< II Samuel 3 >
1 Ita, adda napaut a gubat iti nagbaetan ti balay ni Saul ken iti balay ni David. Ket pimmigsa a pimmigsa ni David, ngem kimmapuy a kimmapuy ti balay ni Saul.
Vita kati ya nyumba ya Sauli na nyumba ya Daudi vilidumu kwa muda mrefu. Daudi akaendelea kuwa imara zaidi na zaidi, wakati nyumba ya Sauli iliendelea kudhoofika zaidi na zaidi.
2 Naipasngay dagiti putot ni David idiay Hebron. Ti inauna a putot ket ni Amnon, a putotna kenni Ahinoam manipud Jezreel.
Wana walizaliwa kwa Daudi huko Hebroni: Mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Amnoni mwana wa Ahinoamu wa Yezreeli;
3 Ti maikaddua a putotna ket ni Keleab, nga impasngay ni Abigail, ti balo ni Nabal a taga Carmel. Ti maikatlo, ni Absalon, a putot ni Maaca a putot Tolmai nga ari ti Gesur.
mzaliwa wake wa pili alikuwa Danieli mwana wa Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli; wa tatu, Absalomu mwana wa Maaka, binti Talmai mfalme wa Geshuri;
4 Ti maikapat a putot ni David, ni Adonija nga anak ni Haggit. Ti maikalima a putotna ket ni Sefatias nga anak ni Abital,
wa nne, Adoniya mwana wa Hagithi; wa tano, Shefatia mwana wa Abitali;
5 ken ti maikanem, ni Itream nga anak ti asawa ni David a ni Egla. Dagitoy dagiti lallaki a putot ni David a naiyanak idiay Hebron.
wa sita, Ithreamu mwana wa Egla, mkewe Daudi. Hawa ndio waliozaliwa kwa Daudi huko Hebroni.
6 Dimteng ti tiempo kabayatan ti gubat iti nagbaetan ti balay ni Saul ken iti balay ni David a pinapigsa ni Abner ti bagina iti balay ni Saul.
Wakati wa vita kati ya nyumba ya Sauli na nyumba ya Daudi, Abneri alikuwa anajiimarisha katika nafasi yake kwenye nyumba ya Sauli.
7 Adda inkabbalay ni Saul a managan Rispa, a babai nga anak ni Aiah. Kinuna ni Isboset kenni Abner, “Apay a kinaiddam ti inkabbalay ni amak?”
Basi Sauli alikuwa amekuwa na suria, jina lake Rispa binti wa Aiya. Naye Ish-Boshethi akamwambia Abneri, “Kwa nini umekutana kimwili na suria wa baba yangu?”
8 Ket makaunget unay ni Abner kadagiti sasao ni Isboset ket kinunana, “Maysaak kadi nga ulo ti aso ti Juda? Ita nga aldaw, ipakpakitak ti kinapudnok iti balay ni Saul, nga amam, kadagiti kakabsatna a lallaki ken kadagiti gagayyemna, babaen iti saanko panangipaima kenka kenni David. Ngem pabasulennak pay laeng ita nga aldaw maipapan iti dayta a babai?
Abneri akakasirika sana kwa sababu ya kile Ish-Boshethi alichosema, naye akamjibu, “Je, mimi ni kichwa cha mbwa, kwa upande wa Yuda? Siku hii ya leo mimi ni mtiifu kwa nyumba ya baba yako Sauli, kwa jamaa yake na rafiki zake. Sijakukabidhi kwa Daudi, lakini bado unanilaumu kwa kosa la kuhusika na huyu mwanamke!
9 Aramiden koma ti Dios kaniak, Abner, ken nalablabes pay, no saanko nga aramiden para kenni David ti kas insapata ni Yahweh kenkuana,
Mungu na amshughulikie Abneri, tena kwa ukali, ikiwa sitafanya kwa ajili ya Daudi kile Bwana alichomwahidi kwa kiapo,
10 nga iyakar ti pagarian manipud iti balay ni Saul ken panangisaad iti trono ni David iti entero nga Israel, ken iti entero a Juda, manipud Dan agingga iti Beerseba.”
na kuuhamisha ufalme kutoka kwenye nyumba ya Sauli na kuimarisha kiti cha ufalme cha Daudi juu ya Israeli na Yuda kuanzia Dani mpaka Beer-Sheba.”
