< Lucam 1 >

1 quoniam quidem multi conati sunt ordinare narrationem quae in nobis conpletae sunt rerum
Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.
2 sicut tradiderunt nobis qui ab initio ipsi viderunt et ministri fuerunt sermonis
Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.
3 visum est et mihi adsecuto a principio omnibus diligenter ex ordine tibi scribere optime Theophile
Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,
4 ut cognoscas eorum verborum de quibus eruditus es veritatem
ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
5 fuit in diebus Herodis regis Iudaeae sacerdos quidam nomine Zaccharias de vice Abia et uxor illi de filiabus Aaron et nomen eius Elisabeth
Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.
6 erant autem iusti ambo ante Deum incedentes in omnibus mandatis et iustificationibus Domini sine querella
Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.
7 et non erat illis filius eo quod esset Elisabeth sterilis et ambo processissent in diebus suis
Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8 factum est autem cum sacerdotio fungeretur in ordine vicis suae ante Deum
Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
9 secundum consuetudinem sacerdotii sorte exiit ut incensum poneret ingressus in templum Domini
Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
10 et omnis multitudo erat populi orans foris hora incensi
Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
11 apparuit autem illi angelus Domini stans a dextris altaris incensi
Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
12 et Zaccharias turbatus est videns et timor inruit super eum
Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
13 ait autem ad illum angelus ne timeas Zaccharia quoniam exaudita est deprecatio tua et uxor tua Elisabeth pariet tibi filium et vocabis nomen eius Iohannem
Lakini malaika akamwambia, “Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
14 et erit gaudium tibi et exultatio et multi in nativitate eius gaudebunt
Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15 erit enim magnus coram Domino et vinum et sicera non bibet et Spiritu Sancto replebitur adhuc ex utero matris suae
Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16 et multos filiorum Israhel convertet ad Dominum Deum ipsorum
Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
17 et ipse praecedet ante illum in spiritu et virtute Heliae ut convertat corda patrum in filios et incredibiles ad prudentiam iustorum parare Domino plebem perfectam
Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake.”
18 et dixit Zaccharias ad angelum unde hoc sciam ego enim sum senex et uxor mea processit in diebus suis
Zakariya akamwambia huyo malaika, “Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu.”
19 et respondens angelus dixit ei ego sum Gabrihel qui adsto ante Deum et missus sum loqui ad te et haec tibi evangelizare
Malaika akamjibu, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.
20 et ecce eris tacens et non poteris loqui usque in diem quo haec fiant pro eo quod non credidisti verbis meis quae implebuntur in tempore suo
Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia.”
21 et erat plebs expectans Zacchariam et mirabantur quod tardaret ipse in templo
Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.
22 egressus autem non poterat loqui ad illos et cognoverunt quod visionem vidisset in templo et ipse erat innuens illis et permansit mutus
Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
23 et factum est ut impleti sunt dies officii eius abiit in domum suam
Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.
24 post hos autem dies concepit Elisabeth uxor eius et occultabat se mensibus quinque dicens
Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:
25 quia sic mihi fecit Dominus in diebus quibus respexit auferre obprobrium meum inter homines
“Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu.”
26 in mense autem sexto missus est angelus Gabrihel a Deo in civitatem Galilaeae cui nomen Nazareth
Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,
27 ad virginem desponsatam viro cui nomen erat Ioseph de domo David et nomen virginis Maria
kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.
28 et ingressus angelus ad eam dixit have gratia plena Dominus tecum benedicta tu in mulieribus
Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe.”
29 quae cum vidisset turbata est in sermone eius et cogitabat qualis esset ista salutatio
Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
30 et ait angelus ei ne timeas Maria invenisti enim gratiam apud Deum
Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
31 ecce concipies in utero et paries filium et vocabis nomen eius Iesum
Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.
32 hic erit magnus et Filius Altissimi vocabitur et dabit illi Dominus Deus sedem David patris eius
Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.
33 et regnabit in domo Iacob in aeternum et regni eius non erit finis (aiōn g165)
Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
34 dixit autem Maria ad angelum quomodo fiet istud quoniam virum non cognosco
Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?”
35 et respondens angelus dixit ei Spiritus Sanctus superveniet in te et virtus Altissimi obumbrabit tibi ideoque et quod nascetur sanctum vocabitur Filius Dei
Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.
36 et ecce Elisabeth cognata tua et ipsa concepit filium in senecta sua et hic mensis est sextus illi quae vocatur sterilis
Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.
