< 2 Rois 25 >

1 Or il arriva en la neuvième année du règne de Sédécias, au dixième jour, au dixième mois, que Nabuchodonosor, roi de Babylone, vint, lui et toute son armée, contre Jérusalem; et ils l’investirent, et y construisirent tout autour des fortifications.
Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli, akiwa na jeshi lake lote, alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Akapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote.
2 Ainsi la ville fut enfermée et fortifiée jusqu’à la onzième année du roi Sédécias,
Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.
3 Au neuvième jour du mois, et la famine régna dans la ville; et il n’y avait pas de pain pour le peuple du pays.
Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu.
4 Et une brèche fut faite à la ville, et tous les hommes de guerre s’enfuirent durant la nuit, par la voie de la porte qui est entre le double mur près de la porte du jardin du roi (or les Chaldéens assiégeaient tout autour la ville): c’est pourquoi Sédécias s’enfuit par la voie qui conduit aux plaines du désert.
Kisha ukuta wa mji ukavunjwa, na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba.
5 Et l’armée des Chaldéens poursuivit le roi, et le prit dans la plaine de Jéricho; et tous les combattants qui étaient avec lui furent dispersés et l’abandonnèrent.
Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia mfalme na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika,
6 Ayant donc pris le roi, ils l’amenèrent au roi de Babylone à Réblatha, lequel prononça contre lui un arrêt.
naye akakamatwa. Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, mahali ambapo hukumu yake ilitangazwa.
7 Quant aux fils de Sédécias, il les tua devant lui, puis il lui creva les yeux, le chargea de chaînes et l’emmena à Babylone.
Wakawaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Kisha wakayangʼoa macho yake, wakamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
8 Au cinquième mois, au septième jour du mois, c’est la dix-neuvième année même du roi de Babylone, Nabuzardan, chef d’armée, serviteur du roi de Babylone, vint à Jérusalem.
Mnamo siku ya saba ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, afisa wa mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu.
9 Et il brûla la maison du Seigneur et la maison du roi, et il consuma les maisons de Jérusalem, et toute espèce de maison.
Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu.
10 Toute l’armée des Chaldéens, qui était avec ce chef de soldats, détruisit les murs de Jérusalem tout autour.
Jeshi lote la Wakaldayo, chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme, walivunja kuta zilizoizunguka Yerusalemu.
11 Quant à l’autre partie du peuple qui était restée dans la ville, et aux transfuges qui avaient passé au roi de Babylone, et au reste du bas peuple, Nabuzardan, prince de la milice, les transporta à Babylone.
Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi akawapeleka uhamishoni watu waliokuwa wamebaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli.
12 Et il laissa d’entre les pauvres les vignerons et les laboureurs.
Lakini yule jemadari wa askari walinzi akawaacha baadhi ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
13 Mais les colonnes d’airain qui étaient dans le temple du Seigneur, et les bases, et la mer d’airain qui était dans la maison du Seigneur, les Chaldéens les brisèrent, et ils transportèrent tout l’airain à Babylone.
Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba na kuipeleka Babeli.
14 Les marmites d’airain aussi, de même que les pelles, les tridents, les coupes, les petits mortiers, et tous les vases d’airain avec lesquels on faisait le service dans le temple, ils les emportèrent.
Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu.
15 Le prince de la milice emporta également les encensoirs et les patères, ce qui était d’or, à part, et ce qui était d’argent, à part.
Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua vile vyetezo na yale mabakuli ya kunyunyizia, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.
16 C’est-à-dire les deux colonnes, la mer et les bases qu’avait faites Salomon dans le temple du Seigneur; il n’y avait pas de poids pour l’airain de tous ces vases.
Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika.
17 L’une des colonnes avait dix-huit coudées de hauteur, et le chapiteau d’airain de dessus, était de trois coudées de hauteur: et il y avait un réseau et des grenades sur le chapiteau de la colonne; le tout était d’airain: la seconde colonne aussi avait un semblable ornement.
Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane. Sehemu ya shaba juu ya nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tatu na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na wavu wake ilifanana na hiyo ya kwanza.
