< 2 Chroniques 22 >

1 Or les habitants de Jérusalem établirent roi, en sa place, Ochozias, le plus jeune de ses fils; car tous les aînés qui étaient avant lui, les voleurs Arabes qui avaient fait une irruption dans le camp, les avaient tués: ainsi régna Ochozias, fils de Joram, roi de Juda.
Watu wa Yerusalemu wakamfanya Ahazia, mdogo wa wote wa wana wa Yerohamu, kuwa mfalme mahali pa baba yake, kwa sababu washambuliaji wa ghafula waliokuwa wameingia kambini pamoja na Waarabu, walikuwa wamewaua wana wakubwa wote wa Yehoramu. Kwa hiyo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
2 Ochozias avait quarante-deux ans lorsqu’il commença à régner et il ne régna qu’un an à Jérusalem; et le nom de sa mère était Athalie, fille d’Amri.
Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri.
3 Mais ce prince aussi entra dans les voies de la maison d’Achab; car sa mère le porta à se conduire d’une manière impie.
Ahazia naye akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, kwa sababu mama yake alimshawishi katika kutenda maovu.
4 Il fit donc le mal en la présence du Seigneur, comme la maison d’Achab; car ceux-mêmes qui y appartenaient furent ses conseillers après la mort de son père, pour sa perte.
Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana kama walivyokuwa wamefanya nyumba ya Ahabu, kwa kuwa baada ya kufa kwa baba yake nyumba ya Ahabu ndio waliokuwa washauri wake, kwa uangamivu wake.
5 Et il marcha selon leurs conseils, et il alla avec Joram, fils d’Achab, roi d’Israël, à la guerre contre Hazaël, roi de Syrie, à Ramoth-Galaad; et les Syriens blessèrent Joram,
Pia akafuata shauri lao alipokwenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu.
6 Qui revint pour se faire guérir à Jezrahël; car il avait reçu beaucoup de blessures dans le susdit combat. Ainsi Ochozias, fils de Joram, roi de Juda, descendit pour voir Joram, malade à Jezrahël.
Hivyo akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa huko Ramothi alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu. Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu, mfalme wa Yuda, akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.
7 Car il fut dans la volonté de Dieu contre Ochozias, qu’il vint vers Joram; et, lorsqu’il fut venu, il sortit avec lui contre Jéhu, fils de Namsi, que le Seigneur avait oint pour détruire la maison d’Achab.
Mungu alikuwa ameamuru kwamba kuanguka kwa Ahazia kungetokea atakapokwenda kumwona Yoramu. Ahazia alipowasili, wakatoka pamoja na Yoramu ili kwenda kukutana na Yehu mwana wa Nimshi, ambaye Bwana alikuwa amemtia mafuta kuangamiza nyumba ya Ahabu.
8 Comme donc Jéhu s’en allait pour détruire la maison d’Achab, il trouva les princes de Juda et les fils des frères d’Ochosias qui le servaient, et il les tua.
Yehu alipokuwa anatekeleza hukumu juu ya nyumba ya Ahabu, akawakuta wakuu wa Yuda na wana wa jamaa ya Ahazia waliokuwa wanamhudumia Ahazia, naye akawaua.
9 Et cherchant aussi Ochosias lui-même, il le surprit caché dans Samarie; et, après qu’on le lui eut amené, il le tua: or on l’ensevelit, parce qu’il était fils de Josaphat, qui avait cherché le Seigneur en tout son cœur; mais il n’y avait plus d’espérance qu’il régnât quelqu’un de la race d’Ochosias,
Ndipo akaenda kumsaka Ahazia, nao watu wake wakamkamata alipokuwa amejificha huko Samaria. Akaletwa kwa Yehu, naye Yehu akamuua. Wakamzika kwani walisema, “Alikuwa mwana wa Yehoshafati, ambaye alimtafuta Bwana kwa moyo wake wote.” Hivyo hapakuwa na mtu mwenye uwezo katika nyumba ya Ahazia aliyeweza kushika ufalme.
10 Attendu qu’Athalie, sa mère, voyant que son fils était mort, se leva, et tua toute la race royale de la maison de Joram.
Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme ya nyumba ya Yuda.
11 Mais Josabeth, fille du roi, prit Joas, fils d’Ochosias, et le déroba du milieu des enfants du roi, lorsqu’on les massacrait, et elle le cacha, avec sa nourrice, dans la chambre des lits: or Josabeth, qui l’avait caché, était fille de Joram, femme de Joïada, le pontife, et sœur d’Ochosias; et c’est pour cela qu’Athalie ne fit pas mourir Joas.
Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala. Kwa kuwa Yehosheba, aliyekuwa binti wa Mfalme Yehoramu, na pia alikuwa mke wa kuhani Yehoyada, alikuwa dada yake Ahazia, akamficha huyo mtoto ili Athalia asimuue.
12 Ce prince fut caché avec eux dans la maison de Dieu, durant les six années que régna Athalie sur la terre de Juda.
Alibaki amefichwa pamoja nao katika Hekalu la Mungu kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.

< 2 Chroniques 22 >