< Lévitique 11 >

1 Le Seigneur parla encore à Moïse et à Aaron, disant:
Bwana akawaambia Mose na Aroni,
2 Dites aux enfants d’Israël: Voici les animaux que vous devez manger, d’entre tous les animaux de la terre:
“Waambieni Waisraeli: ‘Kati ya wanyama wote waishio juu ya nchi, hawa ndio mtakaowala:
3 Tout ce qui a l’ongle fendu et qui rumine parmi les bêtes, vous en mangerez.
Mwaweza kula mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika sehemu mbili na ambaye hucheua.
4 Pour tout ce qui rumine et qui a un ongle, mais qui ne l’a pas fendu, comme le chameau et tous les autres, vous n’en mangerez point, et vous le compterez parmi les bêtes impures.
“‘Kuna wanyama wengine ambao hucheua tu au wenye kwato zilizogawanyika tu, lakini hao kamwe msiwale. Ngamia ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; kwa kawaida ya ibada hiyo ni najisi kwenu.
5 Le chérogrylle qui rumine, mais qui n’a point l’ongle fendu, est impur.
Pelele ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
6 Le lièvre également; car il rumine, lui aussi, mais il n’a pas l’ongle fendu.
Sungura ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
7 Le pourceau encore, qui quoiqu’il ait l’ongle fendu, ne rumine point.
Naye nguruwe ingawa anazo kwato zilizogawanyika sehemu mbili, hacheui; huyo ni najisi kwenu.
8 Vous ne mangerez point de la chair de ces bêtes, et vous ne toucherez point leurs corps morts, parce qu’ils sont impurs pour vous.
Kamwe msile nyama yao wala kugusa mizoga yao; wao ni najisi kwenu.
9 Voici les bêtes qui sont engendrées dans les eaux, et dont il est permis de manger. Tout ce qui a des nageoires et des écailles, tant dans la mer que dans les rivières et dans les étangs, vous en mangerez.
“‘Kuhusu viumbe wote wanaoishi ndani ya maji ya bahari na vijito, mtakula wale wote wenye mapezi na magamba.
10 Mais tout ce qui n’a pas de nageoires et d’écaillés dans ce qui se meut et vit dans les eaux, vous sera abominable,
Lakini viumbe wote ndani ya bahari au vijito wasio na mapezi na magamba, wakiwa miongoni mwa makundi au viumbe wote ndani ya maji, hao ni machukizo kwenu.
11 Et vous l’aurez en exécration; vous n’en mangerez point la chair et vous éviterez leurs corps morts.
Nao watakuwa machukizo kwenu. Msile nyama yao, nayo mizoga yao itakuwa machukizo.
12 Tout ce qui n’a pas de nageoires et d’écaillés dans les eaux sera impur.
Chochote kinachoishi ndani ya maji ambacho hakina mapezi na magamba kitakuwa chukizo kwenu.
13 Voici ceux des oiseaux que vous ne devez pas manger, et qui sont à éviter pour vous: l’aigle, le griffon, l’aigle de mer,
“‘Wafuatao ndio ndege watakaokuwa machukizo kwenu, hivyo msiwale kwa sababu ni chukizo: tai, furukombe, kipungu,
14 Le milan, le vautour, selon son espèce;
mwewe mwekundu, aina zote za mwewe mweusi,
15 Tout ce qui dans l’espèce du corbeau est à sa ressemblance:
aina zote za kunguru,
16 L’autruche, le hibou, le larus, l’épervier selon son espèce;
mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga, shakwe, aina zote za kipanga,
17 Le chat-huant, le plongeon, l’ibis,
bundi, mnandi, bundi mkubwa,
18 Le cygne, l’onocrotale, le porphyrion,
mumbi, mwari, nderi,
19 Le héron, le pluvier selon son espèce; la huppe et la chauve-souris.
korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
20 Tout ce qui d’entre les volatiles, marche sur quatre pieds, vous sera abominable.
“‘Wadudu wote warukao ambao hutembea kwa miguu minne watakuwa chukizo kwenu.
