< Psaumes 80 >

1 Pour la fin, pour ceux qui seront changés, témoignage d’Asaph, psaume. Vous qui gouvernez Israël, soyez attentif: vous qui conduisez, comme une brebis, Joseph. Vous qui êtes assis sur les Chérubins, manifestez-vous
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
2 Devant Ephraïm, Benjamin et Manassé.
mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
3 Ô Dieu, convertissez-nous, et montrez votre face, et nous serons sauvés.
Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
4 Seigneur, Dieu des armées, jusques à quand serez-vous irrité au sujet de la prière de votre serviteur?
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
5 Jusques à quand nous nourrirez-vous d’un pain de larmes, et nous donnerez-vous à boire des larmes dans une mesure?
Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
6 Vous nous avez posés comme un objet de contradiction à nos voisins; et nos ennemis nous ont insultés.
Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
7 Dieu des armées, convertissez-nous, et montrez votre face, et nous serons sauvés.
Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
8 Vous avez transporté de l’Égypte une vigne, vous avez chassé des nations, et vous l’avez plantée.
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
9 Vous avez été un guide de route devant elle: vous avez planté ses racines, et elle a rempli la terre.
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
10 Son ombre a couvert les montagnes, et ses rameaux les cèdres de Dieu.
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
11 Elle a étendu ses branches jusqu’à la mer, et ses rameaux jusqu’au fleuve.
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
12 Pourquoi donc avez-vous détruit son mur de clôture, et pourquoi la vendangent-ils, tous ceux qui passent dans le chemin?
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
13 Un sanglier de forêt l’a entièrement dévastée; et une bête sauvage l’a broutée.
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
14 Dieu des armées, revenez, regardez du haut du ciel et voyez, et visitez cette vigne.
Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
15 Faites-la prospérer, celle que votre droite à plantée, et portez vos regards sur le fils de l’homme que vous avez établi fermement pour vous.
mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
16 Elle a été brûlée par le feu et déchaussée; par la réprimande de votre visage ils périront.
Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
17 Que votre main repose sur l’homme de votre droite, et sur le fils de l’homme que vous avez établi fermement pour vous.
Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
18 Et nous ne nous éloignerons plus de vous; vous nous rendrez la vie, et nous invoquerons votre nom.
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
19 Seigneur, Dieu des armées, convertissez-nous; et montrez votre face, et nous serons sauvés.
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.

< Psaumes 80 >