< 2 Chroniques 19 >

1 Mais Josaphat, roi de Juda, retourna paisiblement en sa maison à Jérusalem.
Mfalme Yehoshafati wa Yuda akarudi salama kwenye jumba lake la kifalme huko Yerusalemu.
2 Jéhu, le Voyant, fils d’Hanani, vint à sa rencontre, et lui dit: Vous donnez du secours à l’impie, et vous vous liez d’amitié avec ceux qui haïssent le Seigneur; et c’est pour cela certainement que vous méritiez la colère de Dieu.
Yehu mwonaji, mwana wa Hanani, akapanda kwenda kuonana naye akamwambia Mfalme Yehoshafati, “Je, utawasaidia waovu na kuwapenda wale wanaomchukia Bwana? Kwa sababu ya jambo hili, ghadhabu ya Bwana iko juu yako.
3 Mais de bonnes œuvres ont été trouvées en vous, parce que vous avez enlevé les bois sacrés de la terre de Juda, et que vous avez préparé votre cœur pour chercher le Seigneur Dieu de vos pères.
Hata hivyo, kuna mema yaliyoonekana kwako, kwa kuwa umeondoa katika nchi nguzo za Ashera na umeukaza moyo wako katika kumtafuta Mungu.”
4 Josaphat habita donc à Jérusalem, et il sortit de nouveau vers le peuple, depuis Bersabée jusqu’à la montagne d’Ephraïm, et il les rappela au culte du Seigneur, le Dieu de leurs pères.
Yehoshafati aliishi huko Yerusalemu, naye akatoka akaenda tena miongoni mwa watu, kuanzia Beer-Sheba hadi nchi ya vilima ya Efraimu na kuwageuza wakamrudia Bwana, Mungu wa baba zao.
5 Et il établit des juges pour le pays dans toutes les villes de Juda fortifiées, pour chaque lieu en particulier.
Akawaweka waamuzi katika nchi, kwenye miji yote ya Yuda yenye maboma.
6 Et il ordonna aux juges: Prenez garde, dit-il, à tout ce que vous ferez; car ce n’est pas la justice d’un homme que vous exercez, mais celle du Seigneur, et tout ce que vous aurez jugé retombera sur vous.
Akawaambia, “Angalieni kwa makini yale mtendayo, kwa kuwa hamkuhukumu kwa ajili ya mwanadamu bali kwa ajili ya Bwana ambaye yu pamoja nanyi kila mtoapo hukumu.
7 Que la crainte du Seigneur soit avec vous, et faites tout avec soin; car il n’y a dans le Seigneur notre Dieu, ni iniquité, ni acception de personnes, ni désir de présents.
Basi sasa hofu ya Bwana na iwe juu yenu. Hukumuni kwa uangalifu, kwa kuwa kwa Bwana Mungu wetu hakuna jambo lisilo la haki, upendeleo, wala rushwa.”
8 Josaphat établit aussi dans Jérusalem des Lévites, des prêtres, et des princes des familles d’Israël, afin de juger le jugement et la cause du Seigneur pour ses habitants.
Pia huko Yerusalemu, Yehoshafati akaweka baadhi ya Walawi, makuhani na viongozi wa jamaa za Waisraeli ili kutoa hukumu kwa ajili ya Bwana na kuamua magomvi. Nao waliishi huko Yerusalemu.
9 Et il leur ordonna, disant: C’est ainsi que vous agirez dans la crainte du Seigneur, fidèlement et avec un cœur parfait.
Akawapa maagizo haya: “Ni lazima mtumike kwa uaminifu na kwa moyo wote katika kicho cha Bwana.
10 Quant à toute cause (qui vous viendra) de vos frères qui habitent dans leurs villes, entre parenté et parenté, partout où il sera question de loi, de commandement, de cérémonies, d’ordonnances, faites-la leur connaître, afin qu’ils ne pèchent point contre le Seigneur, et que sa colère ne vienne point sur vous et sur vos frères; agissant donc ainsi, vous ne pécherez point.
Katika kila shauri lifikalo mbele yenu kutoka kwa ndugu zenu wale waishio katika miji, ikiwa ni la umwagaji wa damu au mambo mengine yahusuyo sheria, amri, hukumu au maagizo, inawapasa ninyi kuwaonya kwamba wasiingie katika hatia dhidi ya Bwana, la sivyo ghadhabu yake itakuja juu yenu na ndugu zenu. Tendeni hivyo, nanyi hamtatenda dhambi.
11 Or Amarias, le prêtre, votre pontife, présidera dans les choses qui regardent Dieu, et Zabadias, fils d’Ismael, chef dans la maison de Juda, sera préposé sur les ouvrages qui appartiennent au service du roi. Vous avez aussi pour maîtres les Lévites devant vous; fortifiez-vous et agissez avec soin, et le Seigneur sera avec vous, vous comblant de biens.
“Amaria kuhani mkuu atakuwa juu yenu katika jambo lolote linalomhusu Bwana naye Zebadia mwana wa Ishmaeli, kiongozi wa kabila la Yuda, atakuwa juu yenu kwa jambo lolote linalomhusu mfalme, nao Walawi watatumika kama maafisa mbele yenu. Tendeni kwa ujasiri, naye Bwana atakuwa pamoja na wale watendao vyema.”

< 2 Chroniques 19 >