11 Saan a makasungbat ni Isboset kenni Abner, gapu ta mabuteng isuna kenkuana.
Ish-Boshethi hakuthubutu kusema neno jingine kwa Abneri, kwa sababu alimwogopa Abneri.
12 Ket nangibaon ni Abner kadagiti mensahero a mapan kenni David a makisarita para kenkuana a mangibaga, “Siasino ti makindaga iti daytoy? Makitulagka kaniak ket makitamto nga adda kenka ti imak, a mangiyeg kenka iti amin nga Israel.”
Ndipo Abneri akatuma wajumbe kwa niaba yake kwa Daudi, kumwambia, “Nchi hii ni ya nani? Fanya mapatano na mimi, nami nitakusaidia kuiweka Israeli yote juu yako.”
13 Simmungbat ni David, “Nasayaat, makitulagak kenka. Ngem maysa a banag ti kiddawek kenka ket saanmo a makita ti rupak malaksid no iyegmo nga umuna ni Mikal, ti putot a babai ni Saul inton umaynak kitaen.”
Daudi akasema, “Vyema, nitafanya mapatano nawe. Lakini nahitaji jambo moja kwako: Usije mbele yangu mpaka umemleta Mikali binti Sauli wakati utakapokuja kuniona.”
14 Ket nangibaon ni David kadagiti mensahero kenni Isboset, a putot ni Saul, a kunkunana, “Itedmo kaniak ti asawak a ni Mikal, ta binayadak iti gatad a sangagasut a kudil ti mabagbagi dagiti Filisteo.”
Kisha Daudi akapeleka wajumbe kwa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, kudai, “Nipe Mikali mke wangu, ambaye nilimposa mwenyewe kwa mahari ya magovi 100 ya Wafilisti.”
15 Isu a nangibaon ni Isboset iti mangala kenni Mikal manipud iti asawana, a ni Paltiel a putot ni Lais.
Kwa hiyo Ish-Boshethi akatoa amri kwamba Mikali achukuliwe kutoka kwa Paltieli mumewe, mwana wa Laishi.
16 Kimmuyog kenkuana ti asawana nga agsangsangit kabayatan ti ipapanna, ket simmurot kenkuana agingga idiay Bahurim. Ket kinuna ni Abner kenkuana, “Agawidkan.” Isu a nagsubli isuna.
Hata hivyo, mumewe alikwenda pamoja naye, akilia nyuma ya mkewe njia yote hadi Bahurimu. Ndipo Abneri akamwambia Paltieli, “Rudi nyumbani!” Kwa hiyo akarudi.
17 Nakisarita ni Abner kadagiti panglakayen ti Israel a kunana, “Iti napalabas kinalikagumanyo nga agari koma ni David kadakayo.
Abneri akafanya shauri pamoja na wazee wa Israeli, akasema, “Muda mrefu mmetaka kumfanya Daudi mfalme wenu.
18 Aramidenyo itan. Gapu ta imbaga ni Yahweh maipapan kenni David a kunana, 'Babaen iti ima ti adipenko a ni David isalakankonto dagiti tattaok nga Israel manipud iti pannakabalin dagiti Filisteo ken kadagiti amin a kabusorda.'”
Sasa fanyeni hivyo! Kwa maana Bwana alimwahidi Daudi akisema, ‘Kwa kupitia Daudi mtumishi wangu nitawaokoa watu wangu Israeli kutoka mikononi mwa Wafilisti na kutoka mikononi mwa adui zako wote.’”
19 Nakisao pay a mismo ni Abner kadagiti tattao ti Benjamin. Kalpasanna, napan pay ni Abner a makisarita kenni David idiay Hebron tapno ipalawagna amin a banbanag a tinarigagayan dagiti Israelita ken ti sangkabalayan ti Benjamin nga aramiden.
Pia Abneri mwenyewe akazungumza na kabila la Benyamini. Kisha akaenda mpaka Hebroni kumwambia Daudi kila kitu ambacho Israeli na nyumba yote ya Benyamini walichotaka kufanya.
20 Idi simmangpet idiay Hebron da Abner ken dagiti duapulo kadagiti tattaona a mangkita kenni David, nangisagana ni David iti padaya para kadakuada.
Wakati Abneri aliyekuwa na watu ishirini pamoja naye, alipokuja kwa Daudi huko Hebroni, Daudi akamwandalia karamu pamoja na watu wake.
