< 2 Chroniques 27 >

1 Jonatham avait vingt-cinq ans quand il commença à régner, et il régna seize ans à Jérusalem; le nom de sa mère était Jérusa, fille de Sadoc.
Yothamu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
2 Et il fit ce qui était droit devant le Seigneur, selon tout ce qu’avait fait Ozias, son père, excepté qu’il n’entra point dans le temple du Seigneur; mais le peuple péchait encore.
Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya, lakini tofauti na yeye, hakuingilia huduma za hekaluni mwa Bwana. Lakini hata hivyo, watu wakaendelea na desturi zao mbaya.
3 Ce fut lui qui bâtit la grande porte de la maison du Seigneur, et sur le mur d’Ophel il fit beaucoup de constructions.
Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana na kufanya kazi kubwa kwenye ukuta katika kilima cha Ofeli.
4 Il bâtit aussi des villes sur les montagnes de Juda, et, dans les bois, des châteaux et des tours.
Akajenga miji katika vilima vya Yuda pamoja na ngome na minara mwituni.
5 Ce fut lui qui combattit contre le roi des enfants d’Ammon, et il les vainquit; et les enfants d’Ammon lui donnèrent en ce temps-là cent talents d’argent, dix mille cors de froment et autant d’orge: c’est là ce que lui donnèrent les enfants d’Ammon en l’année seconde et troisième.
Yothamu akafanya vita na mfalme wa Waamoni na kumshinda. Mwaka ule Waamoni wakamlipa talanta 100 za fedha, kori 10,000 za ngano na kori 10,000 za shayiri. Waamoni wakamletea kiasi hicho hicho mwaka wa pili na wa tatu.
6 Et Joatham s’affermit, parce qu’il avait dirigé ses voies devant le Seigneur son Dieu.
Yothamu akaendelea kuwa na nguvu kwa sababu alienenda kwa ukamilifu mbele za Bwana Mungu wake.
7 Mais si le reste des actions de Joatham, tous ses combats, et ses œuvres sont écrits dans le Livre des rois d’Israël et de Juda.
Matukio mengine ya utawala wa Yothamu, pamoja na vita vyake vyote na vitu vingine alivyofanya, vimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
8 Il avait vingt-cinq ans, lorsqu’il commença à régner, et il régna seize ans dans Jérusalem.
Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita.
9 Et Joatham dormit avec ses pères, et on l’ensevelit dans la cité de David, et Achaz, son fils, régna en sa place.
Yothamu akalala na baba zake na akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Chroniques 27 >