< 2 Samuel 4 >

1 Or, Isboseth, fils de Saül, apprit qu’Abner avait succombé à Hébron, et ses mains perdirent leur force, et tout Israël fut troublé.
Ish-Boshethi mwana wa Sauli aliposikia kwamba Abneri amekufa huko Hebroni, akakosa ujasiri, nayo Israeli yote wakatiwa hofu kuu.
2 Cependant il y avait deux hommes, chefs de voleurs, auprès du fils de Saül; le nom de l’un était Baana, et le nom de l’autre, Réchab, fils de Remmon, le Bérothite, des fils de Benjamin, puisque Béroth aussi était réputée de Benjamin.
Basi mwana wa Sauli alikuwa na watu wawili waliokuwa viongozi wa vikundi vya uvamizi. Mmoja aliitwa Baana na mwingine Rekabu, waliokuwa wana wa Rimoni, Mbeerothi, kutoka kabila la Benyamini. Beerothi alihesabiwa kuwa sehemu ya Benyamini,
3 Et les Bérothites s’enfuirent à Géthaïm, et ils ont été là comme étrangers jusqu’à ce temps-ci.
kwa sababu watu wa Beerothi walikimbilia huko Gitaimu na wameishi huko kama wageni mpaka siku hii ya leo.
4 Or, Jonathas, fils de Saül, avait un fils, infirme des pieds; il avait cinq ans, quand vint de Jezraël la nouvelle touchant Saül et Jonathas; c’est pourquoi sa nourrice, le prenant, s’enfuit; et, comme elle se hâtait de fuir, il tomba, et devint boiteux; et il eut pour nom Miphiboseth.
(Yonathani mwana wa Sauli alikuwa na mwana aliyekuwa mlemavu miguu yote miwili. Alikuwa na miaka mitano wakati habari kuhusu Sauli na Yonathani zilipofika kutoka Yezreeli. Yaya wake akambeba ili kukimbia, lakini yaya alipokuwa anaharakisha kuondoka, mtoto alianguka akawa kiwete. Jina lake aliitwa Mefiboshethi.)
5 Etant donc venus, les fils de Remmon, le Bérothite, Réchab et Baana, entrèrent, à la chaleur du jour, dans la maison d’Isboseth, qui dormait sur son lit à midi; et la portière de la maison, vannant du blé, s’endormit.
Basi Rekabu na Baana, wana wa Rimoni Mbeerothi wakaenda nyumbani kwa Ish-Boshethi, nao walifika huko wakati alipokuwa kwenye mapumziko yake ya mchana.
6 Ils entrèrent donc dans la maison secrètement, prenant des épis de froment; et Réchab et son frère le frappèrent à l’aîne, et s’enfuirent,
Wakaingia kwenye chumba cha ndani kana kwamba wanachukua ngano, wakamchoma Ish-Boshethi mkuki wa tumboni. Ndipo Rekabu na Baana nduguye wakatoroka.
7 Ainsi lorsqu’ils furent entrés dans la maison, Isboseth dormait sur son lit dans sa chambre à coucher; et, le frappant, ils le tuèrent; puis, sa tête enlevée, ils s’en allèrent par la voie du désert, durant toute la nuit,
Walikuwa wameingia ndani ya nyumba wakati alipokuwa amelala kitandani chumbani kwake. Baada ya kumchoma mkuki na kumuua, walikata kichwa chake. Wakiwa wamekichukua, walitembea usiku kucha kwa njia ya Araba.
8 Et ils apportèrent la tête d’Isboseth à David à Hébron, et ils dirent au roi: Voici la tête d’Isboseth, fils de Saül, votre ennemi, qui cherchait votre âme: et le Seigneur a vengé aujourd’hui mon seigneur le roi de Saül et de sa race.
Wakamletea Daudi kichwa cha Ish-Boshethi huko Hebroni, wakamwambia mfalme, “Hiki hapa kichwa cha Ish-Boshethi mwana wa Sauli, adui yako, aliyejaribu kuondoa uhai wako. Siku hii ya leo Bwana amemlipia kisasi mfalme bwana wangu dhidi ya Sauli na mzao wake.”
9 Mais David répondant à Réchab et à Baana son frère, fils de Remmon, le Bérothite, il leur dit: Le Seigneur vit, lui qui a délivré mon âme de toute angoisse!
Daudi akawajibu Rekabu na Baana nduguye, wana wa Rimoni, Mbeerothi, akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, ambaye ameniokoa kutoka taabu zote,
10 Celui qui m’avait annoncé et dit: Saül est mort, et qui pensait qu’il annonçait une heureuse nouvelle, je le pris et le tuai à Siceleg, lui à qui il fallait donner une récompense pour son message;
yule mtu aliponiambia, ‘Sauli amekufa,’ akadhani ananiletea habari njema, nilimkamata, nikamuua huko Siklagi. Hiyo ndiyo zawadi niliyompa kwa ajili ya taarifa yake!
11 Combien plus maintenant que des hommes impies ont tué l’homme innocent, dans sa maison, sur son lit, demanderai-je son sang à votre main, et vous enlèverai-je de la terre!
Je, ni mara ngapi zaidi wakati watu waovu wamemuua mtu asiye na hatia akiwa ndani ya nyumba yake mwenyewe na kwenye kitanda chake mwenyewe? Je, sasa nisidai damu yake mikononi mwenu na kuwaondoa duniani?”
12 C’est pourquoi David ordonna à ses serviteurs, et ils les tuèrent; et coupant leurs mains et leurs pieds, ils les suspendirent! à la piscine, à Hébron; mais la tête d’Isboseth, ils la prirent et l’ensevelirent dans le sépulcre d’Abner à Hébron.
Kwa hiyo Daudi akawaamuru watu wake, wakawaua. Wakakata mikono yao na miguu, na kutundika viwiliwili vyao kando ya dimbwi huko Hebroni. Lakini wakakichukua kichwa cha Ish-Boshethi na kukizika katika kaburi la Abneri huko Hebroni.

< 2 Samuel 4 >