< Psalm 73 >
1 Ein Psalm Assaphs. Israel hat dennoch Gott zum Trost, wer nur reines Herzens ist.
Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
2 Ich aber hätte schier gestrauchelt mit meinen Füßen, mein Tritt hätte beinahe geglitten.
Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
3 Denn es verdroß mich auf die Ruhmredigen, da ich sah, daß es den Gottlosen so wohl ging.
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
4 Denn sie sind in keiner Fahr des Todes, sondern stehen fest wie ein Palast.
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5 Sie sind nicht in Unglück wie andere Leute und werden nicht wie andere Menschen geplagt.
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6 Darum muß ihr Trotzen köstlich Ding sein, und ihr Frevel muß wohlgetan heißen.
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7 Ihre Person brüstet sich wie ein fetter Wanst; sie tun, was sie nur gedenken.
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8 Sie vernichten alles und reden übel davon, und reden und lästern hoch her.
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9 Was sie reden, das muß vom Himmel herab geredet sein; was sie sagen, das muß gelten auf Erden.
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10 Darum fällt ihnen ihr Pöbel zu und laufen ihnen zu mit Haufen wie Wasser
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11 und sprechen: Was sollte Gott nach jenen fragen? Was sollte der Höchste ihrer achten?
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
12 Siehe, das sind die Gottlosen; die sind glückselig in der Welt und werden reich.
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
13 Soll's denn umsonst sein, daß mein Herz unsträflich lebt und ich meine Hände in Unschuld wasche
Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
14 und bin geplagt täglich, und meine Strafe ist alle Morgen da?
Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
15 Ich hätte auch schier so gesagt wie sie; aber siehe, damit hätte ich verdammt alle deine Kinder, die je gewesen sind.
Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
16 Ich gedacht ihm nach, daß ich's begreifen möchte; aber es war mir zu schwer
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
17 bis daß ich ging in das Heiligtum Gottes und merkte auf ihr Ende.
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
18 Aber du setzest sie aufs Schlüpfrige und stürzest sie zu Boden.
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
19 Wie werden sie so plötzlich zunichte! Sie gehen unter und nehmen ein Ende mit Schrecken.
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
20 Wie ein Traum, wenn einer erwachet, so machst du, HERR, ihr Bild in der Stadt verschmähet.
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
21 Aber es tut mir wehe im Herzen und sticht mich in meinen Nieren,
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
22 daß ich muß ein Narr sein und nichts wissen und muß wie ein Tier sein vor dir.
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
23 Dennoch bleibe ich stets an dir; denn du hältst mich bei meiner rechten Hand,
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24 du leitest mich nach deinem Rat und nimmst mich endlich mit Ehren an.
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25 Wenn ich nur dich habe, so frage ich nichts nach Himmel und Erde.
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26 Wenn mir gleich Leib und Seele verschmachtet, so bist du doch, Gott, allezeit meines Herzens Trost und mein Teil.
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
27 Denn, siehe, die von dir weichen, werden umkommen; du bringest um alle, die wider dich huren.
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 Aber das ist meine Freude, daß ich mich zu Gott halte und meine Zuversicht setze auf den HERRN HERRN, daß ich verkündige all dein Tun.
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.