< 2 Samuel 23 >
1 Torej to so zadnje Davidove besede. Jesejev sin David je rekel in mož, ki je bil vzdignjen na visoko, maziljenec Jakobovega Boga in prijeten Izraelov psalmist, je rekel:
Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi: “Neno la Daudi mwana wa Yese, neno la mtu aliyeinuliwa na Aliye Juu Sana, mtu aliyepakwa mafuta na Mungu wa Yakobo, mwimbaji wa nyimbo wa Israeli:
2 » Gospodov Duh je govoril po meni in njegova beseda je bila na mojem jeziku.
“Roho wa Bwana alinena kupitia kwangu, neno lake lilikuwa ulimini mwangu.
3 Izraelov Bog je rekel: ›Izraelova skala mi je spregovorila: ›Kdor vlada nad ljudmi, mora biti pravičen, vladajoč v strahu Božjem.‹‹
Mungu wa Israeli alinena, mwamba wa Israeli akaniambia: ‘Mtu anatawala watu kwa haki, wakati anapotawala akiwa na hofu ya Mungu,
4 In on bo kakor svetloba jutra, ko vzhaja sonce, celó brezoblačno jutro, kakor nežna trava, ki poganja iz zemlje, s čistim sijanjem po dežju.
yeye ni kama mwanga wa asubuhi jua lichomozapo asubuhi isiyo na mawingu, kama mwanga baada ya mvua uchipuzao majani kutoka ardhini.’
5 Čeprav moja hiša ni takšna z Bogom, vendar je z menoj sklenil večno zavezo, urejeno v vseh stvareh in zanesljivo. Kajti to je vsa moja rešitev duše in vsa moja želja, čeprav ji on ne daje rasti.
“Je, si hivyo ilivyo nyumba yangu mbele za Mungu? Je, hajafanya Agano la milele nami, lililopangwa na kuimarishwa kila sehemu? Je, hatanifanya niufurahie wokovu wangu na kunijalia matakwa yangu yote?
6 Toda Beliálovi sinovi bodo vsi izmed njih kakor zavrženo trnje, ker ne morejo biti prijeti z rokami,
Lakini watu waovu wote watatupwa kando kama miiba, ambayo haikusanywi kwa mkono.
7 toda človek, ki se jih bo dotaknil, mora biti ograjen z železom in palico sulice, in na istem kraju bodo popolnoma požgani z ognjem.«
Yeyote agusaye miiba hutumia chombo cha chuma au mpini wa mkuki, nayo huchomwa pale ilipo.”
8 To so imena mogočnih mož, ki jih je imel David: Tahkemoníjec, ki je sedel na sedežu, glavni izmed poveljnikov; enak je bil Ezničan Adino. Svojo sulico je vzdignil proti osemstotim, ki jih je enkrat pobil.
Haya ndiyo majina ya mashujaa wa Daudi: Yosheb-Bashebethi, Mtahkemoni, alikuwa kiongozi wa wale Watatu; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 800, ambao aliwaua katika pambano moja.
9 Za njim je bil Eleazar, sin Dodója, Ahóahovca, z Davidom eden izmed treh mogočnih mož, ko so izzivali Filistejce, ki so bili tam skupaj zbrani za boj in Izraelovi možje so odšli proč.
Wa pili wake alikuwa Eleazari mwana wa Dodai, Mwahohi. Akiwa mmojawapo wa wale mashujaa watatu, alikuwa pamoja na Daudi wakati waliwadhihaki Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko Pas-Damimu kwa ajili ya vita. Kisha watu wa Israeli wakarudi nyuma,
10 Ta je vstal in udarjal Filistejce, dokler njegova roka ni bila izmučena in se je njegova roka trdno oklenila meča in Gospod je tisti dan izvršil veliko zmago in ljudstvo se je vrnilo za njim, [vendar] samo da plenijo.
lakini yeye alisimama imara akawaua Wafilisti hadi mkono wake ukachoka na ukagandamana na upanga. Bwana akawapa ushindi mkubwa siku ile. Vikosi vikarudi kwa Eleazari, kuteka tu nyara za waliokufa.
11 Za njim je bil Šamá, sin Hararéjca Agaja. Filistejci so bili skupaj zbrani v krdelo, kjer je bil kos polja poln leče in ljudstvo je pobegnilo pred Filistejci.
Aliyefuata alikuwa Shama mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti walipokusanyika pamoja mahali palipokuwa shamba lililojaa dengu, vikosi vya Israeli viliwakimbia.
12 Toda on je stal na sredi polja in ga obranil in pobil Filistejce, in Gospod je izvršil veliko zmago.
Lakini Shama akasimama imara katikati ya lile shamba. Akalitetea na kuwaua Wafilisti, naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
13 Trije izmed tridesetih vodij so odšli dol in prišli k Davidu v času žetve, k votlini Adulám, in krdelo Filistejcev je taborilo v dolini Rafájim.
Wakati wa mavuno, viongozi watatu kati ya viongozi thelathini walishuka, wakamwendea Daudi katika pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
14 David je bil takrat v utrdbi in garnizija Filistejcev je bila takrat v Betlehemu.
Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
15 David je hrepenel in rekel: »Oh, da bi mi nekdo dal piti od vode betlehemskega vodnjaka, ki je pri velikih vratih!«
Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu!”
