< Jean 5 >
1 Après cela se trouvait la fête des Juifs, et Jésus monta à Jérusalem.
Baada ya hapo kulikuwa na sikukuu ya Wayahudi, na Yesu alipanda kwenda Yerusalemu.
2 Or il y a à Jérusalem une piscine probatique appelée en hébreu Bethsaïda, et ayant cinq portiques.
Na kule Yerusalemu palikuwa na birika kwenye mlango wa kondoo, lililokuwa likiitwa kwa lugha ya Kiebrania Bethzatha, nalo lina matao matano.
3 Sous lesquels gisait une grande multitude de malades, d’aveugles, de boiteux, de paralytiques, attendant le mouvement des eaux.
Idadi kubwa ya wagonjwa ilikuwemo, vipofu, viwete, au waliopooza walikuwa wamelala katika matao hayo. (Zingatia: Maneno ya mstari wa 3 hayaonekani katika nakala nzuri za kale. “Wakisubiri maji kutibuliwa.”) Kwa hakikia wakati fulani malaika alishuka ndani ya Bwana na kuyatibua maji.
4 Car un ange du Seigneur descendait en un certain temps dans la piscine, et l’eau s’agitait. Et celui qui le premier descendait dans la piscine après le mouvement de l’eau, était guéri de quelque maladie qu’il fût affligé.
Kwahiyo, yule ambaye alikuwa wa kwanza kuingia ndani ya baada ya maji kutibuliwa alifanywa mzima kutokana na chochote kilichokuwa kimemshika kwa wakati huo.
5 Or il y avait là un homme qui était malade depuis trente-huit ans.
Na mtu mmoja aliyekuwa ameugua kwa muda wa miaka thelathini na minane alikuwa ndani ya matao.
6 Lorsque Jésus le vit couché et qu’il sut qu’il était malade depuis longtemps, il lui dit: Veux-tu être guéri?
Yesu alipomwona amelala ndani ya matao na baada ya kutambua kuwa amelala pale kwa muda mrefu Yesu alimwambia, “Je unataka kuwa mzima?”
7 Le malade lui répondit: Seigneur, je n’ai personne qui, lorsque l’eau est agitée, me jette dans la piscine; car, tandis que je viens, un autre descend avant moi.
Yule mgonjwa akamjibu, “Bwana sina mtu, wa kuniweka katika birika wakati maji yanapotibuliwa. Wakati ninapojaribu kuingia mtu mwingine hunitangulia.”
8 Jésus lui dit: Lève-toi, prends ton grabat et marche.
Yesu akamwambia, “Inuka na uchukue godoro lako na uende.”
9 Et aussitôt cet homme fut guéri, et il prit son grabat, et il marchait. Or c’était un jour de sabbat.
Mara yule mtu akaponywa, akachukua kintanda chake na akaenda. Na siku hiyo ilikuwa siku ya Sabato.
10 Les Juifs donc disaient à celui qui avait été guéri: C’est un jour de sabbat, il ne t’est pas permis d’emporter ton grabat.
Hivyo Wayahudi wakamwambia yule mtu aliyeponywa, “Leo ni siku ya Sabato, na hauruhusiwi kubeba godoro lako.”
11 Il leur répondit: Celui qui m’a guéri m’a dit lui-même: Prends ton grabat et marche.
Akajibu, yeye aliyeniponya ndiye aliyeniambia, “Chukua godoro lako na uende.”
12 Alors ils lui demandèrent: Qui est cet homme qui t’a dit: Prends ton grabat et marche?
Wakauliza, “Ni nani aliyekuambia 'Chukua godoro lako na uende?'''
13 Mais celui qui avait été guéri ne savait qui il était; car Jésus s’était retiré de la foule assemblée en ce lieu.
Ingawa, yule aliyeponywa hakumjua, kwa sababu Yesu alikuwa ameondoka kwa siri. Kwa kuwa kulikuwa na watu wengi katika sehemu hiyo.
14 Jésus ensuite le trouva dans le temple, et lui dit: Voilà que tu es guéri, ne pèche plus, de peur qu’il ne t’arrive quelque chose de pis.
Baada ya hapo Yesu alimkuta yule mtu hekaluni na akamwambia, “Tazama, umepona! “Usitende dhambi tena usije ukapatwa na jambo baya zaidi.”
15 Cet homme s’en alla et annonça aux Juifs que c’était Jésus qui l’avait guéri.
Yule mtu akaenda na kuwataarifu Wayahudi kuwa Yesu ndiye aliyemponya.
