< Isaïe 29 >

1 Malheur à Ariel, Ariel, cité qu’a prise d’assaut David; une année s’est jointe à une année; des solennités se sont écoulées.
Ole wako, wewe Arieli, Arieli, mji alimokaa Daudi! Ongezeni mwaka kwa mwaka, na mzunguko wa sikukuu zenu uendelee.
2 Et j’environnerai Ariel de tranchées; et elle sera triste, affligée, et elle sera pour moi comme Ariel.
Hata hivyo nitauzunguka Arieli kwa jeshi, utalia na kuomboleza, utakuwa kwangu kama mahali pa kuwashia moto madhabahuni.
3 Et je ferai comme un cercle tout autour de toi, et je poserai un rempart contre toi; et je placerai des fortifications pour ton siège.
Nitapiga kambi pande zote dhidi yako, nitakuzunguka kwa minara na kupanga mazingirwa yangu dhidi yako.
4 Tu seras humiliée, c’est du sein de la terre que tu parleras, et de la poussière que sera entendue ta parole; et sortant de la terre, ta voix sera comme celle d’un python, et de la poussière ta parole ne rendra qu’un faible son.
Utakaposhushwa, utanena kutoka ardhini, utamumunya maneno yako kutoka mavumbini. Sauti yako itatoka katika nchi kama vile ya mzimu, utanongʼona maneno yako toka mavumbini.
5 Et sera comme la poudre menue la multitude de ceux qui t’ont agitée, et comme la cendre brûlante qui se dissipe, la multitude de ceux qui contre toi ont prévalu;
Lakini adui zako wengi watakuwa kama vumbi laini, kundi la wakatili watakuwa kama makapi yapeperushwayo. Naam, ghafula, mara moja,
6 Et ce sera soudain, sur-le-champ. Et par le Seigneur des armées elle sera visitée au milieu d’un tonnerre, et d’un tremblement de terre, et de la grande voix d’un tourbillon, et d’une tempête, et de la flamme d’un feu dévorant.
Bwana Mwenye Nguvu Zote atakuja na ngurumo, tetemeko la ardhi, na kwa sauti kuu, atakuja na dhoruba, tufani na miali ya moto iteketezayo.
7 Et sera comme le songe d’une vision nocturne la multitude de toutes les nations qui ont combattu contre Ariel, et il en sera ainsi de tous ceux qui lui ont fait la guerre, et l’ont assiégée, et ont prévalu contre elle.
Kisha makundi ya mataifa yote yale yapiganayo dhidi ya Arieli, yale yanayomshambulia yeye na ngome zake, na kumzunguka kwa jeshi, watakuwa kama ilivyo ndoto, kama maono wakati wa usiku:
8 Et comme celui qui a faim songe qu’il mange, mais lorsqu’il est réveillé, son âme se trouve vide; et comme celui qui a soif songe qu’il boit, mais après qu’il est réveillé, il est las et a encore soif, et son âme est vide; ainsi sera la multitude de toutes ces nations qui ont combattu contre la montagne de Sion.
kama vile mtu aliye na njaa aotavyo kuwa anakula, lakini huamka, bado njaa yake ingalipo, kama vile mtu mwenye kiu aotavyo kuwa anakunywa maji, lakini huamka akiwa anazimia, akiwa bado angali ana kiu. Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa makundi yote ya mataifa yanayopigana dhidi ya Mlima Sayuni.
9 Soyez frappés de stupeur et admirez, soyez flottants et vacillants; enivrez-vous, mais non de vin; chancelez, mais non par l’ivresse.
Duwaeni na kushangaa, jifanyeni vipofu wenyewe na msione, leweni, lakini si kwa mvinyo, pepesukeni lakini si kwa kileo.
10 Parce que le Seigneur a répandu sur vous un esprit d’assoupissement, il fermera vos yeux; vos prophètes et vos princes qui voient des visions, il mettra sur eux un voile.
Bwana amewaleteeni usingizi mzito: Ameziba macho yenu (ninyi manabii); amefunika vichwa vyenu (ninyi waonaji).
11 Et la vision d’eux tous sera pour vous comme le livre scellé; lorsqu’on le donnera à un homme qui sait lire, on dit: Lis ce livre; et il répondra: Je ne puis, car il est scellé.
Kwa maana kwenu ninyi, maono haya yote si kitu ila maneno yaliyotiwa lakiri katika kitabu. Kama mkimpa mtu yeyote awezaye kusoma kitabu hiki, nanyi mkamwambia, “Tafadhali kisome,” yeye atajibu, “Mimi siwezi, kwa kuwa kimetiwa lakiri.”