21 Tout ce qui au contraire marche, à la vérité, sur quatre pieds, mais a les jambes de derrière plus longues, avec lesquelles il saute sur la terre,
Lakini wako viumbe wenye mabawa ambao hutembea kwa miguu minne mtakaowala: wale wenye vifundo katika miguu yao ya kurukaruka juu ya ardhi.
22 Vous devez en manger; tel est le bruchus dans son espèce, l’attachus, l’ophiomachus, la sauterelle, chacun selon son espèce.
Miongoni mwa hawa, mtakula nzige wa aina zote, senene, parare au panzi.
23 Mais tout ce qui d’entre les volatiles a seulement quatre pieds vous sera en exécration;
Lakini viumbe wengine wote wenye mabawa na wenye miguu minne ni machukizo kwenu.
24 Et quiconque touchera leurs corps morts, sera souillé, et il sera impur jusqu’au soir;
“‘Mtajinajisi kwa wanyama hawa. Yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
25 Et s’il est nécessaire qu’il porte quelqu’un de ces animaux mort, il lavera ses vêtements, et il sera impur jusqu’au coucher du soleil.
Yeyote atakayebeba mizoga ya viumbe hawa ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
26 Tout animal qui a un ongle, mais qui ne l’a pas fendu et qui ne rumine pas, est impur; et celui qui le touchera sera souillé.
“‘Kila mnyama mwenye ukwato ulioachana lakini haukugawanyika kabisa, au yule asiyecheua, huyo ni najisi kwenu; yeyote agusaye mzoga wowote wa hao atakuwa najisi.
27 Ce qui marche sur quatre mains, d’entre tous les animaux quadrupèdes qui marchent, sera impur: celui qui touchera leurs corps morts sera souillé jusqu’au soir.
Miongoni mwa wanyama wote watembeao kwa miguu minne, wale watembeao kwa vitanga vyao ni najisi kwenu; yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
28 Et celui qui portera des corps morts de cette sorte, lavera ses vêtements, et il sera impur jusqu’au soir, parce que toutes ces choses sont immondes pour vous.
Yeyote atakayebeba mizoga yao ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni. Wanyama hawa ni najisi kwenu.
29 Vous compterez aussi parmi les choses souillées d’entre les animaux qui se meuvent sur la terre, la belette, le rat et le crocodile, chacun selon son espèce;
“‘Kuhusu wanyama watambaao juu ya ardhi, hawa ni najisi kwenu: kicheche, panya, aina yoyote ya mijusi mikubwa,
30 La musaraigne, le caméléon, le stellion, le lézard et la taupe.
guruguru, kenge, mijusi ya ukutani, goromoe na kinyonga.
31 Tout ces animaux sont impurs. Celui qui touchera leurs corps morts sera impur jusqu’au soir;
Hao wote watambaao juu ya ardhi ni najisi kwenu. Yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
32 Et sur quoi que ce soit que tombe quelque chose de leurs corps morts, il sera souillé; que ce soit un vase de bois, ou un vêtement, ou des peaux et des cilices; et tous les objets avec lesquels se fait quelque ouvrage, seront lavés dans l’eau, et seront souillés jusqu’au soir, et de cette manière ils seront ensuite purifiés.
Ikiwa mmoja wao atakufa na kuangukia juu ya kitu fulani, chombo hicho, hata kikiwa cha matumizi gani, kitakuwa najisi, kiwe kimetengenezwa kwa mti, nguo, ngozi au gunia. Kiweke ndani ya maji; kitakuwa najisi mpaka jioni, kisha kitakuwa safi tena.
33 Mais le vase de terre dans l’intérieur duquel quelqu’une de ces choses sera tombée, sera souillé; il doit être brisé.
Ikiwa mmoja wa wanyama aliyekufa ataangukia ndani ya chungu, kila kilichomo katika chungu hicho kitakuwa najisi, nawe ni lazima uvunje chungu hicho.
34 Tout aliment que vous mangerez, s’il se répand de l’eau sur lui, sera impur; et toute liqueur qui se boit dans un vase quelconque, sera impure.
