< 1 Samuel 4 >

1 Or il arriva en ces jours-là, que les Philistins se rassemblèrent pour le combat; et Israël sortit au devant des Philistins pour la bataille, et il campa près de la pierre du Secours. Mais les Philistins vinrent à Aphec,
Nalo neno la Samweli likaja kwa Israeli yote. Basi Waisraeli walitoka kwenda kupigana dhidi ya Wafilisti. Waisraeli wakapiga kambi huko Ebenezeri, nao Wafilisti wakapiga kambi huko Afeki.
2 Et ils rangèrent leur armée en bataille en face d’Israël. Or, le combat engagé, Israël tourna le dos aux Philistins; et il y eut de taillés en pièces dans ce combat çà et là, à travers les champs, environ quatre mille hommes.
Wafilisti wakapanga safu za majeshi yao kupambana na Israeli, wakati vita vilipoenea, Israeli wakashindwa na Wafilisti, ambao waliwaua askari wa Israeli wapatao 4,000 kwenye uwanja wa vita.
3 Et le peuple revint dans le camp, et les anciens d’Israël dirent: Pourquoi le Seigneur nous a-t-il frappés aujourd’hui, devant les Philistins? Apportons près de nous de Silo, l’arche de l’alliance du Seigneur, et qu’elle vienne au milieu de nous, afin qu’elle nous sauve de la main de nos ennemis.
Askari waliporudi kambini, wazee wa Israeli wakawauliza, “Kwa nini Bwana ameruhusu leo tushindwe mbele ya Wafilisti? Tuleteni Sanduku la Agano la Bwana kutoka Shilo, ili lipate kwenda pamoja nasi, na kutuokoa kutoka mikono ya adui zetu.”
4 Le peuple envoya donc à Silo, et ils en apportèrent l’arche de l’alliance du Seigneur des armées, assis sur les chérubins; et les deux fils d’Héli, Ophni et Phinéès, étaient avec l’arche de l’alliance de Dieu.
Hivyo wakawatuma watu huko Shilo, nao wakalichukua Sanduku la Agano la Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliyekaa kwenye kiti chake cha enzi kati ya makerubi. Nao wale wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, walikuwako huko pamoja na Sanduku la Agano la Mungu.
5 Et lorsque l’arche de l’alliance du Seigneur fut venue dans le camp, tout Israël cria d’un grand cri, et la terre retentit.
Wakati Sanduku la Agano la Bwana lilikuja kambini, Waisraeli wote wakapiga kelele kwa sauti kuu hata ardhi ikatikisika.
6 Et les Philistins entendirent le bruit de la clameur et dirent: Quel est le bruit de cette grande clameur dans le camp des Hébreux? Et ils connurent que l’arche du Seigneur était dans le camp.
Wafilisti waliposikia makelele wakauliza, “Ni nini makelele haya yote katika kambi ya Waebrania?” Walipofahamu kuwa Sanduku la Bwana limekuja kambini,
7 Alors les Philistins craignirent, disant: Dieu est venu dans le camp. Et ils gémirent, disant:
Wafilisti wakaogopa, wakasema, “Mungu amekuja kambini, ole wetu. Halijatokea jambo kama hili tangu hapo.
8 Malheur à nous! car il n’y eut pas une si grande allégresse hier et avant-hier; malheur à nous! Qui nous sauvera de la main de ces dieux suprêmes? ce sont ces dieux qui ont frappé l’Égypte de toute sorte de plaies dans le désert,
Ole wetu! Ni nani atakayetuokoa kutoka mikononi mwa miungu hii yenye nguvu? Ni miungu ile iliyowapiga Wamisri kwa mapigo ya aina zote huko jangwani.
9 Prenez courage, et soyez hommes de cœur, Philistins; ne servez pas les Hébreux comme eux vous ont servis; prenez courage et combattez.
Tuweni hodari, enyi Wafilisti! Tuweni wanaume, la sivyo mtakuwa watumwa wa Waebrania, kama wao walivyokuwa kwenu. Kuweni wanaume, mpigane!”
10 Les Philistins combattirent donc, et Israël fut taillé en pièces, et chacun s’enfuit dans son tabernacle; et il se fit un très grand carnage, et il tomba du côté d’Israël trente mille hommes de pied.
Basi Wafilisti wakapigana, nao Waisraeli wakashindwa na kila mtu akakimbilia hemani mwake. Mauaji yalikuwa makubwa sana, Israeli wakapoteza askari 30,000 waendao kwa miguu.
11 De plus, l’arche de Dieu fut prise, et les deux fils d’Héli, Ophni et Phinéès moururent aussi.
Sanduku la Mungu likatekwa, na hao wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, wakauawa.
