< 2 Samuel 7 >

1 Or il arriva que lorsque le roi se fut établi en sa maison, et que le Seigneur lui eut donné le repos de toutes parts du côté de tous ses ennemis,
Baada ya mfalme kuingia rasmi katika jumba lake la kifalme, naye Bwana akiwa amemstarehesha pande zote mbali na adui zake,
2 Il dit à Nathan le prophète: Vois-tu que j’habite dans une maison de cèdre, et que l’arche de Dieu est placée au milieu des peaux?
akamwambia nabii Nathani, “Mimi hapa, ninaishi katika jumba la kifalme la mierezi, wakati Sanduku la Mungu limebaki katika hema.”
3 Et Nathan répondit au roi: Tout ce qui est en votre cœur, allez, faites-le, parce que le Seigneur est avec vous.
Nathani akamjibu mfalme, “Lolote ulilo nalo moyoni, endelea ukalifanye, kwa maana Bwana yu pamoja nawe.”
4 Or il arriva pendant cette nuit-là, que voilà que la parole du Seigneur vint à Nathan, disant:
Usiku ule neno la Bwana likamjia Nathani, kusema:
5 Va, et dis à mon serviteur David: Voici ce que dit le Seigneur: Est-ce que tu ne me bâtiras point une maison pour l’habiter?
“Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ewe ndiwe wa kunijengea mimi nyumba ili nikae ndani yake?
6 Car je n’ai pas habité dans une maison, depuis le jour que j’ai retiré les enfants d’Israël de la terre d’Egypte, jusqu’à ce jour-ci; mais je marchais dans un tabernacle, dans une tente.
Sijakaa ndani ya nyumba tangu siku niliyowaleta Waisraeli kutoka Misri hadi leo. Nimekuwa nikitembea kutoka mahali pamoja hadi mahali pengine ndani ya hema kama makao yangu.
7 Dans tous les lieux par où j’ai passé avec tous les enfants d’Israël, est-ce que j’ai jamais dit à une des tribus d’Israël, à laquelle j’ai ordonné de conduire mon peuple Israël, disant: Pourquoi ne m’avez-vous pas bâti une maison de cèdre?
Popote nilipotembea pamoja na Waisraeli wote, je, nimewahi kumwambia kiongozi wao yeyote niliyemwamuru kuwachunga watu wangu Israeli, “Kwa nini hujanijengea nyumba ya mierezi?”’
8 Et maintenant tu diras ceci à mon serviteur David: Voici ce que dit le Seigneur des armées: C’est moi qui t’ai tiré des pâturages, lorsque tu suivais les troupeaux, afin que tu fusses chef sur mon peuple Israël;
“Sasa basi, mwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Nilikutoa wewe kutoka machungani na kutoka kuandama kundi la kondoo na mbuzi ili kuwaongoza watu wangu Israeli.
9 Et j’ai été avec toi dans tous les lieux où tu as marché, et j’ai tué tous tes ennemis devant toi, et j’ai rendu ton nom grand, comme le nom des grands qui sont sur la terre.
Nimekuwa pamoja nawe popote ulipokwenda, nami nimekuondolea mbali adui zako wote mbele yako. Basi nitalifanya jina lako kuwa kuu kama majina ya watu walio wakuu sana duniani.
10 Et je fixerai un lieu à mon peuple Israël, et je le planterai, et il y habitera, et il ne sera plus troublé; et des fils d’iniquité ne recommenceront pas à l’affliger, comme auparavant,
Nami nitawapatia watu wangu Israeli mahali niwapande humo ili kwamba wawe na nyumbani kwao wenyewe wasisumbuliwe tena. Watu waovu hawatawaonea tena, kama walivyofanya mwanzoni,
11 Depuis le jour que j’ai établi des juges sur mon peuple Israël; et je te donnerai le repos du côté de tous tes ennemis; et le Seigneur t’annonce qu’il te fera une maison.
na kama walivyofanya tangu mwanzo wakati nilipowaweka viongozi juu ya watu wangu Israeli. Pia nitawapa raha mbele ya adui zenu wote. “‘Bwana akuambia kwamba Bwana mwenyewe atakujengea nyumba.
12 Et lorsque tes jours seront accomplis, et que tu dormiras avec tes pères, je te susciterai un fils après toi, lequel sortira de tes entrailles, et j’affermirai son règne.
Siku zako zitakapokwisha nawe ulale pamoja na baba zako, nitainua mzao wako aingie mahali pako, ambaye atatoka viunoni mwako, nami nitauimarisha ufalme wake.
13 C’est lui qui bâtira une maison à mon nom, et j’établirai fermement le trône de son royaume pour toujours.
Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya Jina langu, nami nitaimarisha kiti cha enzi cha ufalme wake milele.
14 Moi je serai son père, et lui sera mon fils; et s’il fait quelque chose iniquement, je le châtierai avec une verge d’homme, et avec des plaies des enfants des hommes.
Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu. Atakapokosea nitamwadhibu kwa fimbo ya wanadamu, kwa adhabu ya kupigwa na wanadamu.
15 Mais ma miséricorde, je ne la retirerai pas de lui, comme je l’ai retirée de Saül, que j’ai écarté de ma face.
Lakini upendo wangu kamwe hautaondolewa kwake, kama nilivyouondoa kwa Sauli, niliyemwondoa atoke mbele yako.
