< Job 5 >

1 Vois donc s'il est quelqu'un que tu puisses invoquer et qui t'écoute; peut-être l'un des saints anges t'apparaîtra.
Ita sasa; je kuna yeyote ambaye atakujibu? Utamrudia yupi katika watakatifu hao?
2 Songe que la colère détruit l'insensé; l'envie tue celui qui s'égare.
Kwa kuwa hasira huua mtu mpumbavu; wivu huua mjinga.
3 J'ai cependant vu des insensés prendre racine; mais leurs richesses ont été aussitôt dévorées.
Nimemuona mtu mpumbavu akishika mzizi, lakini ghafla niliyalaani makazi yake.
4 Qu'il n'y ait point de salut pour leurs enfants; que l'on forme autour d'eux des danses railleuses, devant la porte des petits; que nul ne les délivre.
Watoto wake wako mbali na uzima; wameangamia langoni mwa mji. Hakuna yeyote atakaye waponya.
5 Que les justes mangent ce qu'ils ont amassé; qu'eux-mêmes ne puissent sortir de leur infortune et que leur force soit épuisée.
Mwenye njaa hula mavuno yao; hata huyachukua katikati ya miiba. Wenye kiu huzihemea mali zao.
6 Ce n'est point de la terre que naît le mal; ce n'est point dans les montagnes que germent les peines.
Kwa kuwa magumu hayatoki udongoni; wala taabu haichipuki katika nchi.
7 Mais l'homme est né pour se rendre malheureux comme les petits des vautours pour voler sur les hautes cimes.
Badala yake, wanadamu huzaliwa kwaajili ya taabu, kama tu cheche za moto zirukavyo juu.
8 Pour moi, je prierai le Seigneur, j'invoquerai le Seigneur maître de toutes choses,
Lakini kwa mimi, ningemrudia Mungu mwenyewe; kwake ningeaminisha kusudi langu -
9 Qui fait des merveilles innombrables et incompréhensibles, et des actions glorieuses et grandes,
yeye afanyae makuu na mambo yasiyochunguzika, mambo ya ajabu yasiyo na hesabu.
10 Qui donne à la terre de la pluie et lui envoie l'eau du ciel,
Hutoa mvua juu ya nchi, na huyapeleka maji mashambani.
11 Qui élève les humbles et ranime ceux qui se croyaient perdus,
Hufanya haya kwaajili ya kuwainua juu hao walio chini; huwapandisha sehemu salama hao waombolezao.
12 Qui dissipe les desseins des trompeurs et empêche leurs mains de les exécuter,
Yeye huharibu mipango ya watu wenye hila, ili mikono yao isipate mafanikio.
13 Qui confond la prudence des sages et bouleverse les artifices des gens dissimulés.
Yeye huwanasa watu wenye hekima katika matendo ya hila zao wenyewe; mipango ya watu waliogeuzwa huharibika haraka.
14 Il les enveloppe en plein jour de ténèbres; il les fait marcher à tâtons, à midi comme à minuit.
Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, na hupapasa mchana kama vile ni usiku.
15 Puissent-ils périr dans les batailles; puisse le faible être délivré de la main des grands.
Lakini yeye huokoa maskini kwa upanga wa vinywa vyao na mhitaji kwa mkono wa mtu mwenye nguvu.
16 Puisse le petit conserver de l'espérance; puisse le Seigneur fermer la bouche de l'injuste.
Hivyo mtu maskini ana matumaini, na udhalimu hufumba kinywa chake mwenyewe.
17 Heureux l'homme qu'a châtié le Seigneur; qu'il se garde de rejeter de tels avertissements.
Tazama, amebarikiwa mtu ambaye hutiwa adabu na Mungu; kwa sababu hiyo, usidharau uongozi wa Mwenyezi.
18 Car le Seigneur fait souffrir et il répare: il frappe et ses mains guérissent.
Kwa kuwa yeye hujeruhi na kisha huuguza; yeye hutia jeraha na kisha mikono yake huponya.
19 Six fois il te tirera de peine; la septième fois, le mal ne t'atteindra plus.
Yeye atakuokoa na mateso sita; kweli, katika mateso saba, hakuna uovu utakao kugusa.
20 Pendant la famine, il te préservera de la mort; à la guerre il détournera de toi le fer ennemi.
Wakati wa njaa atakukomboa na kifo, na kwa uwezo wa upanga wakati wa vita.
21 Il te mettra à l'abri des flagellations de la langue et tu n'auras rien à craindre des fléaux qui surviendront.
Wewe utafichwa na mateso ya ulimi; na usitishike na uharibifu utakapokuja.
22 Tu te riras des injustes et des déréglés; tu braveras les bêtes fauves.
Wewe utaufurahia uharibifu na njaa, na hutatishika na wanyama wakali wa nchi.
23 Les animaux les plus farouches te laisseront en paix.
Kwa kuwa wewe utakuwa na mapatano na mawe ya shambani mwako, na wanyama wa mwituni watakuwa na amani na wewe.
24 Tu sentiras d'où vient le calme de ta maison; et tes habitudes seront irréprochables.
Wewe utajua kwamba hema lako lina usalama; utatembelea zizi la kondoo wako na hutakosa kitu chochote.
25 Tu verras croître une florissante famille, aussi nombreuse que les herbes des champs.
Pia utafahamu kwamba uzao wako utakuwa mwingi, na vizazi vyako vitakuwa kama nyasi ardhini.
26 Et tu descendras à la tombe mûr comme le blé que l'on moissonne en la saison, ou comme le monceau que l'on a renfermé dans l'aire après l'avoir récolté.
Wewe utafika kaburini kwako mwenye umri kamili, kama vile rundo la mashuke ya nafaka liendavyo juu wakati wake.
27 Telles sont les pensées que j'ai cherchées et conçues; rentre en toi-même et vois ce que tu as fait.
Tazama, tumelipeleleza jambo hili; ndivyo lilivyo; lisikie, na ulifahamu kwa ajili yako mwenyewe.”

< Job 5 >