12 Et on donnera le livre à un homme qui ne sait pas lire, et on lui dira: Lis; et il répondra: Je ne sais pas lire.
Au kama mkimpa mtu yeyote kitabu hiki asiyeweza kusoma na kumwambia, “Tafadhali kisome,” atajibu, “Mimi sijui kusoma.”
13 Et a dit le Seigneur: Parce que ce peuple s’approche de moi par sa bouche, et me glorifie par ses lèvres, mais que son cœur est loin de moi, et qu’ils m’ont craint par le commandement et les enseignements des hommes:
Bwana anasema: “Watu hawa hunikaribia kwa vinywa vyao na kuniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami. Ibada yao kwangu inatokana na maagizo waliyofundishwa na wanadamu.
14 C’est pour cela, voici que moi j’exciterai encore l’admiration de ce peuple par un miracle grand et étonnant; car la sagesse périra du milieu des sages, et l’intelligence des prudents sera obscurcie.
Kwa hiyo mara nyingine tena nitawashangaza watu hawa, kwa ajabu juu ya ajabu. Hekima ya wenye hekima itapotea, nayo akili ya wenye akili itatoweka.”
15 Malheur à vous qui êtes impénétrables de cœur, afin que vous cachiez au Seigneur un dessein; leurs œuvres sont dans les ténèbres, et ils disent: Qui nous voit, et qui nous connaît?
Ole kwa wale wanaokwenda kwenye vilindi virefu kumficha Bwana mipango yao, wafanyao kazi zao gizani na kufikiri, “Ni nani anayetuona? Ni nani atakayejua?”
16 Elle est perverse, cette pensée que vous avez; comme si l’argile se révoltait contre le potier, et lui disait: Tu ne m’as pas fait; et comme si l’œuvre disait à celui qui l’ a façonnée: Tu ne comprends pas.
Mnapindua mambo juu chini, kana kwamba mfinyanzi aweza kufikiriwa kuwa kama udongo wa mfinyanzi! Je, kile kilichofinyangwa chaweza kumwambia yule aliyekifinyanga, “Wewe hukunifinyanga mimi?” Je, chungu kinaweza kumwambia mfinyanzi, “Wewe hujui chochote?”
17 Encore un peu de temps, et le Liban ne sera-t-il pas bientôt converti en Carmel, et le Carmel ne sera-t-il pas réputé pour la forêt?
Kwa muda mfupi sana, je, Lebanoni haitageuzwa kuwa shamba lenye rutuba, na shamba lenye rutuba liwe kama msitu?
18 Et en ce jour-là, les sourds entendront les paroles d’un livre, et, affranchis des ténèbres et de l’obscurité, les yeux des aveugles verront.
Katika siku ile viziwi watasikia maneno ya kitabu, na katika utusitusi na giza macho ya kipofu yataona.
19 Et les hommes doux ajouteront à leur joie dans le Seigneur, les hommes pauvres exulteront dans le saint d’Israël;
Mara nyingine tena wanyenyekevu watafurahi katika Bwana, wahitaji watafurahi katika yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
20 Parce qu’il a disparu, celui qui prévalait, et qu’il a été détruit le railleur, et qu’ils ont été retranchés, ceux qui veillaient pour l’iniquité;
Wakatili watatoweka na wenye kudhihaki watatokomea, nao wote wenye jicho la uovu watakatiliwa mbali,
21 Qui faisaient pécher les hommes par leur parole, qui à la porte tendaient des pièges à celui qui les réfutait, et sans motif s’éloignaient du juste.
wale ambao kwa neno humfanya mtu kuwa mwenye hatia, wamtegeao mtego mtetezi katika mahakama, na kwa ushuhuda wa uongo humnyima haki yeye asiye na hatia.
22 À cause de cela, voici ce que dit, à la maison de Jacob, le Seigneur, qui a racheté Abraham: Jacob ne sera plus confondu, et son visage ne rougira plus;
Kwa hiyo hili ndilo Bwana, aliyemkomboa Abrahamu, analosema kwa nyumba ya Yakobo: “Yakobo hataaibishwa tena, wala nyuso zao hazitabadilika sura tena.
23 Mais lorsqu’il verra ses fils, ouvrages de mes mains, sanctifiant au milieu de lui mon nom, ils sanctifieront ensemble le saint de Jacob, et annonceront le Dieu d’Israël,
Wakati watakapoona watoto wao miongoni mwao, kazi ya mikono yangu, watalitakasa Jina langu takatifu; wataukubali utakatifu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Yakobo, nao watamcha Mungu wa Israeli.
24 Et ceux qui étaient égarés d’esprit recevront l’intelligence, et les murmurateurs apprendront la loi.
Wale wanaopotoka rohoni watapata ufahamu, nao wale wanaolalamika watayakubali mafundisho.”

< Isaïe 29 >