< 잠언 7 >

1 내 아들아 내 말을 지키며 내 명령을 네게 간직하라
Mwanangu, shika maneno yangu na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.
2 내 명령을 지켜서 살며 내 법을 네 눈동자처럼 지키라
Shika amri zangu nawe utaishi; linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.
3 이것을 네 손가락에 매며 이것을 네 마음판에 새기라
Yafunge katika vidole vyako; yaandike katika kibao cha moyo wako.
4 지혜에게 너는 내 누이라 하며 명철에게 너는 내 친족이라 하라
Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,” uite ufahamu jamaa yako;
5 그리하면 이것이 너를 지켜서 음녀에게, 말로 호리는 이방 계집에게 빠지지 않게 하리라
watakuepusha na mwanamke mzinzi, kutokana na mwanamke mpotovu na maneno yake ya kubembeleza.
6 내가 내 집 들창으로, 살창으로 내어다 보다가
Kwenye dirisha la nyumba yangu nilitazama nje kupitia upenyo kwenye mwimo wa dirisha.
7 어리석은 자 중에, 소년 중에 한 지혜 없는 자를 보았노라
Niliona miongoni mwa wajinga, nikagundua miongoni mwa wanaume vijana, kijana asiye na akili.
8 그가 거리를 지나 음녀의 골목 모퉁이로 가까이 하여 그 집으로 들어가는데
Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake, akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke
9 저물 때, 황혼 때, 깊은 밤 흑암 중에라
wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake, giza la usiku lilipokuwa likiingia.
10 그 때에 기생의 옷을 입은 간교한 계집이 그를 맞으니
Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki, hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.
11 이 계집은 떠들며 완패하며 그 발이 집에 머물지 아니하여
(Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi, miguu yake haitulii nyumbani;
12 어떤 때에는 거리, 어떤 때에는 광장 모퉁이, 모퉁이에 서서 사람을 기다리는 자라
mara kwenye barabara za mji, mara kwenye viwanja vikubwa, kwenye kila pembe huvizia.)
13 그 계집이 그를 붙잡고 입을 맞추며 부끄러움을 모르는 얼굴로 말하되
Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu, na kwa uso usio na haya akamwambia:
14 내가 화목제를 드려서 서원한 것을 오늘날 갚았노라
“Nina sadaka za amani nyumbani; leo nimetimiza nadhiri zangu.
15 이러므로 내가 너를 맞으려고 나와서 네 얼굴을 찾다가 너를 만났도다
Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki; nimekutafuta na nimekupata!
16 내 침상에는 화문 요와 애굽의 문채 있는 이불을 폈고
Nimetandika kitanda changu kwa kitani za rangi kutoka Misri.
17 몰약과 침향과 계피를 뿌렸노라
Nimetia manukato kitanda changu kwa manemane, udi na mdalasini.
18 오라 우리가 아침까지 흡족하게 서로 사랑하며 사랑함으로 희락하자
Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi; tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!
19 남편은 집을 떠나 먼 길을 갔는데
Mume wangu hayupo nyumbani; amekwenda safari ya mbali.
20 은 주머니를 가졌은즉 보름에나 집에 돌아오리라 하여
Amechukua mkoba uliojazwa fedha na hatakuwepo nyumbani karibuni.”
21 여러가지 고운 말로 혹하게 하며 입술의 호리는 말로 꾀므로
Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha; alimshawishi kwa maneno yake laini.
22 소년이 곧 그를 따랐으니 소가 푸주로 가는 것 같고 미련한 자가 벌을 받으려고 쇠사슬에 매이러 가는 것과 일반이라
Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke kama fahali aendaye machinjoni, kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi,
23 필경은 살이 그 간을 뚫기까지에 이를 것이라 새가 빨리 그물로 들어가되 그 생명을 잃어버릴 줄을 알지 못함과 일반이니라
mpaka mshale umchome ini lake, kama ndege anayenaswa kwenye mtego, bila kujua itamgharimu maisha yake.
24 아들들아 나를 듣고 내 입의 말에 주의하라
Sasa basi wanangu, nisikilizeni; sikilizeni kwa makini nisemalo.
25 네 마음이 음녀의 길로 치우치지 말며 그 길에 미혹지 말지어다
Usiruhusu moyo wako ugeukie njia za huyo mwanamke, wala usitangetange katika mapito yake.
26 대저 그가 많은 사람을 상하여 엎드러지게 하였나니 그에게 죽은 자가 허다하니라
Aliowaangusha ni wengi; aliowachinja ni kundi kubwa.
27 그 집은 음부의 길이라 사망의 방으로 내려가느니라 (Sheol h7585)
Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini, ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol h7585)

< 잠언 7 >