< I Królewska 15 >

1 W osiemnastym roku króla Jeroboama, syna Nebata, Abijam [zaczął] królować nad Judą.
Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
2 Trzy lata królował w Jerozolimie, a jego matka miała na imię Maaka [i była] córką Abiszaloma.
naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
3 Szedł on śladem wszystkich grzechów swego ojca, które popełnił przed nim. Jego serce nie było doskonałe wobec PANA, swego Boga, jak serce Dawida, jego ojca.
Alitenda dhambi zote baba yake alizotenda kabla yake; moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana Mungu wake kama moyo wa Daudi baba yake ulivyokuwa.
4 Jednak ze względu na Dawida PAN, jego Bóg, dał mu pochodnię w Jerozolimie, wzbudzając po nim jego syna i umacniając Jerozolimę;
Pamoja na hayo, kwa ajili ya Daudi, Bwana Mungu wake akampa taa katika Yerusalemu kwa kumwinua mwana atawale badala yake na kwa kuifanya Yerusalemu kuwa imara.
5 Ponieważ Dawid czynił to, co było prawe w oczach PANA, i nie odstąpił od niczego, co mu rozkazał, przez wszystkie dni swego życia, z wyjątkiem sprawy Uriasza Chetyty.
Kwa kuwa Daudi alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana na hakushindwa kushika maagizo yote ya Bwana siku zote za uhai wake, isipokuwa katika habari ya Uria, Mhiti.
6 I trwała wojna między Roboamem a Jeroboamem przez wszystkie dni jego życia.
Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu wakati wote wa maisha ya Abiya.
7 A pozostałe dzieje Abijama i wszystko, co czynił, czyż nie są zapisane w kronikach o królach Judy. I trwała wojna między Abijamem a Jeroboamem.
Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Abiya na yote aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
8 Potem Abijam zasnął ze swoimi ojcami i pogrzebano go w mieście Dawida. I jego syn Asa królował w jego miejsce.
Naye Abiya akalala na baba zake akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake.
9 W dwudziestym roku Jeroboama, króla Izraela, Asa królował nad Judą.
Katika mwaka wa ishirini wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Asa akawa mfalme wa Yuda,
10 I królował czterdzieści jeden lat w Jerozolimie. Jego matka miała na imię Maacha [i była] córką Abiszaloma.
naye akatawala katika Yerusalemu miaka arobaini na mmoja. Bibi yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
11 Asa czynił to, co było prawe w oczach PANA, jak Dawid, jego ojciec.
Asa akatenda yaliyo mema machoni mwa Bwana, kama alivyokuwa ametenda Daudi baba yake.
12 Usunął z ziemi sodomitów i wszystkie bożki, które wykonali jego ojcowie.
Akawafukuza mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu kutoka nchi na kuondoa sanamu zote ambazo baba zake walikuwa wametengeneza.
13 Również Maachę, swoją matkę, odsunął od panowania za to, że sporządziła bożka w gaju. Asa zniszczył więc jej bożka i spalił [go] przy potoku Cedron.
Hata akamwondoa bibi yake Maaka kwenye wadhifa wake kama mama malkia, kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
14 I chociaż wyżyny nie zostały zniszczone, jednak serce Asy było doskonałe wobec PANA przez wszystkie jego dni.
Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
15 I wniósł do domu PANA rzeczy poświęcone przez swego ojca i rzeczy, które sam poświęcił: srebro, złoto i naczynia.
Akaleta ndani ya Hekalu la Bwana fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
16 I między Asą a Baszą, królem Izraela, trwała wojna przez wszystkie ich dni.
Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli siku zote za utawala wao.
17 Basza, król Izraela, nadciągnął przeciwko Judzie i rozbudował Rama, aby [nikomu] nie pozwolić wychodzić od Asy, króla Judy, i przychodzić do niego.
Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
18 Asa wziął więc całe srebro i złoto, które pozostało w skarbcach domu PANA i w skarbcach domu królewskiego, i dał je w ręce swoich sług. Następnie król Asa posłał ich do Ben-Hadada, syna Tabrimona, syna Chezjona, króla Syrii, który mieszkał w Damaszku, mówiąc:
Kisha Asa akachukua fedha yote na dhahabu iliyokuwa imeachwa katika hazina za Hekalu la Bwana na za jumba lake mwenyewe la kifalme. Akawakabidhi maafisa wake na kuwatuma kwa Ben-Hadadi mwana wa Tabrimoni, mwana wa Hezioni, mfalme wa Aramu, aliyekuwa akitawala Dameski.
19 Jest przymierze między mną a tobą, między moim ojcem a twoim ojcem. Oto posyłam ci dar: srebro i złoto. Idź, zerwij swoje przymierze z Baszą, królem Izraela, aby odstąpił ode mnie.
