< 1 Rois 17 >

1 Et Elie, le Thesbite, un des habitants de Galaad, dit à Achab: Il vit, le Seigneur Dieu d’Israël, en la présence duquel je suis! il n’y aura pendant ces années-ci ni rosée ni pluie que selon les paroles de ma bouche.
Basi Eliya, Mtishbi kutoka Tishbi katika Gileadi, akamwambia Ahabu, “Kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninamtumikia, hapatakuwa na umande wala mvua katika miaka hii, isipokuwa kwa neno langu.”
2 Et la parole du Seigneur fut adressée à Elie, disant:
Kisha neno la Bwana likamjia Eliya, kusema,
3 Retire-toi d’ici; va contre l’orient, et cache-toi près du torrent de Carith, qui est contre le Jourdain;
“Ondoka hapa, elekea upande wa mashariki ukajifiche katika Kijito cha Kerithi, mashariki mwa Yordani.
4 Et là tu boiras au torrent; et j’ai ordonné aux corbeaux qu’ils te nourrissent là.
Utakunywa maji kutoka kile kijito, nami nimeagiza kunguru wakulishe huko.”
5 Elie s’en alla donc, et fit selon la parole du Seigneur, et lorsqu’il s’en fut allé, il s’assit près du torrent de Carith, qui est contre le Jourdain.
Hivyo akafanya kile alichoambiwa na Bwana. Akaenda katika Kijito cha Kerithi, mashariki ya Yordani na akakaa huko.
6 Et les corbeaux lui apportaient du pain et de la chair le matin, également du pain et de la chair le soir, et il buvait au torrent.
Kunguru wakamletea mkate na nyama asubuhi na mkate na nyama jioni, naye akanywa maji kutoka kile kijito.
7 Mais après quelques jours le torrent se sécha; car il n’avait pas plu sur la terre.
Baada ya muda, kile kijito kikakauka kwa sababu mvua haikuwa imenyesha katika nchi.
8 La parole du Seigneur lui fut donc adressée, disant:
Kisha neno la Bwana likamjia, kusema,
9 Lève-toi, et va à Sarephta, ville des Sidoniens, et tu demeureras là; car j’ai ordonné là à une femme veuve qu’elle te nourrisse.
“Ondoka, uende Sarepta ya Sidoni na ukae huko. Nimemwagiza mjane katika sehemu ile akupatie chakula.”
10 Il se leva et s’en alla à Sarephta. Et lorsqu’il fut venu à la porte de la ville, il aperçut une femme veuve qui ramassait du bois; et il l’appela, et lui dit: Donne-moi un peu d’eau dans le vase, afin que je boive.
Hivyo akaenda Sarepta. Alipofika kwenye lango la mji, mjane alikuwa huko akiokota kuni. Akamwita na kumwambia, “Naomba uniletee maji kidogo kwenye gudulia ili niweze kunywa.”
11 Et lorsque celle-ci allait pour en apporter, il cria derrière elle, disant: Apporte-moi aussi, je te prie, un peu de pain en ta main.
Alipokuwa anakwenda kumletea, akamwita akasema, “Tafadhali niletee pia kipande cha mkate.”
12 Elle lui répondit: Le Seigneur ton Dieu vit! je n’ai point de pain, mais seulement dans la cruche autant de farine qu’une main peut en contenir, et un peu d’huile dans le flacon. Voilà que je ramasse deux morceaux de bois, pour que j’entre et que je fasse du pain pour moi et pour mon fils, afin que nous mangions, et que nous mourions.
Akamjibu, “Hakika kama Bwana Mungu wako aishivyo, sina mkate wowote, isipokuwa konzi ya unga kwenye gudulia na mafuta kidogo kwenye chupa. Ninakusanya kuni chache nipeleke nyumbani na nikapike chakula kwa ajili yangu na mwanangu, ili kwamba tule, kiishe, tukafe.”
13 Élie lui dit: Ne crains point; mais va, et fais comme tu as dit; cependant fais pour moi auparavant, avec ce peu de farine même, un petit pain cuit sous la cendre, et apporte-le-moi; mais pour toi et pour ton fils, tu en feras ensuite.
