< 1 Samuel 29 >

1 Toutes les troupes des Philistins s’assemblèrent donc à Aphec; mais Israël aussi campa près de la fontaine de Jezraël.
Wafilisti wakakusanya majeshi yao yote huko Afeki, nao Waisraeli wakapiga kambi karibu na chemchemi iliyoko Yezreeli.
2 Or, les satrapes des Philistins marchaient avec des compagnies de cent et de mille hommes; mais David et ses hommes étaient à l’arrière-garde avec Achis.
Watawala wa Wafilisti walipokuwa wakipita pamoja na vikosi vyao vya mamia na vya maelfu, Daudi na watu wake walikuwa wakitembea huko nyuma pamoja na Akishi.
3 Les princes des Philistins dirent à Achis: Que veulent dire ces Hébreux? Et Achis répondit aux princes des Philistins: Est-ce que vous ne connaissez pas David, qui a été serviteur de Saül, roi d’Israël, qui est avec moi depuis nombre de jours et même d’années, et dans lequel je n’ai rien trouvé, depuis le jour qu’il s’est réfugié auprès de moi jusqu’à ce jour-ci?
Majemadari wa Wafilisti wakauliza, “Vipi kuhusu hawa Waebrania?” Akishi akajibu, “Huyu si Daudi, aliyekuwa afisa wa Sauli mfalme wa Israeli? Ameshakuwa pamoja nami kwa zaidi ya mwaka, naye tangu alipomwacha Sauli hadi sasa, sikuona kosa lolote kwake.”
4 Mais les princes des Philistins s’irritèrent contre lui, et lui dirent: Que cet homme s’en retourne; qu’il demeure dans son lieu, dans lequel vous l’avez établi, et qu’il ne descende pas avec nous au combat, afin qu’il ne devienne point notre ennemi, lorsque nous aurons commencé à combattre; car comment pourra-t-il apaiser son seigneur autrement qu’avec nos têtes?
Lakini majemadari wa Wafilisti wakamkasirikia na kusema, “Mrudishe mtu huyu, apate kurudi mahali pale ulipompangia. Haimpasi kufuatana pamoja nasi vitani, asije akageuka, akawa kinyume chetu vitani. Ni kwa njia ipi bora zaidi angeweza kujipatia tena kibali kwa bwana wake, isipokuwa kwa vichwa vya watu wetu wenyewe?
5 N’est-ce pas ce David, en l’honneur duquel on chantait dans les chœurs: Saül a frappé sur ses mille, et David sur ses dix mille?
Je, huyu si ndiye Daudi walioimba kumhusu katika ngoma zao, wakisema: “‘Sauli amewaua elfu zake, naye Daudi makumi elfu yake’?”
6 Achis donc appela David, et lui dit: Le Seigneur vit! tu es droit et bon en ma présence, et ta sortie et ton entrée est avec moi dans le camp; et je n’ai trouvé en toi rien de mal, depuis le jour que tu es venu vers moi jusqu’à ce jour-ci; mais tu ne plais pas aux satrapes.
Basi Akishi akamwita Daudi na kumwambia, “Kama vile Bwana aishivyo, wewe umekuwa mtu mwaminifu, nami ningependa utumike pamoja nami katika jeshi. Tangu siku ile uliyofika kwangu hadi sasa, sijaona kosa lolote kwako, lakini hao watawala hawakukubali.
7 Retourne-t’en donc, et va en paix, et n’offense pas les yeux des satrapes des Philistins.
Rudi na uende kwa amani; usifanye chochote cha kuwakasirisha watawala wa Kifilisti.”
8 Et David demanda à Achis: Qu’ai-je donc fait, et qu’avez-vous trouvé en moi, votre serviteur, depuis le jour que j’ai été en votre présence jusqu’à ce jour-ci, pour que je ne vienne point, et que je ne combatte point contre les ennemis de mon seigneur roi?
Daudi akamuuliza Akishi, “Lakini mimi nimefanya nini? Je, umeona nini kibaya juu ya mtumishi wako tangu siku ile niliyokuja kwako hadi leo? Kwa nini nisirudi na kupigana na adui za bwana wangu mfalme?”
9 Mais répondant, Achis dit à David: Je sais que tu es bon à mes yeux comme un ange de Dieu; mais les princes des Philistins ont dit: Il ne montera point avec nous au combat.
Akishi akamjibu Daudi, “Mimi ninajua ya kuwa wewe umekuwa wa kupendeza machoni pangu kama vile malaika wa Mungu. Lakini hao majemadari wa Wafilisti wamesema, ‘Huyu haimpasi kwenda vitani pamoja nasi.’
10 Ainsi lève-toi, dès le matin, toi et les serviteurs de ton seigneur qui sont venus avec toi; et lorsque vous vous serez levés pendant la nuit, et qu’il aura commencé à faire jour, partez.
Sasa amka mapema, pamoja na watumishi wa bwana wako waliofuatana nawe, nanyi ondokeni asubuhi mara kutakapopambazuka.”
11 C’est pourquoi David se leva pendant la nuit, lui et ses hommes, pour partir dès le matin, et retourner dans la terre des Philistins; mais les Philistins montèrent à Jezraël.
Hivyo Daudi na watu wake wakaamka asubuhi na mapema, wakaenda zao kurudi katika nchi ya Wafilisti, nao Wafilisti wakapanda kwenda Yezreeli.

< 1 Samuel 29 >