< Ézéchiel 14 >

1 Et vinrent vers moi des hommes des anciens d’Israël, et ils s’assirent devant moi.
Baadhi ya wazee wa Israeli walinijia na kuketi mbele yangu.
2 Et la parole du Seigneur me fut adressée, disant:
Ndipo neno la Bwana likanijia kusema:
3 Fils d’un homme, ces hommes ont mis leurs impuretés dans leurs cœurs, et placé le scandale de leur iniquité devant leur face; est-ce que consulté, je leur répondrai?
“Mwanadamu, watu hawa wameweka sanamu katika mioyo yao na kuweka vitu viovu vya kukwaza mbele ya macho yao. Je, kweli niwaruhusu waniulize jambo lolote?
4 À cause de cela, parle-leur, et tu leur diras: Voici ce que dit le Seigneur Dieu: Tout homme de la maison d’Israël qui aura mis ses impuretés dans son cœur, et aura placé le scandale de son iniquité devant sa face, et sera venu vers le prophète, m’interrogeant par lui, moi le Seigneur, je lui répondrai selon la multitude de ses impuretés;
Kwa hiyo sema nao uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati Mwisraeli yeyote anapoweka sanamu moyoni mwake na kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akaenda kwa nabii, Mimi Bwana nitamjibu peke yangu sawasawa na ukubwa wa ibada yake ya sanamu.
5 Afin que la maison d’Israël soit prise dans son cœur, par lequel ils se sont retirés de moi pour s’attacher à toutes leurs idoles.
Nitafanya jambo hili ili kukamata tena mioyo ya watu wa Israeli, ambao wote wameniacha kwa ajili ya sanamu zao.’
6 À cause de cela, dis à la maison d’Israël: Voici ce que dit le Seigneur Dieu: Convertissez-vous, retirez-vous de vos idoles, et de toutes vos souillures détournez vos faces.
“Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Tubuni! Geukeni kutoka kwenye sanamu zenu na mkatae matendo yenu yote ya machukizo!
7 Car tout homme de la maison d’Israël, et quiconque d’entre les prosélytes est étranger en Israël, s’il s’est détourné de moi et qu’il ait mis ses idoles dans son cœur, et qu’il ait placé le scandale de son iniquité devant sa face, et qu’il soit venu vers le prophète pour me consulter par lui; moi, le Seigneur, je lui répondrai moi-même.
“‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi katika Israeli anapojitenga nami na kujiwekea sanamu katika moyo wake na kwa hivyo kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akamwendea nabii kuuliza shauri kwangu, mimi Bwana nitamjibu mwenyewe.
8 Et je tournerai ma face contre cet homme, et je le donnerai en exemple et en proverbe, et je l’exterminerai du milieu de mon peuple; et vous saurez que je suis le Seigneur.
Nitaukaza uso wangu dhidi ya mtu huyo na kumwadhibu na kumfanya ishara kwa watu. Nitamkatilia mbali kutoka watu wangu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
9 Et lorsque le prophète a erré et qu’il a dit une parole, c’est moi, le Seigneur, qui ai trompé ce prophète; et j’étendrai ma main sur lui, et je l’effacerai du milieu de mon peuple d’Israël.
“‘Naye nabii kama atakuwa ameshawishika kutoa unabii, Mimi Bwana nitakuwa nimemshawishi nabii huyo, nami nitaunyoosha mkono wangu dhidi yake na kumwangamiza kutoka miongoni mwa watu wangu Israeli.
10 Et ils porteront leur iniquité; selon l’iniquité de celui qui consulte, ainsi sera l’iniquité du prophète;
Watachukua hatia yao, nabii atakuwa na hatia sawa na yule mtu aliyekuja kuuliza neno kwake.
11 Afin que la maison d’Israël ne s’égare plus en se retirant de moi, et qu’elle ne se souille point par toutes ses prévarications; mais qu’ils soient mon peuple, et que moi je sois leur Dieu, dit le Seigneur des armées.
“‘Ndipo watu wa Israeli hawataniacha tena, wala kujitia unajisi tena kwa dhambi zao zote. Ndipo watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao, asema Bwana Mwenyezi.’”