16 Trije mogočni možje so predrli vojsko Filistejcev in zajeli vodo iz betlehemskega vodnjaka, ki je bil pri velikih vratih in jo vzeli ter jo prinesli k Davidu, pa vendar ni hotel piti od nje, temveč jo je izlil Gospodu.
Basi mashujaa hao watatu wakapenya katikati ya Wafilisti, wakaenda kuchota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini Daudi akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
17 Rekel je: »Daleč naj bo od mene, oh Gospod, da bi to storil. Mar ni to kri mož, ki so šli v nevarnosti za svoja življenja?« Zato tega ni hotel piti. Te stvari so storili ti trije mogočni možje.
Akasema, “Iwe mbali nami, Ee Bwana, kufanya kitu hiki. Je, hii si damu ya watu ambao walikwenda kwa kuhatarisha maisha yao?” Naye Daudi hakuyanywa. Haya yalifanywa na hao mashujaa watatu.
18 Abišáj, Joábov brat, Cerújin sin, je bil vodja med tremi. Svojo sulico je dvignil proti tristotim in jih pobil in imel je ime med tremi.
Abishai ndugu yake Yoabu mwana wa Seruya ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300 ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
19 Mar ni bil on najbolj častitljiv izmed treh? Zato je bil njihov poveljnik, vendar prvih treh ni dosegel.
Je, hakupata heshima kubwa zaidi kuliko hao Watatu? Alikuwa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
20 Jojadájev sin Benajá, sin hrabrega moža iz Kabceéla, ki je storil mnogo dejanj, je usmrtil dva, levom podobna moža iz Moába. Odšel je tudi dol in ubil leva v sredi jame v času snega.
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
21 Ubil je Egipčana, čednega moža. Egipčan je imel v svoji roki sulico, toda dol k njemu je šel s palico in iztrgal sulico iz Egipčanove roke in ga ubil z njegovo lastno sulico.
Pia alimuua Mmisri mrefu mkubwa. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki mkononi mwake, Benaya alimwendea akiwa na rungu. Alipokonya mkuki kutoka mkononi mwa Mmisri na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe.
22 Te stvari je storil Jojadájev sin Benajá in imel je ime med tremi mogočnimi možmi.
Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
23 Bil je častitljivejši od tridesetih, vendar prvih treh ni dosegel. In David ga je postavil nad svojo stražo.
Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu. Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
24 Joábov brat Asaél je bil eden izmed tridesetih: Dodójev sin Elhanán iz Betlehema,
Miongoni mwa wale Thelathini walikuwepo: Asaheli ndugu wa Yoabu; Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu;
25 Haródec Šamá, Haródec Eliká,
Shama, Mharodi; Elika, Mharodi;
26 Paltičan Helec, Irá, sin Tekójčana Ikéša,
Helesi, Mpalti; Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa;
27 Anatóčan Abiézer, Hušán Mebunáj,
Abiezeri kutoka Anathothi; Mebunai, Mhushathi;
28 Ahóahovec Calmón, Netófčan Mahráj,
Salmoni, Mwahohi; Maharai, Mnetofathi;
29 Heleb, sin Netófčana Baanája, Ribájev sin Itáj iz Gíbee Benjaminovih otrok,
Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi; Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini;
30 Piratónec Benajá, Hidáj iz Gáaševih potokov,
Benaya Mpirathoni; Hidai kutoka mabonde ya Gaashi;
31 Arbatéjec Abialbón, Barhuméjec Azmávet,
Abi-Alboni, Mwaribathi; Azmawethi, Mbarhumi;
32 Šaalbónec Eljahbá, izmed Jašénovih sinov Jonatan,
Eliaba, Mshaalboni; wana wa Yasheni; Yonathani
33 Hararéjec Šamá, Ahiám, sin Hararéjca Šarárja,
mwana wa Shama, Mharari; Ahiamu mwana wa Sharari, Mharari;
34 Elifélet, sin Ahasbája, sin Maahčána, Eliám, sin Gilčana Ahitófela,
Elifeleti mwana wa Ahasbai, Mmaakathi; Eliamu mwana wa Ahithofeli, Mgiloni;
35 Karmélčan Hecrai, Arbéjec Paarai,
Hezro, Mkarmeli; Paarai, Mwarbi;
36 Natánov sin Jigál iz Cobe, Gádovec Baní,
Igali mwana wa Nathani kutoka Soba; Bani, Mgadi;
37 Amónec Celek, Beeróčan Nahráj, nosilec bojne opreme Cerújinega sina Joába,
Seleki, Mwamoni; Naharai, Mbeerothi, aliyekuwa mbeba silaha za Yoabu mwana wa Seruya;
38 Jéterjevec Irá, Jéterjevec Garéb,
Ira, Mwithiri; Garebu, Mwithiri;
39 Hetejec Urijá; skupaj sedemintrideset.
na Uria, Mhiti. Jumla yao wote walikuwa watu thelathini na saba.