18 Le prince de la milice emmena aussi Saraïas, le premier prêtre, et Sophonias, second prêtre, et les trois portiers.
Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu.
19 Et un eunuque de la ville qui commandait aux hommes de guerre, et cinq hommes qui étaient toujours devant le roi, qu’il trouva dans la ville, et Sopher, le prince de l’armée, qui exerçait les jeunes soldats pris d’entre le peuple du pays, et soixante hommes du bas peuple, qui avaient été trouvés dans la ville.
Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri watano wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji.
20 Nabuzardan, chef des soldats, les ayant pris, les amena au roi de Babylone à Réblatha.
Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla.
21 Et le roi de Babylone les frappa et les tua à Réblatha, dans la terre d’Emath; ainsi Juda fut transféré hors de son pays,
Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe. Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao.
22 Quant au peuple qui était resté dans la terre de Juda, qu’avait laissé Nabuchodonosor, roi de Babylone, il mit à sa tête Godolias, fils d’Ahicam, fils de Saphan.
Nebukadneza mfalme wa Babeli akamteua Gedalia mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, awe msimamizi wa watu aliowaacha Yuda.
23 Ce qu’ayant appris tous les chefs des soldats, eux et les hommes qui étaient avec eux, à savoir que le roi de Babylone avait établi Godolias pour gouverneur, Ismaël, fils de Nathanias, Johanan, fils de Carée, et Saraïa, fils de Thanéhumeth, le Nétophathite, et Jézonias, fils de Maachathi, vinrent vers Godolias à Maspha, eux et tous les leurs.
Maafisa wote wa jeshi na watu wao waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemteua Gedalia kuwa mtawala, wakamjia Gedalia huko Mispa. Hawa walikuwa Ishmaeli mwana wa Nethania, Yohanani mwana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofathi, na Yezania mwana wa Mmaaka, pamoja na watu wao.
24 Et Godolias leur jura, à eux et aux leurs, disant: Ne craignez point de servir les Chaldéens; demeurez dans cette terre, et servez le roi de Babylone, et vous serez bien.
Gedalia akaapa ili kuwatia moyo wao na watu wao. Akasema, “Msiwaogope maafisa wa Kikaldayo. Kaeni katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babeli, na itakuwa vyema kwenu.”
25 Or il arriva, au septième mois après, qu’Ismaël, fils de Nathanias, fils d’Elisama, de la race royale, vint à Maspha, et dix hommes avec lui; et ils frappèrent Godolias, qui mourut, et aussi les Juifs et les Chaldéens qui étaient avec lui.
Hata hivyo, katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi, nao wakamuua Gedalia, na pia watu wa Yuda, pamoja na Wakaldayo waliokuwa naye huko Mispa.
26 Et se levant, tout le peuple, depuis le petit jusqu’au grand, et les chefs des soldats, vinrent en Egypte, craignant les Chaldéens.
Baada ya haya, watu wote kuanzia aliye mdogo sana hadi aliye mkubwa kabisa, pamoja na maafisa wa jeshi, wakakimbilia Misri kwa kuwaogopa Wakaldayo.
27 Mais il arriva qu’en la trente-septième année de la captivité de Joachin, roi de Juda, au douzième mois, au vingt-septième jour du mois, Evilmérodach, roi de Babylone, en l’année même qu’il commença à régner tira Joachin, roi de Juda, de prison.
Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini kutoka gerezani siku ya ishirini na saba ya mwezi wa kumi na mbili.
28 Et il lui parla avec bonté, et il mit son trône au-dessus du trône des rois qui étaient auprès de lui à Babylone.
Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli.
29 Et il changea ses vêtements qu’il avait eus dans la prison; et Joachin mangea toujours du pain en sa présence tous les jour? de sa vie.
Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme.
30 Il lui assigna aussi sans interruption des vivres, qui même lui étaient donnés chaque jour par le roi, tous les jours de sa vie.
Siku kwa siku mfalme alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake.

< 2 Rois 25 >