12 Et la parole du Seigneur me fut adressée, disant:
Neno la Bwana likanijia kusema,
13 Fils d’un homme, quant à une terre, lorsqu’elle aura péché contre moi en multipliant ses prévarications, j’étendrai ma main sur elle, et je briserai la verge de son pain, et j’enverrai sur elle la famine, et j’en tuerai les hommes et les bêtes.
“Mwanadamu, kama nchi itanitenda dhambi kwa kutokuwa waaminifu nami nikinyoosha mkono wangu dhidi yake kukatilia mbali upatikanaji wake wa chakula na kuipelekea njaa na kuua watu wake na wanyama wao,
14 Et si ces trois hommes justes, Noé, Daniel et Job, sont au milieu d’elle, eux-mêmes, par leur justice, délivreront leurs âmes, dit le Seigneur des armées.
hata kama watu hawa watatu: Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa ndani ya nchi hiyo, ndio hao tu wangeweza kujiokoa wenyewe kwa uadilifu wao, asema Bwana Mwenyezi.
15 Que si j’amène sur cette terre des bêtes cruelles, afin que je la dévaste, et qu’elle devienne inaccessible, pour qu’il n’y ait personne qui y passe à cause des bêtes;
“Au kama nikipeleka wanyama pori katika nchi hiyo yote na kuifanya isiwe na watoto, nayo ikawa ukiwa kwamba hakuna mtu apitaye katika nchi hiyo kwa sababu ya wanyama pori,
16 Si ces trois hommes y sont, je vis, moi, dit le Seigneur Dieu, ils ne délivreront ni leurs fils, ni leurs filles; mais eux seuls seront délivrés, et la terre sera désolée.
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao peke yao wangeokolewa, lakini nchi ingekuwa ukiwa.
17 Ou si j’amène le glaive sur cette terre, et que je dise au glaive: Passe par cette terre, et que j’en tue les hommes et les bêtes;
“Au kama nikileta upanga dhidi ya nchi hiyo na kusema, ‘Upanga na upite katika nchi yote,’ nami nikiua watu wake na wanyama wao,
18 Et que ces trois hommes soient au milieu d’elle; je vis, moi, dit le Seigneur Dieu, ils ne délivreront ni leurs fils, ni leurs filles; mais eux seuls seront délivrés.
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao wenyewe tu wangeokolewa.
19 Mais si j’envoie la peste sur cette terre et que je répande mon indignation sur elle par le sang, afin que j’en enlève les hommes et les bêtes;
“Au kama nikipeleka tauni katika nchi hiyo na kumwaga ghadhabu yangu juu yake kwa njia ya kumwaga damu, kuua watu wake na wanyama wao,
20 Et que Noé, Daniel et Job soient au milieu d’elle, je vis, moi, dit le Seigneur Dieu, ils ne délivreront ni fils, ni fille; mais par leur justice ils délivreront leurs propres âmes.
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kumwokoa mwana wala binti. Wao wangeweza kujiokoa wenyewe tu kwa uadilifu wao.
21 Parce que voici ce que dit le Seigneur Dieu: Que si j’envoie à Jérusalem mes quatre jugements cruels, le glaive, la famine, les bêtes mauvaises, et la peste, afin que j’en tue homme et bétail,
“Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Itakuwa vibaya kiasi gani nitakapopeleka dhidi ya Yerusalemu hukumu zangu nne za kutisha, yaani, upanga, njaa, wanyama pori na tauni, ili kuua watu wake na wanyama wao!
22 Cependant il y sera laissé des hommes qui se sauveront, et feront sortir leurs fils et leurs filles; voilà qu’eux-mêmes viendront vers vous, et que vous verrez leur voie et leurs inventions, et que vous serez consolés du mal que j’aurai amené sur Jérusalem, et de tous les fléaux dont je l’aurai accablée.
Lakini watakuwepo wenye kuokoka, wana na binti wataletwa kutoka nje ya nchi hiyo. Watawajia ninyi, nanyi mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, mtafarijika kuhusu maafa niliyoleta juu ya Yerusalemu, kwa ajili ya yale yote niliyoleta juu yake.
23 Et ils vous consoleront, lorsque vous verrez leur voie et leurs inventions; et vous reconnaîtrez que ce n’est pas sans raison que j’aurai fait à Jérusalem tout ce que j’y aurai lait, dit le Seigneur Dieu.
Mtafarijika wakati mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, kwa kuwa mtajua kwamba sikufanya lolote ndani yake bila sababu, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ézéchiel 14 >