Chakula chochote ambacho chaweza kuliwa lakini kikawa kimeingia maji kutoka kwenye chungu hicho ni najisi, na kitu chochote cha majimaji ambacho chaweza kunyweka kutoka kwenye chungu hicho ni najisi.
35 Et tout ce qui de tels corps morts tombera sur le vase, sera impur; que ce soient des fours, ou des marmites, ils seront brisés et ils seront impurs.
Chochote ambacho mzoga wa mmojawapo utaangukia kitakuwa najisi. Jiko au chungu cha kupikia ni lazima kivunjwe. Ni najisi, nawe ni lazima uvihesabu kuwa najisi.
36 Mais les fontaines et les citernes et tout réservoir d’eaux sera pur. Celui qui touchera le corps mort de ces animaux, sera souillé.
Lakini chemchemi au kisima, mahali pa kuchota maji, patakuwa safi, lakini yeyote atakayegusa moja ya mizoga hii ni najisi.
37 S’il tombe sur la semence, il ne la souillera pas.
Kama mzoga ukianguka juu ya mbegu zozote ambazo ni za kupanda, zinabaki safi.
38 Mais si quelqu’un répand de l’eau sur la semence, et qu’après cela elle soit touchée par les corps morts, elle sera aussitôt souillée.
Lakini kama mbegu imetiwa maji na mzoga ukaanguka juu yake, hiyo mbegu ni najisi kwenu.
39 S’il meurt un animal qu’il vous est permis de manger, celui qui touchera son corps sera impur jusqu’au soir;
“‘Kama mnyama ambaye mnaruhusiwa kumla akifa, yeyote atakayeugusa mzoga wake atakuwa najisi mpaka jioni.
40 Et celui qui en mangera quelque chose ou en portera, lavera ses vêtements et sera impur jusqu’au soir.
Yeyote atakayekula sehemu ya mzoga huo ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni. Yeyote atakayebeba mzoga huo ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
41 Tout ce qui rampe sur la terre sera abominable; et l’on n’en prendra point pour nourriture.
“‘Kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi ni chukizo; kisiliwe.
42 Tout ce qui étant quadrupède, et ce qui ayant beaucoup de pieds marche sur la poitrine, ou se traîne sur la terre, vous n’en mangerez point, parce qu’il est abominable.
Msile kiumbe chochote kitambaacho juu ya ardhi, kiwe kitambaacho kwa tumbo lake, au kitambaacho kwa miguu minne au kwa miguu mingi; ni chukizo.
43 Ne souillez point vos âmes, et ne touchez aucune de ces choses, de peur que vous ne soyez impurs.
Msijitie unajisi kwa chochote katika viumbe hivi. Msijitie unajisi kwa viumbe hivyo au kutiwa unajisi navyo.
44 Car c’est moi qui suis le Seigneur votre Dieu: soyez saints, parce que moi, je suis saint. Ne souillez point vos âmes par aucun reptile qui se meut sur la terre.
Mimi ndimi Bwana Mungu wenu; jitakaseni mwe watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu. Msijitie unajisi wenyewe kwa kiumbe chochote kile kiendacho juu ya ardhi.
45 Car c’est moi qui suis le Seigneur qui vous ai retirés de la terre d’Egypte, afin que je fusse Dieu pour vous. Soyez saints, parce que moi, je suis saint.
Mimi ndimi Bwana niliyewapandisha mtoke Misri ili niwe Mungu wenu. Kwa hiyo kuweni watakatifu kwa sababu Mimi ni mtakatifu.
46 Telle est la loi des animaux et des volatiles et de toute âme vivante, qui se meut dans l’eau, et qui rampe sur la terre;
“‘Haya ndiyo masharti kuhusu wanyama, ndege, kila kiumbe hai kiendacho ndani ya maji, na kila kiumbe kiendacho juu ya ardhi.
47 Afin que vous connaissiez les différences de ce qui est pur et impur, et que vous sachiez ce que vous devez manger et ce que vous devez rejeter
Ni lazima mpambanue kati ya kilicho najisi na kilicho safi, kati ya viumbe hai vinavyoweza kuliwa na vile visivyoweza kuliwa.’”

< Lévitique 11 >