16 C’est pourquoi les Juifs persécutaient Jésus, parce qu’il faisait ces choses un jour de sabbat.
Hivyo, kwa sababu ya mambo hayo Wayahudi walimtesa Yesu, kwa sababu alifanya mambo haya siku ya Sabato.
17 Mais Jésus leur répondit: Mon Père agit sans cesse, et moi j’agis aussi.
Yesu akawambia, “Baba yangu anafanya kazi hata sasa nami nafanya kazi.”
18 Sur quoi les Juifs cherchaient encore plus à le faire mourir; parce que non seulement il violait le sabbat, mais qu’il disait que Dieu était son Père, se faisant ainsi égal à Dieu. Jésus répondant, leur dit:
Kwa sababu hiyo Wayahudi walizidi kumtafuta ili wamuue sio tu kwa sababu ya kuivunja Sabato, bali kwa kumwita Mungu Baba yake, akijifanya kuwa sawa na Mungu.
19 En vérité, en vérité, je vous le dis, le Fils ne peut rien faire de lui-même, si ce n’est ce qu’il voit que le Père fait; car tout ce que le Père fait, le Fils le fait pareillement.
Yesu akawajibu, “Amini, amini, Mwana hawezi kufanya kitu chochote isipokuwa kile ambacho amemwona Baba yake anakifanya, kwa kuwa chochote Baba akifanyacho ndicho na Mwana atakachofanya.
20 Car le Père aime le Fils, et lui montre tout ce qu’il fait; et il lui montrera des œuvres encore plus grandes que celles-ci, de sorte que vous en serez vous-mêmes dans l’admiration.
Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, na amwonyesha kila kitu anachokifanya na atamwonyesha mambo makubwa kuliko haya ili kwamba mzidi kushangaa.”
21 Car, comme le Père réveille les morts et les rend à la vie, ainsi le Fils vivifie ceux qu’il veut.
Kwa kuwa kama vile ambavyo Baba awafufuavyo wafu na kuwapa uzima, halikadhalika Mwana pia humpa yeyote ampendaye.
22 Le Père ne juge personne, mais il a remis tout jugement à son Fils.
Kwa kuwa Baba hamhukumu yeyote, bali amempa Mwana hukumu yote
23 Afin que tous honorent le Fils comme ils honorent le Père: qui n’honore point le Fils n’honore point le Père qui l’a envoyé.
ili kwamba wote wamuheshimu Mwana kama vile Mwana anavyomuheshimu Baba. Yeye asiyemuheshimu Mwana hamuheshimu Baba aliyemtuma.
24 En vérité, en vérité, je vous dis que celui qui écoute ma parole et croit à celui qui m’a envoyé, a la vie éternelle et ne’ vient pas en jugement; mais il a passé de la mort à la vie. (aiōnios )
Amini, amini, yeye asikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenituma anao uzima wa milele na hatahukumiwa. Badala yake, amepita kutoka mautini na kuingia uzimani. (aiōnios )
25 En vérité, en vérité, je vous le dis, vient une heure, et elle est déjà venue, où les morts entendront la voix du Fils de Dieu, et ceux qui l’auront entendue, vivront.
Amini, amini, nawambia wakati unakuja na sasa upo ambao wafu watasikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wote watakao sikia wataishi.
26 Car, comme le Père a la vie en lui-même, ainsi il a donné au Fils d’avoir la vie en lui-même;
Kwa kuwa kama vile Baba alivyo na uzima ndani yake mwenyewe,
27 Et il lui a donné le pouvoir de juger, parce qu’il est Fils de l’homme.
kadhalika amempa Mwana kuwa na uzima ndani yake, na Baba amempa Mwana mamlaka ili kwamba ahukumu kwa kuwa ni Mwana wa Adamu.
28 Ne vous en étonnez pas, parce que vient l’heure où tous ceux qui sont dans les sépulcres entendront la voix du Fils de Dieu,
Msishangazwe na hili, kwa kuwa wakati unakuja ambao wafu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake
29 Et en sortiront, ceux qui auront faille bien, pour ressusciter à la vie; mais ceux qui auront fait le mal, pour ressusciter à leur condamnation.
nao watatoka nje: kwa waliotenda mema kwa ufufuo wa uzima, na walio tenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.
30 Je ne puis rien faire de moi-même. Selon que j’entends, je juge; et mon jugement est juste, parce que je ne cherche point ma volonté, mais la volonté de celui qui m’a envoyé.
