya moyo wa mjane kuimba kwa furaha.
14 Me vestí de justicia, y me vistió. Mi justicia era como un manto y una diadema.
Nilijivika utakatifu, nao ulinifunika; haki yangu ilikuwa kama kanzu na kilemba.
15 Yo era los ojos de los ciegos, y los pies a los cojos.
Niliwasaidia vipofu; niliwasaidia walemavu.
16 Fui padre de los necesitados. Investigué la causa de él que no conocía.
Niliwasaidia wahitaji; niliwasaidia hata wasionijua.
17 Rompí las mandíbulas de los injustos y arrancó la presa de sus dientes.
Nilimnyamazisha mwovu; nilimpokonya manusura kutoka katika meno yake.
18 Entonces dije: “Moriré en mi propia casa, Contaré mis días como la arena.
Kisha nilisema nitakufa mahali salama; nitazizidisha siku zangu kama mchanga.
19 Mi raíz se extiende hasta las aguas. El rocío reposa toda la noche en mi rama.
Mizizi yangu imeenea majini, na umande kukaa usiku wote katika matawi yangu.
20 Mi gloria está fresca en mí. Mi arco se renueva en mi mano’.
Heshima yangu ni mpya daima, na nguvu za upinde wangu zipo katika mkono wangu kila wakati.
21 “Los hombres me escucharon, esperaron, y guardé silencio por mi consejo.
Watu walinisikiliza; walinisubiri; walisikiliza ushauri wangu.
22 Después de mis palabras no volvieron a hablar. Mi discurso cayó sobre ellos.
Nilipo maliza kuongea hawakunena tena, maneno yangu yaliwatia nguvu kama mvua.
23 Me esperaron como a la lluvia. Sus bocas bebieron como con la lluvia de primavera.
Waliningoja kama kungoja mvua; waliyathamini maneno yangu, kama walivyotamani mvua iliyokawia.
24 Les sonreí cuando no tenían confianza. No rechazaron la luz de mi rostro.
Niliwafurahia bila wao kutarajia; hawakukataa uzuri wa uso wangu.
25 elegí fuera de su camino, y me senté como jefe. Viví como un rey en el ejército, como quien consuela a los dolientes.
Nilikuwa kama mfalme wao na kuwachagulia cha kufanya; nilikuwa kama mfalme katika jeshi lake, kama awafarijiye waombolezaji mazishini.

< Job 29 >