12 Or, un homme de Benjamin accourant de l’armée, vint à Silo, ce jour-là, ayant son vêtement déchiré, et la tête couverte de poussière.
Siku ile ile mtu mmoja wa kabila la Benyamini akakimbia kutoka kwenye uwanja wa vita na kwenda Shilo, nguo zake zikiwa zimeraruka na akiwa na mavumbi kichwani mwake.
13 Et lorsque cet homme arriva, Héli était assis sur son siège, tourné vers le chemin; car son cœur tremblait de crainte pour l’arche de Dieu. Mais, cet homme, après qu’il fut entré, donna la nouvelle à la ville; et toute la cité poussa des hurlements.
Alipofika, Eli alikuwa ameketi juu ya kiti chake kando ya barabara akiangalia, kwa sababu moyo wake ulikuwa na hofu kwa ajili ya Sanduku la Mungu. Mtu yule alipoingia mjini na kueleza kilichokuwa kimetokea, mji wote ukalia.
14 Et, Héli entendit le bruit de la clameur et dit: Quel est le bruit de ce tumulte? Et cet homme se hâta, et vint, et donna la nouvelle à Héli.
Eli akasikia kelele za kilio, naye akauliza, “Ni nini maana ya makelele haya?” Yule mtu akafanya haraka kwenda kwa Eli,
15 Or, Héli avait quatre-vingt-dix-huit ans, et ses yeux étaient obscurcis, et il ne pouvait pas voir.
wakati huu Eli alikuwa na miaka tisini na minane nayo macho yake yalikuwa yamepofuka na hakuweza kuona.
16 Et cet homme dit à Héli: C’est moi qui suis venu de la bataille, et moi qui me suis enfui de l’armée aujourd’hui. Héli lui demanda: Qu’a-t-il été fait, mon fils?
Akamwambia Eli, “Mimi nimetoka vitani sasa hivi, nimekimbia kutoka huko leo hii.” Eli akamuuliza, “Je, mwanangu, ni nini kimetokea huko?”
17 Celui qui donnait la nouvelle répondant: Israël, dit-il, a fui devant les Philistins et il a été fait une grande ruine dans le peuple; et de plus vos deux fils, Ophni et Phinéès, sont morts, et l’arche de Dieu a été prise.
Yule mtu aliyeleta habari akajibu, “Israeli amekimbia mbele ya Wafilisti, nalo jeshi limepata hasara kubwa. Pia wana wako wawili, Hofni na Finehasi, wamekufa, na Sanduku la Mungu limetekwa.”
18 Lorsque cet homme eut nommé l’arche de Dieu, Héli tomba de son siège à la renverse près de la porte, et, la tête brisée, il mourut. C’était un homme vieux et très avancé en âge; et il jugea lui-même Israël pendant quarante ans.
Mara alipotaja Sanduku la Mungu, Eli alianguka kutoka kwenye kiti chake kwa nyuma kando ya lango. Shingo yake ikavunjika naye akafa, kwa kuwa alikuwa mzee tena mzito. Alikuwa amewaongoza Israeli kwa miaka arobaini.
19 Or, sa belle-fille, femme de Phinéès, était enceinte et près d’enfanter; et ayant appris la nouvelle que l’arche de Dieu avait été prise, et que son beau-père était mort, ainsi que son mari, elle se baissa et enfanta; car les douleurs subites l’avaient saisie.
Mkwewe, mke wa Finehasi, alikuwa mjamzito na karibu wakati wa kujifungua. Aliposikia habari kwamba Sanduku la Mungu limetekwa na ya kuwa baba mkwe wake na mumewe wamekufa, akapata utungu naye akajifungua lakini akazidiwa na utungu.
20 Mais au moment même de sa mort, celles qui se tenaient auprès d’elle, lui dirent: Ne crains point, car tu as enfanté un fils. Et elle ne répondit pas, et n’y fit pas même attention.
Alipokuwa akifa, wanawake waliokuwa wanamhudumia wakamwambia, “Usikate tamaa, umemzaa mwana.” Lakini hakujibu wala kuweka maanani.
21 Et elle appela son fils Ichabod, disant: La gloire d’Israël a été transférée, parce que l’arche de Dieu fut prise, et à cause de son beau-père et de son mari;
Alimwita yule mtoto Ikabodi, akisema, “Utukufu umeondoka katika Israeli,” kwa sababu ya kutekwa kwa Sanduku la Mungu na vifo vya baba mkwe na mumewe.
22 Et elle dit: La gloire d’Israël a été transférée, parce que l’arche de Dieu avait été prise.
Akasema, “Utukufu umeondoka katika Israeli, kwa kuwa Sanduku la Mungu limetekwa.”

< 1 Samuel 4 >