< Nombres 35 >

1 Yahweh parla à Moïse, dans les plaines de Moab, près du Jourdain, vis-à-vis de Jéricho, en disant:
Bwana akamwambia Mose katika nchi tambarare ya Moabu, kando ya Mto Yordani kuvukia Yeriko,
2 « Ordonne aux enfants d’Israël de céder aux Lévites, sur l’héritage qu’ils posséderont, des villes pour y habiter. Vous donnerez aussi aux Lévites des lieux de pâture autour de ces villes.
“Waagize Waisraeli kuwapa Walawi miji ya kuishi kutoka urithi ambao Waisraeli wataumiliki. Wape maeneo ya malisho kuzunguka hiyo miji.
3 Ils auront les villes pour y habiter, et leurs lieux de pâture seront pour leur gros bétail, pour leurs autres biens et pour tous leurs animaux.
Kisha watakuwa na miji ya kuishi na maeneo ya malisho kwa ajili ya ngʼombe zao, mbuzi, kondoo na mifugo yao mingine yote.
4 Les lieux de pâture des villes que vous donnerez aux Lévites seront, à partir du mur de la ville, en dehors, de mille coudées tout autour.
“Maeneo ya malisho kuzunguka miji hiyo ambayo mtawapa Walawi yataenea mita 450 kutoka kwenye ukuta wa miji.
5 Vous mesurerez, en dehors de la ville, deux mille coudées pour le côté oriental, deux mille coudées pour le côté méridional, deux mille coudées pour le côté occidental et deux mille coudées pour le côté septentrional; la ville sera au milieu: tels seront les lieux de pâture de leurs villes.
Nje ya mji, pima mita 900 upande wa mashariki, upande wa kusini mita 900, upande wa magharibi mita 900, na upande wa kaskazini mita 900, na mji utakuwa katikati. Eneo hili litakuwa lao kwa ajili ya malisho.
6 Quant aux villes que vous donnerez aux Lévites, ce sont les six villes de refuge, que vous disposerez pour que le meurtrier s’y réfugie; et, en plus, vous donnerez quarante-deux autres villes.
“Miji sita mtakayowapa Walawi itakuwa ya makimbilio, ambayo mtu anayemuua mwenzake aweza kukimbilia humo. Zaidi ya hiyo, wapeni miji mingine arobaini na miwili.
7 Ainsi toutes les villes que vous donnerez aux Lévites seront au nombre de quarante-huit villes avec leurs lieux de pâture.
Kwa jumla inawapasa kuwapa Walawi miji arobaini na minane, pamoja na maeneo ya malisho yao.
8 Pour les villes que vous donnerez sur les possessions des enfants d’Israël, vous prendrez plus de ceux qui ont plus, et vous prendrez moins de ceux qui ont moins. Chacun cédera de ses villes aux Lévites à proportion de l’héritage qu’il aura reçu. »
Miji ambayo mtawapa Walawi kutoka nchi ambayo Waisraeli wanamiliki itatolewa kwa uwiano wa urithi wa kila kabila. Chukua miji mingi kutoka lile kabila lenye miji mingi, lakini uchukue miji michache kutoka kwa kabila lile lenye miji michache.”
9 Yahweh parla à Moïse, en disant:
Kisha Bwana akamwambia Mose:
10 « Parle aux enfants d’Israël, et dis-leur: Lorsque vous aurez passé le Jourdain et que vous serez entrés dans le pays de Chanaan,
“Sema na Waisraeli, uwaambie: ‘Mtakapovuka Yordani kuingia Kanaani,
11 vous vous choisirez des villes qui soient pour vous des villes de refuge, où pourra se retirer le meurtrier qui aura tué quelqu’un par mégarde.
chagueni baadhi ya miji iwe miji yenu ya makimbilio, ambayo mtu ambaye ameua mwenzake bila kukusudia aweza kukimbilia humo.
12 Ces villes vous serviront de refuge contre le vengeur du sang, afin que le meurtrier ne soit pas mis à mort avant d'avoir comparu en jugement devant l’assemblée.
Itakuwa mahali pa kukimbilia kutoka mlipiza kisasi, ili kwamba mtu aliyeshtakiwa kwa mauaji asife kabla ya kujitetea mbele ya mkutano.
13 Quant aux villes que vous donnerez, vous aurez six villes de refuge.
Miji hii sita mtakayoitoa itakuwa miji yenu ya makimbilio.
14 Vous donnerez trois villes au-delà du Jourdain, et vous donnerez trois villes dans le pays de Chanaan; elles seront villes de refuge.
Mtatoa miji mitatu ngʼambo hii ya Yordani na miji mingine mitatu upande wa Kanaani kama miji ya makimbilio.
15 Ces six villes serviront de refuge pour les enfants d’Israël, pour l’étranger et pour celui qui demeure au milieu de vous, afin que tout homme qui aura tué quelqu’un par mégarde puisse s’y retirer.
Miji hii sita itakuwa mahali pa makimbilio kwa ajili ya Waisraeli, wageni na watu wengine wanaoishi katikati yenu, ili kwamba mtu yeyote ambaye ameua mtu mwingine pasipo kukusudia aweze kukimbilia humo.