Siwezi kufanya kitu chochote kutoka kwangu mwenyewe. Kama nisikiavyo, ndivyo ninavyo hukumu na hukumu yangu ni ya haki kwa kuwa sitafuti mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenituma.
31 Si je rends témoignage de moi-même, mon témoignage n’est pas vrai.
Kama nikijishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu usingelikuwa wa kweli.
32 C’est un autre qui rend témoignage de moi, et je sais que le témoignage qu’il rend de moi est véritable.
Kuna mwingine anayeshuhudia kuhusu mimi na ninajua kwa hakika ushuhuda anaonishuhudia ni wa kweli.
33 Vous, vous avez envoyé vers Jean, et il a rendu témoignage à la vérité.
Mmetuma kwa Yohana naye ameishuhudia kweli.
34 Pour moi, ce n’est pas d’un homme que je reçois témoignage; mais je dis ceci afin que vous soyez sauvés.
Hatahivyo, ushuhuda ninaoupokea hautoki kwa mwanadamu. Ninayasema haya ili kwamba mweze kuokolewa.
35 Il était la lampe ardente et luisante, et un moment vous avez voulu vous réjouir à sa lumière.
Yohana alikuwa ni taa iliyokuwa ikiwaka na kung'ara, na mlikuwa tayari kuifurahia kwa muda kitambo nuru yake.
36 Mais moi, j’ai un témoignage plus grand que celui de Jean. Car les œuvres que mon Père m’a données à accomplir, ces œuvres que je fais moi-même, rendent témoignage de moi, que le Père m’a envoyé.
Ushuhuda nilionao ni mkuu kuliko ule wa Yohana, kwa kazi ambazo Baba amenipa kuzikamilisha, hizo kazi nizifanyazo zashuhudia kuwa Baba amenituma.
37 Et mon Père qui m’a envoyé a rendu lui-même témoignage de moi; vous n’avez jamais entendu sa voix ni vu sa figure;
Baba aliyenituma yeye mwenyewe ameshuhudia kuhusu mimi. Hamjawahi kusikia sauti yake wala kuona umbo lake wakati wowote.
38 Et vous n’avez pas sa parole demeurant en vous, parce que vous ne croyez pas à celui qu’il a envoyé.
Hamna neno lake likikaa ndani yenu kwa kuwa hamumwamini yeye aliyetumwa.
39 Scrutez les Ecritures, puisque vous pensez avoir en elles la vie éternelle, car ce sont elles qui rendent témoignage de moi; (aiōnios )
Mnayachunguza maandiko mkidhani ndani yake mna uzima wa milele, na hayo maandiko yanashuhudia habari zangu na (aiōnios )
40 Mais vous ne voulez pas venir à moi pour avoir la vie.
hamtaki kuja kwangu ili mpate uzima wa milele.
41 Je n’accepte point une gloire venant des hommes.
Sipokei sifa kutoka kwa watu,
42 Mais j’ai reconnu que vous n’avez pas l’amour de Dieu en vous.
lakini ninajua kuwa hamna upendo wa Mungu ndani yenu ninyi wenyewe.
43 Je suis venu moi-même au nom de mon Père, et vous ne me recevez point; si un autre vient en son nom, vous le recevrez.
Nimekuja kwa jina la Baba yangu, hamukuweza kunipokea. Kama mwingine akija kwa jina lake mngempokea.
44 Comment pouvez-vous croire, vous qui recevez la gloire l’un de l’autre, et ne cherchez point la gloire qui vient de Dieu seul?
Je mnawezaje kuamini ninyi ambao mnapokea sifa kutoka kwa kila mmoja wenu lakini hamtafuti sifa itokayo kwa Mungu wa pekee?
45 Ne pensez pas que ce soit moi qui doive vous accuser devant le Père: celui qui vous accuse, c’est Moïse, en qui vous espérez.
Msidhani mimi nitawashitaki mbele za Baba. Anayewashitaki ninyi ni Musa, ambaye ninyi mmeweka matumaini yenu kwake.
46 Car si vous croyiez à Moïse, vous croiriez sans doute à moi aussi, parce que c’est de moi qu’il a écrit.
Kama mngekuwa mnamwamini Musa, mngeniamini mimi kwa sababu aliandika kuhusu habari zangu.
47 Mais si vous ne croyez point à ses écrits, comment croirez-vous à mes paroles?
Kama hamuamini maandiko yake, mtawezaje kuamini maneno yangu?