< 2 Rois 1 >

1 Or, après la mort d’Achab, Moab se révolta contre Israël.
Baada ya kifo cha Mfalme Ahabu, nchi ya Moabu iliasi dhidi ya Israeli.
2 Et Ochozias tomba par la fenêtre de sa chambre haute qu’il avait à Samarie, et il fut malade, et il envoya des messagers, leur disant: Allez, consultez Béelzébub, le dieu d’Accaron, pour savoir si je pourrai réchapper de cette maladie.
Basi Ahazia alikuwa ameanguka huko Samaria kutoka baraza ya chumba chake cha juu, akaumia. Hivyo akatuma wajumbe, akiwaambia, “Nendeni mkaulize kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni, mkaone kama nitapona kutokana na kuumia huku.”
3 Mais un ange du Seigneur parla à Élie, le Thesbite, disant: Lève-toi, et monte à la rencontre des messagers du roi de Samarie, et tu leurs diras: Est-ce qu’il n’y a pas un Dieu dans Israël, pour que vous alliez consulter Béelzébub, le dieu d’Accaron?
Lakini malaika wa Bwana akamwambia Eliya, Mtishbi, “Panda ukakutane na wajumbe wa mfalme wa Samaria, uwaulize, ‘Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana mnakwenda kumuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni?’
4 C’est pourquoi voici ce que dit le Seigneur: Tu ne descendras point du lit sur lequel tu es monté; mais tu mourras de mort. Et Élie s’en alla.
Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana, ‘Hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!’” Hivyo Eliya akaenda.
5 Et les messagers revinrent vers Ochozias. Il leur dit: Pourquoi êtes-vous revenus?
Wajumbe waliporudi kwa mfalme, akawauliza, “Kwa nini mmerudi?”
6 Mais eux lui répondirent: Un homme est venu à notre rencontre, et nous a dit: Allez, et retournez vers le roi qui vous a envoyés, et vous lui direz: Voici ce que dit le Seigneur: Est-ce parce qu’il n’y a pas un Dieu dans Israël, que tu envoies pour que soit consulté Béelzébub, le dieu d’Accaron? C’est pourquoi tu ne descendras point du lit sur lequel tu es monté; mais tu mourras de mort.
Wakamjibu, “Mtu fulani alikuja kukutana nasi, naye akatuambia, ‘Rudini kwa mfalme aliyewatuma na mkamwambie, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana unawatuma watu kwenda kuuliza kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa hiyo hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”’”
7 Le roi leur demanda: Quelle figure et quel vêtement a cet homme qui est venu à votre rencontre, et qui vous a dit ces paroles?
Mfalme akawauliza, “Alikuwa mtu wa namna gani ambaye mlikutana naye, akawaambia hili?”
8 Et ceux-ci lui répondirent: C’est un homme couvert de poil, et ceint sur les reins d’une ceinture de peau. Le roi dit: C’est Élie, le Thesbite.
Wakamjibu, “Alikuwa mtu aliyekuwa na vazi la manyoya na mkanda wa ngozi kiunoni mwake.” Mfalme akasema, “Huyo alikuwa ni Eliya, Mtishbi.”
9 Et il envoya vers lui un chef de cinquante soldats, et les cinquante soldats qui étaient sous lui. Ce chef monta vers Élie, et il lui dit pendant qu’il était sur le sommet de la montagne: Homme de Dieu, le roi commande que vous descendiez.
Ndipo mfalme akamtuma mkuu mmoja wa kikosi pamoja na kikosi chake cha askari hamsini kwa nabii Eliya. Yule mkuu wa kikosi akamwendea Eliya, aliyekuwa ameketi juu ya kilima, na kumwambia, “Mtu wa Mungu, mfalme anasema, ‘Shuka chini!’”
10 Et répondant, Élie dit au chef des cinquante soldats: Si je suis homme de Dieu, qu’il descende un feu du ciel, et qu’il te dévore, toi et tes cinquante. C’est pourquoi il descendit un feu du ciel, et il le dévora, lui et les cinquante qui étaient avec lui.
Eliya akamjibu yule mkuu wa kikosi, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza yule mkuu wa kikosi pamoja na watu wake.
11 Et de nouveau le roi lui envoya un autre chef de cinquante soldats, et cinquante soldats avec lui. Celui-ci dit à Élie: Homme de Dieu, voici ce que dit le roi: Hâte-toi, descends.
Aliposikia hili, mfalme akatuma kwa Eliya mkuu wa kikosi mwingine na askari wake hamsini. Yule mkuu wa kikosi akamwambia Eliya, “Mtu wa Mungu, hili ndilo asemalo mfalme, ‘Shuka chini mara moja!’”
12 Et répondant, Élie dit: Si moi je suis homme de Dieu, qu’il descende un feu du ciel, et qu’il te dévore, toi et tes cinquante. Il descendit donc un feu du ciel, et il le dévora, lui et ses cinquante.
Eliya akajibu, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza yeye na watu wake hamsini.
13 Il envoya encore un troisième chef de cinquante soldats, et les cinquante soldats qui étaient avec lui. Celui-ci, étant venu devant Élie, fléchit les genoux, l’implora, et dit: Homme de Dieu, ne dédaignez point mon âme et les âmes de vos serviteurs qui sont avec moi.
Hivyo mfalme akatuma mkuu wa kikosi wa tatu na watu wake hamsini. Huyu mkuu wa kikosi wa tatu akapanda na kupiga magoti mbele ya Eliya, akiomba, “Mtu wa Mungu, tafadhali niachie uhai wangu na uhai wa hawa watu hamsini, watumishi wako!
14 Voilà qu’il est descendu un feu du ciel, et il a dévoré les deux premiers chefs de cinquante soldats et les cinquante soldats qui étaient avec chacun d’eux; mais maintenant je vous conjure d’avoir pitié de mon âme.
Tazama, moto umeshuka kutoka mbinguni na kuwateketeza wale wakuu wa vikosi viwili vya kwanza pamoja na watu wao. Lakini sasa niachie uhai wangu!”
15 Or l’ange du Seigneur parla à Élie, disant: Descends avec lui, ne crains point. Il se leva donc, et descendit avec lui vers le roi,
Malaika wa Bwana akamwambia Eliya, “Shuka pamoja naye, usimwogope.” Hivyo Eliya akainuka na kushuka pamoja naye kwa mfalme.
16 Et il lui dit: Voici ce que dit le Seigneur: Parce que tu as envoyé des messagers pour consulter Béelzébub, le dieu d’Accaron, comme s’il n’y avait pas un Dieu dans Israël que tu pusses consulter, tu ne te lèveras point du lit sur lequel tu es monté, mais tu mourras de mort.
Akamwambia mfalme, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli wa kumuuliza habari, ndiyo maana ukatuma wajumbe kuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa sababu umefanya hili, kamwe hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”
17 Il mourut donc, selon la parole du Seigneur qu’avait dite Élie. Et Joram, son frère, régna en sa place, la seconde année de Joram, fils de Josaphat, roi de Juda: car Ochozias n’avait point de fils.
Hivyo akafa, sawasawa na lile neno la Bwana ambalo Eliya alikuwa amesema. Kwa kuwa Ahazia hakuwa na mwana, Yoramu akawa mfalme baada yake katika mwaka wa pili wa Yehoramu mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda.
18 Mais le reste des actions qu’Ochozias a faites, n’est-il pas écrit dans le Livre des actions des jours des rois d’Israël?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahazia na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?

< 2 Rois 1 >