< Psalmorum 50 >
1 Psalmus Asaph. Deus deorum Dominus locutus est, et vocavit terram a solis ortu usque ad occasum.
Mungu, Mwenye nguvu, Yahwe, amenena naye aliita nchi toka mawio ya jua mpaka machweo yake.
2 Ex Sion species decoris ejus:
Tokea Sayuni, Mungu ameangaza, ukamilifu wa uzuri.
3 Deus manifeste veniet; Deus noster, et non silebit. Ignis in conspectu ejus exardescet; et in circuitu ejus tempestas valida.
Mungu wetu huja naye hakai kimya; mbele yake moto hula, na kuna dhoruba kubwa karibu naye.
4 Advocabit cælum desursum, et terram, discernere populum suum.
Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
5 Congregate illi sanctos ejus, qui ordinant testamentum ejus super sacrificia.
Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
6 Et annuntiabunt cæli justitiam ejus, quoniam Deus judex est.
Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
7 Audi, populus meus, et loquar; Israël, et testificabor tibi: Deus, Deus tuus ego sum.
Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
8 Non in sacrificiis tuis arguam te; holocausta autem tua in conspectu meo sunt semper.
Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
9 Non accipiam de domo tua vitulos, neque de gregibus tuis hircos:
Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
10 quoniam meæ sunt omnes feræ silvarum, jumenta in montibus, et boves.
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
11 Cognovi omnia volatilia cæli, et pulchritudo agri mecum est.
Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
12 Si esuriero, non dicam tibi: meus est enim orbis terræ et plenitudo ejus.
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi; maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
13 Numquid manducabo carnes taurorum? aut sanguinem hircorum potabo?
Je! sitakula nyama ya ngombe na kunywa damu ya mbuzi?
14 Immola Deo sacrificium laudis, et redde Altissimo vota tua.
Mtoleeni Mungu sadaka za shukurani, na mlipe viapo vyenu kwa Aliye Juu.
15 Et invoca me in die tribulationis: eruam te, et honorificabis me.
Mniite katika siku ya shida; nami nitawaokoa
16 Peccatori autem dixit Deus: Quare tu enarras justitias meas? et assumis testamentum meum per os tuum?
Lakini kwa waovu Mungu anasema, “Inawahusu nini kuitangaza hali yangu, kwamba ninyi mmeliweka agano langu mdomoni mwenu,
17 Tu vero odisti disciplinam, et projecisti sermones meos retrorsum.
wakati ninyi mnayachukia maelekezo na mnayatupa maneno yangu?
18 Si videbas furem, currebas cum eo; et cum adulteris portionem tuam ponebas.
Mumuanapo mwizi, ninyi hukubaliana naye; ninyi na mnashirikiana na wale wafanyao uasherati.
19 Os tuum abundavit malitia, et lingua tua concinnabat dolos.
Mwautoa mdomo wenu kwa mabaya, huelezea udanganyifu.
20 Sedens adversus fratrem tuum loquebaris, et adversus filium matris tuæ ponebas scandalum.
Mnakaa na kuongea dhidi ya ndugu yenu; na kukashfu mwana wa mama yenu.
21 Hæc fecisti, et tacui. Existimasti inique quod ero tui similis: arguam te, et statuam contra faciem tuam.
Mmefanya mambo haya, lakini nimekaa kimya, hivyo mlidhani kuwa ni mtu flani nilliye kama ninyi mlivyo. Lakini nitawakaripia ninyi na kuwafunua, mbele ya macho yenu, mambo yote miliyofanya.
22 Intelligite hæc, qui obliviscimini Deum, nequando rapiat, et non sit qui eripiat.
Mlitilie maanani hili, ninyi mnao msahau Mungu, vinginevyo nitawakata ninyi vipande vipande, na hatakuwepo yeyote wakuja kuwasaidia!
23 Sacrificium laudis honorificabit me, et illic iter quo ostendam illi salutare Dei.
Yule atoaye sadaka ya shukurani hunitukuza, na yeyote apangaye njia zake katika namna iliyo sahihi nitamuonesha wokovu wa Mungu.”