37 quia non erit inpossibile apud Deum omne verbum
Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu.”
38 dixit autem Maria ecce ancilla Domini fiat mihi secundum verbum tuum et discessit ab illa angelus
Maria akasema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema.” Kisha yule malaika akaenda zake.
39 exsurgens autem Maria in diebus illis abiit in montana cum festinatione in civitatem Iuda
Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.
40 et intravit in domum Zacchariae et salutavit Elisabeth
Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
41 et factum est ut audivit salutationem Mariae Elisabeth exultavit infans in utero eius et repleta est Spiritu Sancto Elisabeth
Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
42 et exclamavit voce magna et dixit benedicta tu inter mulieres et benedictus fructus ventris tui
akasema kwa sauti kubwa, “Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
43 et unde hoc mihi ut veniat mater Domini mei ad me
Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44 ecce enim ut facta est vox salutationis tuae in auribus meis exultavit in gaudio infans in utero meo
Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45 et beata quae credidit quoniam perficientur ea quae dicta sunt ei a Domino
Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia.”
46 et ait Maria magnificat anima mea Dominum
Naye Maria akasema,
47 et exultavit spiritus meus in Deo salutari meo
“Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
48 quia respexit humilitatem ancillae suae ecce enim ex hoc beatam me dicent omnes generationes
Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
49 quia fecit mihi magna qui potens est et sanctum nomen eius
Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
50 et misericordia eius in progenies et progenies timentibus eum
Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
51 fecit potentiam in brachio suo dispersit superbos mente cordis sui
Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
52 deposuit potentes de sede et exaltavit humiles
amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
53 esurientes implevit bonis et divites dimisit inanes
Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
54 suscepit Israhel puerum suum memorari misericordiae
Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
55 sicut locutus est ad patres nostros Abraham et semini eius in saecula (aiōn g165)
Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele.” (aiōn g165)
56 mansit autem Maria cum illa quasi mensibus tribus et reversa est in domum suam
Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
57 Elisabeth autem impletum est tempus pariendi et peperit filium
Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
58 et audierunt vicini et cognati eius quia magnificavit Dominus misericordiam suam cum illa et congratulabantur ei
Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
59 et factum est in die octavo venerunt circumcidere puerum et vocabant eum nomine patris eius Zacchariam
Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
60 et respondens mater eius dixit nequaquam sed vocabitur Iohannes
Lakini mama yake akasema, “La, sivyo, bali ataitwa Yohane.”
61 et dixerunt ad illam quia nemo est in cognatione tua qui vocetur hoc nomine
Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”
62 innuebant autem patri eius quem vellet vocari eum
Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
63 et postulans pugillarem scripsit dicens Iohannes est nomen eius et mirati sunt universi
Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.
64 apertum est autem ilico os eius et lingua eius et loquebatur benedicens Deum
Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65 et factus est timor super omnes vicinos eorum et super omnia montana Iudaeae divulgabantur omnia verba haec
Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
66 et posuerunt omnes qui audierant in corde suo dicentes quid putas puer iste erit etenim manus Domini erat cum illo
Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
67 et Zaccharias pater eius impletus est Spiritu Sancto et prophetavit dicens
Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
68 benedictus Deus Israhel quia visitavit et fecit redemptionem plebi suae
“Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
69 et erexit cornu salutis nobis in domo David pueri sui
Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
70 sicut locutus est per os sanctorum qui a saeculo sunt prophetarum eius (aiōn g165)
Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu, (aiōn g165)
71 salutem ex inimicis nostris et de manu omnium qui oderunt nos
kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72 ad faciendam misericordiam cum patribus nostris et memorari testamenti sui sancti
Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
73 iusiurandum quod iuravit ad Abraham patrem nostrum
Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
74 daturum se nobis ut sine timore de manu inimicorum nostrorum liberati serviamus illi
tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
75 in sanctitate et iustitia coram ipso omnibus diebus nostris
kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
76 et tu puer propheta Altissimi vocaberis praeibis enim ante faciem Domini parare vias eius
Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
77 ad dandam scientiam salutis plebi eius in remissionem peccatorum eorum
kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.
78 per viscera misericordiae Dei nostri in quibus visitavit nos oriens ex alto
Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,
79 inluminare his qui in tenebris et in umbra mortis sedent ad dirigendos pedes nostros in viam pacis
na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani.”
80 puer autem crescebat et confortabatur spiritu et erat in deserto usque in diem ostensionis suae ad Israhel
Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.

< Lucam 1 >