< Deutéronome 18 >

1 Les prêtres, les Lévites, et tous ceux qui sont de la même tribu n’auront point de part et d’héritage avec le reste d’Israël, parce qu’ils mangeront des sacrifices du Seigneur et de ses oblations;
Makuhani ambao ni Walawi, yaani kabila lote la Lawi, hawatakuwa na mgawo wala urithi pamoja na Israeli. Wataishi kwa sadaka zitolewazo kwa ajili ya Bwana za kuteketezwa kwa moto, kwa maana huo ndio urithi wao.
2 Et ils ne recevront rien autre chose de la possession de leurs frères; car le Seigneur lui-même est leur héritage, comme il leur a dit.
Hawatakuwa na urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.
3 Voici le droit des prêtres sur le peuple, et sur ceux qui offrent les victimes; soit qu’ils immolent un bœuf ou une brebis, ils donneront au prêtre l’épaule et la poitrine;
Hili ndilo fungu la makuhani kutoka kwa watu watakaotoa dhabihu ya fahali au kondoo: mguu wa mbele, mataya na matumbo.
4 Les prémices du blé, du vin, de l’huile et une partie de la tonte des brebis;
Mtawapa malimbuko ya nafaka zenu, divai mpya, mafuta na sufu ya kwanza kutoka manyoya ya kondoo zenu,
5 Car c’est lui que le Seigneur ton Dieu a choisi d’entre toutes les tribus, afin qu’il assiste devant le Seigneur, et qu’il exerce le ministère en son nom, lui et ses enfants pour toujours.
kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewachagua pamoja na wazao wao kutoka makabila yenu kusimama na kuhudumu katika jina la Bwana siku zote.
6 Si un Lévite sort d’une de vos villes de tout Israël, dans laquelle il habite, et qu’il veuille et désire venir au lieu qu’aura choisi le Seigneur,
Ikiwa Mlawi atahama kutoka mmojawapo ya miji yenu popote katika Israeli ambapo anaishi, akaja kwa moyo wote mahali ambapo Bwana atapachagua,
7 Il exercera le ministère au nom du Seigneur son Dieu, comme tous ses frères les Lévites, qui assisteront en ce temps-là devant le Seigneur.
anaweza akahudumu katika jina la Bwana Mungu wake kama Walawi wenzake wote wanaohudumu hapo mbele za Bwana.
8 Il recevra la même part d’aliments que tous les autres, outre ce qu’il lui est dû dans sa ville de la succession paternelle.
Atashiriki sawa katika mafao yao, hata kama amepokea fedha kutoka mauzo ya mali ya jamaa yake.
9 Quand tu seras entré dans la terre que le Seigneur ton Dieu te donnera, prends garde de vouloir imiter les abominations de ces nations;
Wakati mtakapoingia katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msijifunze kuiga njia za machukizo za mataifa ya huko.
10 Et qu’il ne se trouve au milieu de toi personne qui purifie son fils ou sa fille, les faisant passer par le feu, ou qui interroge des devins, et qui observe les songes et les augures, ni qui use de maléfices,
Asionekane mtu yeyote miongoni mwenu ampitishaye mwanawe au binti yake katika moto, atakayefanya uaguzi, ulozi, anayetabiri nyakati, anayejishughulisha na uchawi,
11 Ni qui soit enchanteur, ni qui consulte ceux qui ont l’esprit de python et les devins, ou qui demande aux morts la vérité;
wala arogaye kwa kupiga mafundo, wala mwaguzi au anayeabudu mizimu, wala awaombaye wafu.
12 Car le Seigneur a toutes ces choses en abomination, et c’est à cause de ces sortes de crimes qu’il détruira ces nations à ton entrée.
Mtu yeyote afanyaye mambo haya ni chukizo kwa Bwana, tena ni kwa sababu ya matendo haya ya kuchukiza wayafanyayo ndiyo maana Bwana Mungu wenu atayafukuza mataifa hayo mbele yenu.
13 Tu seras parfait et sans tache avec le Seigneur ton Dieu.
Kamwe msilaumiwe mbele za Bwana Mungu wenu.
14 Ces nations dont tu posséderas la terre, écoutent les augures et les devins; mais toi, tu as été instruit autrement par le Seigneur ton Dieu.
Mataifa mtakayowafukuza husikiliza wale wafanyao ulozi na uaguzi. Lakini kwenu ninyi, Bwana Mungu wenu hajawaruhusu kufanya hivyo.
15 Le Seigneur ton Dieu te suscitera un Prophète de ta nation et d’entre tes frères, comme moi; c’est lui que tu écouteras;
Bwana Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu wenyewe. Msikilizeni yeye.
16 Comme tu as demandé au Seigneur ton Dieu à Horeb, quand l’assemblée fut réunie, et comme tu as dit: Que je n’entende plus la voix du Seigneur mon Dieu, et que je ne voie plus ce très grand feu, afin que je ne meure pas.
Kwa kuwa hivi ndivyo mlivyomwomba Bwana Mungu wenu kule Horebu siku ile ya kusanyiko, wakati mliposema, “Na tusiisikie sauti ya Bwana Mungu wetu, wala kuuona moto huu mkubwa tena, ama sivyo tutakufa.”
17 Et le Seigneur me répondit: Ils ont bien dit toutes choses.
Bwana akaniambia: “Wanachosema ni vyema.
18 Je leur susciterai un prophète du milieu de leurs frères, semblable à toi, et je mettrai mes paroles en sa bouche, et il leur dira tout ce que je lui aurai ordonné.
Nitawainulia nabii kama wewe kutoka miongoni mwa ndugu zao; nitaweka maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia kila kitu nitakachomwamuru.
19 Or, celui qui ne voudra pas écouter ses paroles, qu’il dira en mon nom, c’est moi qui m’en vengerai.
Kama mtu yeyote hatasikiliza maneno yangu ambayo huyo nabii atayasema kwa Jina langu, mimi mwenyewe nitamwajibisha.
20 Mais le prophète qui, corrompu par orgueil, voudra dire en mon nom des choses que je ne lui ai pas ordonné de dire, ou qui parlera au nom de dieux étrangers, sera mis à mort.
Lakini nabii ambaye atathubutu kusema kwa Jina langu kitu chochote ambacho sikumwamuru akiseme, au nabii ambaye husema kwa jina la miungu mingine ni lazima auawe.”
21 Que si tu réponds secrètement par la pensée: Comment puis-je discerner la parole que le Seigneur n’a pas dite?
Mnaweza kuulizana wenyewe, “Tutawezaje kujua wakati ujumbe haukusemwa na Bwana?”
22 Tu auras ce signe: Ce que ce prophète aura prédit au nom du Seigneur, n’arrivant pas, le Seigneur ne l’a pas dit, mais c’est par l’enflure de son esprit que le prophète l’a inventé: et c’est pourquoi tu ne le craindras pas.
Ikiwa kile nabii anachotangaza kwa jina la Bwana hakikutokea au kutimia, huo ni ujumbe ambao Bwana hakusema. Nabii huyo amesema kwa ujuaji. Msimwogope huyo.

< Deutéronome 18 >