< Psaumes 34 >

1 Psaume par David, lorsqu’il changea son visage devant Achimélech, qui le renvoya, et qu’il s’en alla. Je bénirai le Seigneur en tout temps: toujours sa louange sera dans ma bouche.
Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
2 Mon âme se glorifiera dans le Seigneur: que les hommes doux m’entendent et qu’ils soient comblés de joie.
Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
3 Glorifiez le Seigneur avec moi: et exaltons tous pareillement son nom.
Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
4 J’ai recherché le Seigneur, et il m’a exaucé, et il m’a retiré de toutes mes tribulations.
Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
5 Approchez de lui, et vous serez éclairés, et vos faces n’éprouveront pas la confusion.
Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
6 Ce pauvre a crié, et le Seigneur l’a exaucé, et il l’a sauvé de toutes ses tribulations.
Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
7 Un ange du Seigneur se placera autour de ceux qui le craignent, et il les délivrera.
Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
8 Goûtez et voyez combien le Seigneur est doux: heureux l’homme qui espère en lui.
Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
9 Craignez le Seigneur, vous tous ses saints, parce qu’il n’y a pas d’indigence pour ceux qui le craignent.
Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
10 Des riches ont été dans le besoin, et ont eu faim; mais ceux qui cherchent le Seigneur n’éprouveront l’amoindrissement d’aucun bien.
Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
11 Venez, mes enfants, écoutez-moi: je vous enseignerai la crainte du Seigneur.
Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
12 Quel est l’homme qui veut une vie heureuse, qui aime à voir des jours de bonheur?
Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
13 Préserve ta langue du mal; et que tes lèvres ne profèrent point de discours artificieux.
basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
14 Détourne-toi du mal et fais le bien; cherche la paix, poursuis-la.
Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
15 Les yeux du Seigneur sont sur les justes, et ses oreilles à leurs prières.
Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
16 Mais le visage du Seigneur est sur ceux qui font le mal, afin d’effacer de la terre leur mémoire.
Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
17 Les justes ont crié, et le Seigneur les a exaucés: et il les a délivrés de toutes leurs tribulations.
Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
18 Le Seigneur est près de ceux qui ont le cœur affligé; et il sauvera les humbles d’esprit.
Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
19 Nombreuses sont les tribulations des Justes; mais Dieu les délivrera de toutes ces peines.
Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
20 Le Seigneur garde tous leurs os: et pas un seul ne sera brisé.
huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
21 La mort des pécheurs est très funeste; et ceux qui haïssent le juste seront traités comme coupables.
Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
22 Le Seigneur rachètera l’âme de ses serviteurs: et nul de ceux qui espèrent en lui ne sera traité comme coupable.
Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.

< Psaumes 34 >