< Proverbiorum 9 >

1 sapientia aedificavit sibi domum excidit columnas septem
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo saba kutoka katika miamba.
2 immolavit victimas suas miscuit vinum et proposuit mensam suam
Ameandaa wanyama wake kwa chakula cha usiku; ameichanganya divai yake; na kuandaa meza yake.
3 misit ancillas suas ut vocarent ad arcem et ad moenia civitatis
Amewatuma watumishi wake kupeleka mialiko na kutoka mahali pa juu sana kwenye mji anaita:
4 si quis est parvulus veniat ad me et insipientibus locuta est
“Wale wasiofunzwa waje hapa!” anawaambia wale wasionaufahamu.
5 venite comedite panem meum et bibite vinum quod miscui vobis
Njoo, ule chakula, na unywe divai nimeshaichanganya.
6 relinquite infantiam et vivite et ambulate per vias prudentiae
Acheni njia zenu za kijinga, na mkaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 qui erudit derisorem ipse sibi facit iniuriam et qui arguit impium generat maculam sibi
Yeyote amrekebishaye mwenye dhihaka hukaribisha matusi na yeyote anayemshutumu mtu mbaya atapata madhara.
8 noli arguere derisorem ne oderit te argue sapientem et diliget te
Usimshutumu mwenye dhihaka, ama atakuchukia; mshutumu mtu mwenye busara, naye atakupenda.
9 da sapienti et addetur ei sapientia doce iustum et festinabit accipere
Mpe mafundisho mtu mwenye busara, naye atakuwa na busara zaidi; mfundishe mtu mwenye haki, naye ataongeza elimu.
10 principium sapientiae timor Domini et scientia sanctorum prudentia
Hofu ya Mungu ni chanzo cha hekima na maarifa ya Mtakatifu ni ufahamu.
11 per me enim multiplicabuntur dies tui et addentur tibi anni vitae
Maana kwa njia yangu siku zako zitazidishwa na uzima wako utaongezewa miaka.
12 si sapiens fueris tibimet ipsi eris si inlusor solus portabis malum
Kama unahekima, unahekima kwako mwenyewe, lakini ukidharau, utaibeba peke yako.
13 mulier stulta et clamosa plenaque inlecebris et nihil omnino sciens
Mwanamke mpumbavu anakelele nyingi- hajafunzwa wala haelewi chochote.
14 sedit in foribus domus suae super sellam in excelso urbis loco
Anakaa kwenye mlango wa nyumba yake, kwenye kiti cha sehemu ya juu sana ya mji.
15 ut vocaret transeuntes viam et pergentes itinere suo
Anawaita kwa sauti wanaopita karibu, watu wale wanaotembea wima katika njia zao.
16 quis est parvulus declinet ad me et vecordi locuta est
Wale ambao hamjafunzwa njoni hapa ndani!” anawaambia wale wasio na akili. “
17 aquae furtivae dulciores sunt et panis absconditus suavior
Maji ya kuiba ni matamu na mkate unaoliwa kwa siri unapendeza.”
18 et ignoravit quod gigantes ibi sint et in profundis inferni convivae eius (Sheol h7585)
Lakini hajui kwamba wafu wapo pale, wageni wake wapo kwenye vina vya kuzimu. (Sheol h7585)

< Proverbiorum 9 >