21 Impalawag ni Abner kenni David, “Tumakderak ket ummongek amin nga Israel para kenka, apok nga ari, tapno makitulagda kenka tapno maiturayam dagiti amin a tarigagayam nga iturayan.” Pinapanaw ngarud ni David ni Abner, ket pimmanaw ni Abner nga addaan kapia.
Ndipo Abneri akamwambia Daudi, “Niache niende mara moja nikakusanye Israeli yote kwa ajili ya mfalme bwana wangu, ili waweze kufanya mapatano na wewe, ili kwamba uweze kutawala juu ya yote yale ambayo moyo wako unaonea shauku.” Basi Daudi akamuaga Abneri, naye akaenda kwa amani.
22 Kalpasanna, simmangpet dagiti soldado ni David ken ni Joab manipud iti panangrautda ket adu ti insangpetda a sinamsamda. Ngem awanen ni Abner iti ayan ni David idiay Hebron. Pinapanawen ni David, ket nakapanawen ni Abner addaan kapia.
Wakati huo huo, watu wa Daudi na Yoabu walirudi kutoka kwenye kushambulia, nao wakarudi na nyara nyingi mno. Lakini Abneri hakuwa tena pamoja na Daudi huko Hebroni, kwa sababu Daudi alikuwa amemruhusu aende zake, naye akaenda kwa amani.
23 Idi simmangpet da Joab ken amin nga armada a kaduana, imbagada kenni Joab, “Ni Abner a putot ni Ner ket napan iti ari, ket pinapanaw ti ari isuna, ket pimmanaw ni Abner nga addaan kapia.”
Yoabu na askari wote aliokuwa nao walipowasili, aliambiwa kwamba Abneri mwana wa Neri alikuwa amekuja kwa mfalme na kwamba mfalme alikuwa amemruhusu aende zake, na kwamba alikwisha ondoka kwa amani.
24 Ket napan ni Joab iti ayan ti Ari ket kinunana, “Ania ti inaramidmo? Kitaeman, immay ni Abner kenka! Apay a pinapanawmo isuna, ket awanen isuna?
Basi Yoabu alikwenda kwa mfalme na kumwambia, “Ni nini hiki ulichofanya? Tazama, Abneri alikuja kwako. Kwa nini ukamwacha aende? Sasa amekwenda!
25 Saanmo kadi nga ammo nga immay ni Abner a putot ni Ner tapno allilawennaka ken tapno ammoenna dagiti panggepmo, ken adalenna ti tunggal aramidem?”
Wajua Abneri mwana wa Neri alikuja kukudanganya na kuchunguza nyendo zako na kupata kila kitu unachokifanya.”
26 Idi pinanawan ni Joab ni David, nangibaon ni Joab kadagiti mensahero a mangkamakam kenni Abner, ket insublida isuna manipud iti bubon ti Sira, ngem saan nga ammo ni David daytoy.
Ndipo Yoabu akamwacha Daudi na kutuma wajumbe wamfuate Abneri, nao wakamrudisha kutoka kisima cha Sira. Lakini Daudi hakufahamu jambo hili.
27 Idi nakasubli ni Abner idiay Hebron, inayaban isuna ni Joab idiay igid ti ruangan tapno makisarita kenkuana iti sililimed, ket sadiay a dinuyok ni Joab ti tianna ket pinapatayna isuna. Iti daytoy a wagas, imbales ni Joab ti dara ni Asael a kabsatna.
Basi Abneri aliporudi Hebroni, Yoabu akamchukua kando ndani ya lango, kama vile kuzungumza naye faraghani. Ili kulipiza kisasi damu ya nduguye Asaheli, Yoabu akamchoma mkuki tumboni palepale, naye akafa.
28 Idi nangngeg ni David ti maipapan iti daytoy ket kinunana, “Siak ken ti pagariak ket agnanayon nga inosente iti sangoanan ni Yahweh maipapan iti dara ni Abner nga anak ni Ner. “Agdissuor koma ti dibbut iti pannakatay ni Abner iti ulo ni Joab ken iti amin a balay ti amana.
Baadaye, Daudi aliposikia kuhusu jambo hili, akasema, “Mimi na ufalme wangu kamwe hatuna hatia mbele za Bwana kuhusu damu ya Abneri mwana wa Neri.
29 Adda koma a kanayon iti pamiliana ti agtutot wenno sakit ti kudil wenno lugpi ken agsarrukod a magna wenno matay iti kampilan wenno agkurang iti makan.
