< 詩篇 118 >

1 ヱホバに感謝せよヱホバは恩惠ふかくその憐憫とこしへに絶ることなし
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2 イスラエルは率いふべし その憐憫はとこしへにたゆることなしと
Israeli na aseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
3 アロンの家はいざ言ふべし そのあはれみは永遠にたゆることなしと
Nyumba ya Aroni na iseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
4 ヱホバを畏るるものは率いふべし その憐憫はとこしへにたゆることなしと
Wote wamchao Bwana na waseme sasa: “Upendo wake wadumu milele.”
5 われ患難のなかよりヱホバをよべば ヱホバこたへて我をひろき處におきたまへり
Wakati wa maumivu yangu makuu nilimlilia Bwana, naye akanijibu kwa kuniweka huru.
6 ヱホバわが方にいませばわれにおそれなし 人われに何をなしえんや
Bwana yuko pamoja nami, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
7 ヱホバはわれを助くるものとともに我がかたに坐す この故にわれを憎むものにつきての願望をわれ見ることをえん
Bwana yuko pamoja nami, yeye ni msaidizi wangu. Nitawatazama adui zangu wakiwa wameshindwa.
8 ヱホバに依賴むは人にたよるよりも勝りてよし
Ni bora kumkimbilia Bwana kuliko kumtumainia mwanadamu.
9 ヱホバによりたのむはもろもろの侯にたよるよりも勝りてよし
Ni bora kumkimbilia Bwana kuliko kuwatumainia wakuu.
10 もろもろの國はわれを圍めり われヱホバの名によりて彼等をほろぼさん
Mataifa yote yalinizunguka, lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
11 かれらは我をかこめり我をかこめりヱホバの名によりて彼等をほろぼさん
Walinizunguka pande zote, lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
12 かれらは蜂のごとく我をかこめり かれらは荊の火のごとく消たり われはヱホバの名によりてかれらを滅さん
Walinizunguka kama kundi la nyuki, lakini walikufa haraka kama miiba iteketeayo; kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
13 汝われを倒さんとしていたく剌つれど ヱホバわれを助けたまへり
Nilisukumwa nyuma karibu kuanguka, lakini Bwana alinisaidia.
14 ヱホバはわが力わが歌にしてわが救となりたまへり
Bwana ni nguvu yangu na wimbo wangu, yeye amefanyika wokovu wangu.
15 歓喜とすくひとの聲はただしきものの幕屋にあり ヱホバのみぎの手はいさましき動作をなしたまふ
Sauti za shangwe na ushindi zinavuma hemani mwa wenye haki: “Mkono wa kuume wa Bwana umetenda mambo makuu!
16 ヱホバのみぎの手はたかくあがりヱホバの右の手はいさましき動作をなしたまふ
Mkono wa kuume wa Bwana umeinuliwa juu, mkono wa kuume wa Bwana umetenda mambo makuu!”
17 われは死ることなからん 存へてヤハの事跡をいひあらはさん
Sitakufa, bali nitaishi, nami nitatangaza yale Bwana aliyoyatenda.
18 ヤハはいたく我をこらしたまひしかど死には付したまはざりき
Bwana ameniadhibu vikali, lakini hakuniacha nife.
19 わがために義の門をひらけ 我そのうちにいりてヤハに感謝せん
Nifungulie malango ya haki, nami nitaingia na kumshukuru Bwana.
20 こはヱホバの門なりただしきものはその内にいるべし
Hili ni lango la Bwana ambalo wenye haki wanaweza kuliingia.
21 われ汝に感謝せん なんぢ我にこたへてわが救となりたまへばなり
Nitakushukuru, kwa kuwa ulinijibu, umekuwa wokovu wangu.
22 工師のすてたる石はすみの首石となれり
Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni.
23 これヱホバの成たまへる事にしてわれらの目にあやしとする所なり
Bwana ametenda hili, nalo ni la kushangaza machoni petu.
24 これヱホバの設けたまへる日なり われらはこの日によろこびたのしまん
Hii ndiyo siku Bwana aliyoifanya, tushangilie na kufurahi ndani yake.
25 ヱホバよねがはくはわれらを今すくひたまへ ヱホバよねがはくは我儕をいま榮えしめたまヘ
Ee Bwana, tuokoe, Ee Bwana, utujalie mafanikio.
26 ヱホバの名によりて來るものは福ひなり われらヱホバの家よりなんぢらを祝せり
Heri yule ajaye kwa jina la Bwana. Kutoka nyumba ya Bwana tunakubariki.
27 ヱホバは神なり われらに光をあたへたまへり 繩をもて祭壇の角にいけにへをつなげ
Bwana ndiye Mungu, naye ametuangazia nuru yake. Mkiwa na matawi mkononi, unganeni kwenye maandamano ya sikukuu hadi kwenye pembe za madhabahu.
28 なんぢはわが神なり我なんぢに感謝せん なんぢはわが神なり我なんぢを崇めまつらん
Wewe ni Mungu wangu, nitakushukuru, wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza.
29 ヱホバにかんしやせよ ヱホバは恩惠ふかくその憐憫とこしへに絶ることなし
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.

< 詩篇 118 >