< Daniel 12 >

1 Mais en ce temps-là s’élèvera Michel le grand prince, qui est pour les fils de ton peuple; et viendra un temps, tel qu’il n’y en a pas eu depuis que les nations ont commencé d’être jusqu’alors. Et en ce temps-là, sera sauvé quiconque de ton peuple sera trouvé écrit dans le livre.
“Katika wakati huo Mikaeli, mtawala mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwako wakati wa taabu ambao haujatokea tangu mwanzo wa mataifa hadi wakati huo. Lakini wakati huo, watu wako, kila mmoja ambaye jina lake litakutwa limeandikwa kwenye kitabu, ataokolewa.
2 Et beaucoup de ceux qui dorment dans la poussière de la terre s’éveilleront: les uns pour la vie éternelle, et les autres pour l’opprobre, afin qu’ils le voient toujours.
Wengi ambao wamelala kwenye mavumbi wataamka, baadhi yao kwa uzima wa milele, wengine kwa aibu na kudharauliwa milele.
3 Or ceux qui auront été savants brilleront comme la splendeur du firmament, et ceux qui enseignent la justice à un grand nombre, seront comme les étoiles dans les perpétuelles éternités.
Wale wenye hekima watangʼaa kama mwanga wa mbingu, nao wale ambao huwaongoza wengi kutenda haki, watangʼaa kama nyota milele na milele.
4 Mais toi, Daniel, ferme les paroles, et scelle le livre jusqu’au temps déterminé; beaucoup le parcourront et la science sera multipliée.
Lakini wewe Danieli, yafunge na kuyatia muhuri maneno ya kitabu hiki mpaka wakati wa mwisho. Wengi watakwenda huku na huko, na maarifa yataongezeka.”
5 Et je vis, moi Daniel, et voilà comme deux autres hommes qui se tenaient debout: l’un en deçà, sur la rive du fleuve, et l’autre au-delà, sur la rive du fleuve.
Ndipo mimi Danieli nikaangalia, nako mbele yangu walisimama wengine wawili, mmoja katika ukingo huu wa mto, na mwingine ukingo wa pili wa mto.
6 Et je dis à l’homme qui était vêtu de lin, qui se tenait sur les eaux du fleuve: Quand sera la fin de ces prodiges?
Mmoja wao akasema na yule mtu aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, “Je, itachukua muda gani kabla mambo haya ya kushangaza hayajatimizwa?”
7 Et j’entendis l’homme qui était vêtu de lin, qui se tenait debout sur les eaux du fleuve, lorsqu’il eut élevé sa main droite et sa main gauche au ciel, et qu’il eut juré par celui qui vit éternellement, en disant: Dans un temps, et deux temps, et la moitié d’un temps. Et quand la dispersion de l’assemblée du peuple saint sera accomplie, toutes ces choses seront accomplies.
Kisha mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, akainua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni, nami nikamsikia akiapa kwa jina lake yeye aishiye milele, akisema, “Itakuwa wakati, nyakati mbili, na nusu wakati. Nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimevunjwa kabisa, ndipo mambo haya yote yatakapotimizwa.”
8 Et moi j’entendis et ne compris pas. Et je dis: Mon Seigneur, qu’est-ce qui sera après ceci?
Nilisikia, lakini sikuelewa. Kwa hiyo nikauliza, “Bwana wangu, matokeo ya haya yote yatakuwa nini?”
9 Et il dit: Va, Daniel; car les paroles sont fermées et scellées jusqu’au temps fixé.
Akajibu, “Danieli, enenda zako, kwa sababu maneno haya yamefungwa na kutiwa muhuri mpaka wakati wa mwisho.
10 Beaucoup seront purifiés, et deviendront blancs et éprouvés comme le feu, et les impies agiront avec impiété, et aucun des impies ne comprendra; mais les savants comprendront.
Wengi watatakaswa, na kuondolewa mawaa na kufanywa safi, lakini waovu wataendelea kuwa waovu. Hakuna mmoja wa waovu atakayefahamu, lakini wale wenye hekima watafahamu.
11 Et depuis le temps qu’aura été aboli le sacrifice perpétuel, et qu’aura été établie l’abomination de la désolation, il s’écoulera mille deux cent quatre-vingt-dix jours.
“Tangu wakati ule wa kukomeshwa dhabihu ya kila siku na kusimamishwa kwa chukizo la uharibifu, kutakuwako siku 1,290.
12 Bien heureux celui qui attend et qui parvient jusqu’à mille trois cent trente-cinq jours.
Amebarikiwa mtu yule atakayevumilia hadi kufikia mwisho wa hizo siku 1,335.
13 Mais toi, va jusqu’au terme fixé, et tu seras en repos, et tu demeureras dans ton état jusqu’à la fin des jours.
“Lakini wewe, enenda zako mpaka mwisho. Utapumzika, nawe ndipo mwisho wa hizo siku utafufuka ili kuupokea urithi uliowekewa.”

< Daniel 12 >