16 Et ta maison sera fidèle, et ton royaume éternellement devant ta face, et ton trône sera ferme à jamais.
Nyumba yako na ufalme wako utadumu milele mbele zangu, kiti chako cha enzi kitafanywa imara milele.’”
17 C’est selon toutes ces paroles, et suivant toute cette vision, que Nathan parla à David.
Nathani akamwarifu Daudi maneno yote ya maono haya.
18 Or, le roi David entra, et il s’assit devant le Seigneur et dit: Que suis-je moi, Seigneur Dieu, et quelle est ma maison, pour que vous m’ayez conduit jusque-là?
Ndipo Mfalme Daudi akaingia ndani, akaketi mbele za Bwana, akasema: “Ee Bwana Mwenyezi, mimi ni nani, na jamaa yangu ni nini, hata umenileta mpaka hapa nilipo?
19 Mais cela même a paru peu, en votre présence, Seigneur Dieu, si vous ne parliez aussi de la maison de votre serviteur pour un long avenir; car c’est la loi d’Adam, Seigneur Dieu.
Naam, kana kwamba hili halitoshi machoni pako, Ee Bwana Mwenyezi, wewe umenena pia kuhusu siku zijazo za nyumba ya mtumishi wako. Je, hii ndiyo njia yako ya kawaida ya kushughulika na mwanadamu, Ee Bwana Mwenyezi?
20 Que pourra donc encore ajouter David, pour vous parler? car vous, Seigneur Dieu, vous connaissez votre serviteur.
“Je, Daudi aweza kukuambia nini zaidi? Kwa maana unamjua mtumishi wako, Ee Bwana Mwenyezi.
21 À cause de votre parole et selon votre cœur vous avez fait toutes ces grandes œuvres, afin d’en donner connaissance à votre serviteur.
Kwa ajili ya neno lako na kwa mapenzi yako, umefanya jambo hili kubwa na kulifanya lijulikane na lifahamike kwa mtumishi wako.
22 C’est pour cela que vous avez été exalté, Seigneur Dieu; car nul n’est semblable à vous, et il n’y a point de Dieu hors vous, selon tout ce que nous avons entendu de nos oreilles.
“Tazama jinsi ulivyo mkuu, Ee Bwana Mwenyezi! Hakuna mwingine kama wewe, wala hakuna Mungu ila wewe, kama vile tulivyosikia kwa masikio yetu wenyewe,
23 Mais quelle est la nation sur la terre comme votre peuple d’Israël, à cause de laquelle Dieu est allé pour la racheter comme son peuple, pour se faire un nom, et pour opérer au milieu d’eux des œuvres grandes et terribles sur la terre, à la face de votre peuple, que vous vous êtes racheté de l’Egypte, frappant une nation et son dieu.
Naye ni nani aliye kama watu wako Israeli, taifa pekee duniani ambalo Mungu alitoka kwenda kulikomboa kwa ajili yake mwenyewe, na kujifanyia jina mwenyewe, kwa kufanya maajabu makubwa na ya kutisha kwa kuwafukuza mataifa na miungu yao mbele ya watu wako, ambao uliwakomboa kutoka Misri?
24 Car vous vous êtes assuré de votre peuple Israël comme d’un peuple perpétuel; et vous. Seigneur Dieu, vous êtes devenu leur Dieu.
Umeimarisha watu wako Israeli hasa kama watu wako mwenyewe milele, nawe, Ee Bwana, umekuwa Mungu wao.
25 Maintenant donc. Seigneur Dieu, suscitez pour toujours la parole que vous avez dite sur votre serviteur et sur sa maison, et faites comme vous avez parlé,
“Basi sasa, Bwana, ukaitimize ahadi uliyosema kuhusu mtumishi wako na nyumba yake milele. Fanya kama ulivyoahidi,
26 Afin que votre nom soit exalté à jamais, et que l’on dise: Le Seigneur Dieu des armées est Dieu sur Israël. Et la maison de votre serviteur David sera fermement établie devant le Seigneur,
ili kwamba jina lako litukuke milele. Ndipo watu watasema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ni Mungu juu ya Israeli!’ Nayo nyumba ya mtumishi wako Daudi itakuwa imara mbele zako.
27 Parce que c’est vous, Seigneur des armées, Dieu d’Israël, qui avez ouvert l’oreille de votre serviteur, disant: Je te bâtirai une maison; à cause de cela votre serviteur a trouvé son cœur pour vous adresser cette prière.
“Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, umelifunua hili kwa mtumishi wako, ukisema, ‘Nitakujengea nyumba.’ Hivyo mtumishi wako amepata ujasiri kukuletea dua hii.
28 Maintenant donc, Seigneur Dieu, vous êtes Dieu, et vos paroles seront véritables; car vous avez dit à votre serviteur ces bonnes choses.
Ee Bwana Mwenyezi, wewe ndiwe Mungu! Maneno yako ndiyo kweli, nawe umemwahidi mtumishi wako mambo haya mazuri.
29 Commencez-donc, et bénissez la maison de votre serviteur, afin qu’elle soit à jamais devant vous, parce que c’est vous. Seigneur Dieu, qui avez parlé, et c’est de votre bénédiction que sera bénie la maison de votre serviteur à jamais.
Sasa naomba uwe radhi kuibariki nyumba ya mtumishi wako, ili idumu mbele zako milele, kwa maana wewe, Ee Bwana Mwenyezi, umesema, na kwa baraka zako nyumba ya mtumishi wako itaendelea kubarikiwa milele.”

< 2 Samuel 7 >