Eliya akamwambia, “Usiogope. Nenda nyumbani ukafanye kama ulivyosema. Lakini kwanza unitengenezee mimi mkate mdogo kutoka vile ulivyo navyo kisha uniletee na ndipo utayarishe chochote kwa ajili yako na mwanao.
14 Car voici ce que dit le Seigneur Dieu d’Israël: La cruche de la farine ne manquera point, et le flacon de l’huile ne diminuera point, jusqu’au jour où le Seigneur doit donner de la pluie sur la face de la terre.
Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Lile gudulia la unga halitakwisha wala ile chupa ya mafuta haitakauka hadi siku ile Bwana atakapoleta mvua juu ya nchi.’”
15 Cette femme s’en alla donc, et fit selon la parole d’Elie; et il mangea lui-même, et elle et sa maison; et depuis ce jour-là
Akaondoka na kufanya kama Eliya alivyomwambia. Kwa hiyo kukawa na chakula kila siku kwa ajili ya Eliya, yule mwanamke na jamaa yake.
16 La cruche de farine ne manqua point, et l’huile du flacon ne diminua point, selon la parole que le Seigneur avait dite par l’entremise d’Elie.
Kwa kuwa lile gudulia la unga halikwisha na ile chupa ya mafuta haikukauka, sawasawa na lile neno la Bwana alilosema Eliya.
17 Or il arriva ensuite que le fils de cette femme, mère de famille, fut malade; et sa maladie fut très violente, en sorte qu’il ne restait pas en lui un souffle.
Baada ya muda, mwana wa yule mwanamke mwenye nyumba akaugua. Hali yake ikaendelea kuwa mbaya sana, na hatimaye akaacha kupumua.
18 Cette femme dit donc à Elie: Qu’importe à moi et à toi, homme de Dieu? Es-tu entré chez moi pour renouveler la mémoire de mes péchés et pour faire mourir mon fils?
Akamwambia Eliya, “Una nini dhidi yangu, ewe mtu wa Mungu? Umekuja ili kukumbushia dhambi yangu na kusababisha kifo cha mwanangu?”
19 Et Elie lui répondit: Donne-moi ton fils. Et il le prit de dessus son sein, le porta dans la chambre où lui-même demeurait, et il le mit sur son lit.
Eliya akamjibu, “Nipe mwanao.” Eliya akampokea kutoka kifuani mwake, akambeba mpaka chumba cha juu alipokuwa anaishi, akamlaza kitandani mwake.
20 Puis il cria au Seigneur et dit: Seigneur mon Dieu, même la veuve chez laquelle moi-même en tout cas je suis nourri, vous l’avez affligée au point de faire mourir son fils?
Kisha akamlilia Bwana, akasema “Ee Bwana Mungu wangu, je, pia umeleta msiba juu ya mjane huyu ninayeishi pamoja naye, kwa kusababisha mwanawe kufa?”
21 Et il s’étendit et se rapetissa sur l’enfant jusqu’à sa mesure, par trois fois, puis il cria au Seigneur et dit: Seigneur mon Dieu, je vous conjure, que l’âme de cet enfant retourne en son corps.
Kisha akajinyoosha juu ya kijana mara tatu na kumlilia Bwana, akisema, “Ee Bwana Mungu wangu, nakuomba roho ya huyu kijana imrudie!”
22 Et le Seigneur exauça la voix d’Elie, et l’âme de l’enfant retourna en lui, et il revécut.
Bwana akasikia kilio cha Eliya, na roho ya kijana ikamrudia, naye akafufuka.
23 Alors Elie prit l’enfant, le mena de sa chambre au bas de la maison, le remit à sa mère, et lui dit: Vois, ton fils vit.
Eliya akamtwaa kijana na kumbeba kutoka chumbani mwake akamshusha kumpeleka kwenye nyumba. Akampa mama yake na kusema, “Tazama, mwanao yu hai!”
24 Et la femme répondit à Elie: Maintenant je reconnais en cela que tu es un homme de Dieu, et que la parole du Seigneur en ta bouche est véritable.
Ndipo yule mwanamke akamwambia Eliya, “Sasa ninajua kwamba wewe ni mtu wa Mungu, na kwamba neno la Bwana kutoka kinywani mwako ni kweli.”

< 1 Rois 17 >