“Akasema na pawepo mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea zawadi ya fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
20 I Ben-Hadad posłuchał króla Asy, i posłał dowódców swoich wojsk przeciwko miastom Izraela, napadł na Ijon, Dan i Abel-Bet-Maaka oraz całe Kinerot wraz z całą ziemią Neftalego.
Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Akaishinda miji ya Iyoni, Dani, Abel-Beth-Maaka na Kinerethi yote, pamoja na Naftali.
21 Gdy Basza [o tym] usłyszał, przestał rozbudowywać Rama i mieszkał w Tirsie.
Wakati Baasha aliposikia hili, akaacha kuijenga Rama na akaenda kuishi Tirsa.
22 Wtedy król Asa zwołał cały lud Judy, bez wyjątku, a lud zabrał z Rama kamienie i drewno, z których Basza budował. I król Asa rozbudował nimi Gibea Beniamina oraz Mispę.
Kisha Mfalme Asa akatoa amri kwa Yuda yote, pasipo kumbagua hata mmoja, kubeba mawe na mbao kutoka Rama, ambazo Baasha alikuwa akitumia huko. Mfalme Asa akazitumia kujengea Geba iliyoko Benyamini na Mispa pia.
23 A pozostałe dzieje Asy, cała jego potęga i wszystko, co czynił, oraz miasta, które zbudował, czyż nie są zapisane w kronikach królów Judy? Jednak w okresie swojej starości zachorował na nogi.
Kwa matukio yote ya utawala wa Asa, mafanikio yake yote, yote aliyofanya na miji aliyoijenga, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Katika uzee wake, hata hivyo, alipata ugonjwa wa miguu.
24 I Asa zasnął ze swoimi ojcami, i został pogrzebany z nimi w mieście Dawida, swego ojca. A jego syn Jehoszafat królował w jego miejsce.
Kisha Asa akalala pamoja na baba zake na kuzikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Naye Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake.
25 W drugim roku Asy, króla Judy, nad Izraelem zaczął królować Nadab, syn Jeroboama i królował nad Izraelem dwa lata.
Nadabu mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Asa wa Yuda, naye akatawala Israeli kwa miaka miwili.
26 I czynił to, co złe w oczach PANA, idąc drogami swego ojca i w jego grzechu, którym doprowadził Izraela do grzechu.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za baba yake na katika dhambi yake, ambayo alisababisha Israeli kuifanya.
27 I Basza, syn Achiasza, z domu Issachara, uknuł spisek przeciw niemu. Basza zabił go w Gibbeton, który należał do Filistynów. Nadab bowiem i cały Izrael oblegali Gibbeton.
Baasha mwana wa Ahiya wa nyumba ya Isakari akafanya shauri baya dhidi yake, naye akamuua huko Gibethoni, mji wa Wafilisti, wakati Nadabu na Israeli yote walipokuwa wameuzingira.
28 Basza zabił go w trzecim roku Asy, króla Judy, i [sam] królował w jego miejsce.
Baasha akamuua Nadabu katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, naye Baasha akaingia mahali pake kuwa mfalme.
29 Kiedy zaczął królować, wymordował cały dom Jeroboama i nie pozostawił żywej duszy [z rodu] Jeroboama, dopóki nie wytracił go zgodnie ze słowem PANA, które wypowiedział przez swego sługę Achiasza Szilonitę;
Mara tu alipoanza kutawala, aliua jamaa yote ya Yeroboamu. Hakumwachia Yeroboamu yeyote aliyekuwa hai, bali aliwaangamiza wote, kulingana na neno la Bwana lililotolewa kupitia kwa mtumishi wake Ahiya Mshiloni,
30 Z powodu grzechów Jeroboama, które popełnił i do których skłonił Izraela; z powodu rozdrażnienia, którym pobudził do gniewu PANA, Boga Izraela.
kwa sababu ya dhambi alizokuwa amezitenda Yeroboamu na kusababisha Israeli kuzitenda, tena kwa sababu alimkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli.
31 A pozostałe dzieje Nadaba i wszystko, co czynił, czyż nie są zapisane w kronikach królów Izraela?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Nadabu na yote aliyofanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
32 I między Asą a Baszą, królem Izraela, trwała wojna po wszystkie ich dni.
Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli wakati wote wa utawala wao.
33 W trzecim roku Asy, króla Judy, nad całym Izraelem zaczął królować w Tirsie Basza, syn Achiasza. [I królował] przez dwadzieścia cztery lata.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya akawa mfalme wa Israeli yote huko Tirsa, naye akatawala kwa miaka ishirini na minne.
34 I czynił to, co złe w oczach PANA, idąc drogami Jeroboama i w jego grzechu, do którego skłonił Izraela.
Akatenda maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za Yeroboamu na dhambi yake, ambayo alikuwa amesababisha Israeli kuitenda.

< I Królewska 15 >