Damu yake na iwe juu ya kichwa cha Yoabu na juu ya nyumba yote ya baba yake! Kamwe asikosekane yeyote katika nyumba ya Yoabu mwenye kidonda chenye usaha, au ukoma au mwenye kuegemea fimbo au aangukaye kwa upanga au kupungukiwa na chakula.”
30 Isu a pinatay da Joab ken Abisai a kabsatna ni Abner, gapu ta napatayna ti kasbatda a ni Asael iti ranget idiay Gabaon.
(Yoabu na Abishai ndugu yake walimuua Abneri kwa sababu alikuwa amemuua Asaheli ndugu yao katika vita huko Gibeoni.)
31 Kinuna ni David kenni Joab ken kadagiti amin a tattao a kakaduana, “Pisangenyo dagiti pagan-anayyo, agarwatkayo iti nakirsang a lupot, ket dung-awanyo ti bangkay ni Abner.” Ket nagna ni David iti likudan ti bangkay idi maipunpon daytoy.
Kisha Daudi akamwambia Yoabu na watu wote aliokuwa pamoja nao, “Rarueni nguo zenu na mvae nguo za gunia na mtembee mkiomboleza mbele ya Abneri.” Mfalme Daudi mwenyewe akatembea nyuma ya jeneza.
32 Intanemda ni Abner idiay Hebron. Impigsa ti ari ti sangitna idiay tanem ni Abner, ket nagsangit met dagiti amin a tattao.
Wakamzika Abneri huko Hebroni, naye mfalme akalia kwa sauti kwenye kaburi la Abneri. Pia watu wote wakalia.
33 Nagleddaang ti ari ken nagdung-aw, “Rumbeng kadi a matay ni Abner a kas iti pannakatay ti maysa a maag?
Mfalme akaimba ombolezo hili kwa ajili ya Abneri: “Je, ilipasa Abneri afe kama afavyo mpumbavu?
34 Saan nagalotan dagiti imam. Saan a nakawaran dagiti sakam. Kas iti pannakapasag ti tao iti sangoanan dagiti annak ti awanan hustisia, isu a napasagka.” Nagsangit manen dagiti tattao gapu kenkuana.
Mikono yako haikufungwa, miguu yako haikufungwa pingu. Ulianguka kama yeye aangukaye mbele ya watu waovu.” Nao watu wote wakamlilia tena.
35 Immay dagiti amin a tattao a mangallukoy kenni David a mangan kabayatan nga aldaw pay laeng, ngem nagsapata ni David, “Aramiden koma ti Dios kaniak, ken ad-ada pay koma, no rumamanak ti tinapay wenno anaiman sakbay a lumnek ti init.”
Kisha watu wote wakaja kumsihi Daudi ale chochote kulipokuwa kungali bado mchana; lakini Daudi akaapa, akisema, “Mungu na anishughulikie, tena kwa ukali, kama nikionja mkate au kitu kingine chochote kabla ya jua kutua!”
36 Nadlaw dagiti amin a tattao ti panagladingit ni David, ken naay-ayoda iti daytoy, aniaman nga inaramid ti ari ket naay-ayoda.
Watu wote wakaona hilo nao ikawapendeza; naam, kila kitu mfalme alichofanya kiliwapendeza.
37 Isu a naawatan amin dagiti tattao ken amin nga Israelita a saan a pagayatan ti ari a mapapatay iti dayta nga aldaw ni Abner nga anak ni Ner.
Kwa hiyo siku ile watu wote na Israeli yote wakajua kwamba mfalme hakushiriki katika mauaji ya Abneri mwana wa Neri.
38 Kinuna ti ari kadagiti adipenna “Saanyo kadi nga ammo a maysa a prinsipe ken natan-ok a tao ti napasag iti daytoy nga aldaw iti Israel?
Kisha mfalme akawaambia watu wake, “Je, hamfahamu kwamba mkuu na mtu mashuhuri ameanguka katika Israeli leo?
39 Ken nakapsutak ita nga aldaw, uray no napulotanak nga ari. Dagitoy a lallaki, a putot ni Zeruyas, ket naranggas unay kaniak. Pagbayaden koma ni Yahweh dagiti managdakdakes, babaen iti panangdusana kenkuana gapu iti kinadangkesna, a kas maikari kenkuana.”
Nami leo ingawa ni mfalme mpakwa mafuta, mimi ni dhaifu, nao hawa wana wa Seruya wananizidi nguvu. Bwana na amlipize mtenda maovu sawasawa na matendo yake maovu!”