< Zacarias 1 >

1 No oitavo mês, no segundo ano de Dario, a palavra de Javé chegou ao profeta Zacarias, filho de Berequias, filho de Iddo, dizendo:
Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia, mwana wa Ido, kusema:
2 “Javé ficou muito descontente com seus pais.
“Bwana aliwakasirikia sana baba zako wa zamani.
3 Portanto, diga-lhes, Javé dos Exércitos diz: 'Volte para mim', diz Javé dos Exércitos, 'e eu voltarei para você', diz Javé dos Exércitos.
Kwa hiyo waambie watu: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Nirudieni mimi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitawarudia ninyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
4 Não seja como seus pais, a quem os ex-profetas proclamaram, dizendo: Javé dos Exércitos diz: 'Voltem agora de seus maus caminhos e de suas más ações;' mas eles não ouviram nem me escutaram, diz Javé.
Msiwe kama baba zenu, ambao manabii waliotangulia waliwatangazia: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Geukeni, mziache njia zenu mbaya na matendo yenu maovu.’ Lakini hawakunisikiliza wala kufuata maelekezo yangu, asema Bwana.
5 Seus pais, onde estão eles? E os profetas, eles vivem para sempre?
Wako wapi baba zako sasa? Nao manabii, je, wanaishi milele?
6 Mas minhas palavras e meus decretos, que eu ordenei a meus servos, os profetas, eles não ultrapassaram seus pais? “Então eles se arrependeram e disseram: 'Assim como Javé dos Exércitos determinou fazer conosco, de acordo com nossas maneiras e de acordo com nossas práticas, assim ele tem lidado conosco'”.
Je, maneno yangu na amri zangu nilizowaagiza manabii watumishi wangu, hayakuwapata baba zenu?” “Kisha walitubu na kusema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ametutenda sawasawa na njia zetu na matendo yetu yalivyostahili, kama alivyokusudia kufanya.’”
7 No vigésimo quarto dia do décimo primeiro mês, que é o mês de Shebat, no segundo ano de Dario, a palavra de Javé chegou ao profeta Zacarias, filho de Berequias, filho de Ido, dizendo:
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido.
8 “Tive uma visão à noite, e eis que um homem montado em um cavalo vermelho, e ele estava entre as murtas que estavam em um barranco; e atrás dele havia cavalos vermelhos, pardos e brancos.
Wakati wa usiku nilipata maono, mbele yangu alikuwepo mtu akiendesha farasi mwekundu! Alikuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi kwenye bonde. Nyuma yake walikuwepo farasi wekundu, wa kikahawia na weupe.
9 Então perguntei: “Meu senhor, o que são estes?”. O anjo que falou comigo me disse: “Eu lhe mostrarei o que são estes”.
Nikauliza, “Hivi ni vitu gani bwana wangu?” Malaika aliyekuwa akizungumza na mimi akanijibu, “Nitakuonyesha kuwa ni nini.”
10 O homem que estava entre as murtas respondeu: “Eles são os que Yahweh enviou para ir e voltar através da terra”.
Kisha yule mtu aliyesimama katikati ya miti ya mihadasi akaeleza, “Ni wale ambao Bwana amewatuma waende duniani kote.”
11 Eles relataram ao anjo de Javé que estava entre as murtas, e disseram: “Andamos para frente e para trás através da terra, e eis que toda a terra está em repouso e em paz”.
Nao wakatoa taarifa kwa yule malaika wa Bwana, aliyekuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi, “Tumepita duniani kote na kukuta ulimwengu wote umepumzika kwa amani.”
12 Então o anjo de Javé respondeu: “Ó Javé dos Exércitos, por quanto tempo você não terá misericórdia de Jerusalém e das cidades de Judá, contra as quais você teve indignação nestes setenta anos”?
Kisha malaika wa Bwana akasema, “Bwana Mwenye Nguvu Zote, utazuia mpaka lini rehema kutoka Yerusalemu na miji ya Yuda, ambayo umeikasirikia kwa miaka hii sabini?”
13 Yahweh respondeu ao anjo que falou comigo com palavras gentis e reconfortantes.
Kwa hiyo Bwana akazungumza maneno ya upole na ya kufariji kwa malaika aliyezungumza nami.
14 Então o anjo que falou comigo me disse: “Proclama, dizendo: 'Javé dos Exércitos diz: “Tenho inveja de Jerusalém e de Sião com um grande ciúme.
Kisha malaika yule aliyekuwa akizungumza nami akasema, “Tangaza neno hili: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nina wivu sana kwa ajili ya Yerusalemu na Sayuni,
15 Estou muito zangado com as nações que estão à vontade; pois eu estava apenas um pouco descontente, mas elas acrescentaram à calamidade”.
lakini nimeyakasirikia sana mataifa yanayojisikia kuwa yako salama. Nilikuwa nimewakasirikia Israeli kidogo tu, lakini mataifa hayo yaliwazidishia maafa.’
16 Portanto Yahweh diz: “Voltei a Jerusalém com misericórdia. Minha casa será construída nela”, diz Javé dos Exércitos, “e uma linha será estendida sobre Jerusalém””.
“Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Nitairudia Yerusalemu kwa rehema na huko nyumba yangu itajengwa tena. Nayo kamba ya kupimia itanyooshwa Yerusalemu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
17 “Proclamar mais adiante, dizendo: 'Javé dos Exércitos diz: “Minhas cidades voltarão a transbordar de prosperidade, e Javé voltará a confortar Sião, e voltará a escolher Jerusalém””.
“Endelea kutangaza zaidi kwamba: Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Miji yangu itafurika tena ustawi na Bwana atamfariji tena Sayuni na kumchagua Yerusalemu.’”
18 I ergueu meus olhos e viu, e eis que quatro chifres.
Kisha nikatazama juu, na pale mbele yangu nikaona pembe nne!
19 I perguntou ao anjo que falou comigo: “O que são estes?”. Ele me respondeu: “Estes são os chifres que dispersaram Judá, Israel e Jerusalém”.
Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Ni nini hivi?” Akanijibu, “Hizi ni zile pembe zilizowatawanya Yuda, Israeli na Yerusalemu.”
20 Yahweh me mostrou quatro artesãos.
Kisha Bwana akanionyesha mafundi wanne.
21 Then Eu perguntei: “O que estes vêm fazer?”. Ele disse: “Estes são os chifres que dispersaram Judá, de modo que nenhum homem levantou a cabeça; mas estes vieram para aterrorizá-los, para derrubar os chifres das nações que levantaram seu chifre contra a terra de Judá para espalhá-lo”.
Nikauliza, “Hawa wanakuja kufanya nini?” Akanijibu, “Hizi ndizo pembe zilizowatawanya Yuda ili asiwepo atakayeweza kuinua kichwa chake, lakini mafundi wamekuja kuzitia hofu na kuzitupa chini hizi pembe za mataifa ambayo yaliinua pembe zao dhidi ya nchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.”

< Zacarias 1 >