16 S’il l’a frappé avec un instrument de fer, et que la mort s’ensuive, c’est un meurtrier: le meurtrier sera puni de mort.
“‘Kama mtu akimpiga mwenzake kwa chuma naye mtu huyo akafa, mtu huyo ni muuaji; muuaji sharti atauawa.
17 S’il l’a frappé, ayant à la main une pierre qui peut causer la mort, et que la mort s’ensuive, c’est un meurtrier: le meurtrier sera puni de mort.
Au kama mtu analo jiwe mkononi mwake ambalo laweza kuua, naye akampiga mwenzake akafa, yeye ni muuaji; muuaji huyo sharti atauawa.
18 S’il l’a frappé, ayant à la main un instrument de bois qui peut causer la mort, et que la mort s’ensuive, c’est un meurtrier: le meurtrier sera puni de mort.
Au kama mtu ana chombo cha mti mkononi mwake ambacho chaweza kuua, naye akampiga mwenzake akafa, yeye ni muuaji; muuaji huyo sharti atauawa.
19 Le vengeur du sang fera lui-même mourir le meurtrier; quand il le rencontrera, il le tuera.
Mlipiza kisasi cha damu atamuua muuaji; wakati akikutana naye, atamuua.
20 S’il a renversé un homme par haine, ou s’il lui a jeté quelque chose en guet-apens, et que la mort s’ensuive,
Ikiwa mtu ana chuki ya siku nyingi na mwenzake akamsukuma au akamtupia kitu kwa kukusudia naye akafa,
21 ou s’il l’a frappé de sa main par inimitié, et que la mort s’ensuive, celui qui a frappé sera puni de mort, c’est un meurtrier: le vengeur du sang fera mourir le meurtrier quand il le rencontrera.
au ikiwa katika uadui akampiga ngumi naye akafa, mtu yule sharti atauawa; yeye ni muuaji. Mlipiza kisasi cha damu atamuua muuaji atakapokutana naye.
22 Mais s’il l’a renversé par hasard, sans inimitié, ou s’il lui a jeté quelque chose sans intention,
“‘Lakini kama mtu akimsukuma mwenziwe ghafula pasipo chuki, au kumtupia kitu pasipo kukusudia,
23 ou s’il a fait tomber sur lui par mégarde une pierre qui peut causer la mort, et que la mort s’ensuive, sans qu’il soit son ennemi et qu’il lui cherche du mal,
au, pasipo kumwona, akimwangushia jiwe ambalo laweza kumuua naye akafa, basi kwa kuwa hakuwa adui yake naye hakukusudia kumuumiza,
24 l’assemblée jugera entre celui qui a frappé et le vengeur du sang, selon ces lois.
kusanyiko lazima liamue kati yake na mlipiza kisasi wa damu kufuatana na sheria hizi.
25 Et l’assemblée délivrera le meurtrier du vengeur du sang et le fera retourner dans la ville de refuge où il s’était enfui; et il y demeurera jusqu’à la mort du grand prêtre qui a été oint de l’huile sainte.
Kusanyiko ni lazima limlinde yule anayeshtakiwa kuua kutoka kwa mlipiza kisasi wa damu, na kumrudisha katika mji wa makimbilio alikokuwa amekimbilia. Lazima akae humo mpaka atakapokufa kuhani mkuu ambaye alikuwa amepakwa mafuta matakatifu.
26 Si le meurtrier sort avant ce temps du territoire de la ville de refuge où il s’est enfui,
“‘Lakini kama mshtakiwa atatoka nje ya mipaka ya mji wa makimbilio ambao amekimbilia,
27 et si le vengeur du sang le rencontre hors du territoire de sa ville de refuge, et si le vengeur du sang tue le meurtrier, il ne sera pas coupable de meurtre;
na mlipiza kisasi wa damu akamkuta nje ya mji, mlipiza kisasi wa damu anaweza kumuua mshtakiwa huyo bila kuwa na hatia ya kuua.
28 car le meurtrier doit demeurer dans sa ville de refuge jusqu’à la mort du grand prêtre; et, après la mort du grand prêtre, le meurtrier pourra retourner au pays où se trouve sa possession.
Mshtakiwa lazima akae katika mji wake wa makimbilio mpaka atakapokufa kuhani mkuu; atarudi tu kwenye mali yake baada ya kifo cha kuhani mkuu.
29 Ces ordonnances fixeront le droit pour vous et pour vos descendants dans tous les lieux où vous habiterez.
“‘Hizi ndizo kanuni za sheria zitakazohitajiwa kwenu na katika vizazi vyenu vijavyo, popote mtakapoishi.
30 Quand un homme en a tué un autre, c’est sur la déposition de témoins qu’on ôtera la vie au meurtrier; mais un seul témoin ne peut déposer pour faire condamner une personne à mort.
“‘Yeyote anayeua mtu atauawa kama muuaji ikiwa tu kuna ushuhuda wa mashahidi. Lakini hakuna mtu atakayeuawa kwa ushuhuda wa shahidi mmoja tu.
31 Vous n’accepterez point de rançon pour la vie d’un meurtrier dont le crime mérite la mort, car il doit être mis à mort.
“‘Usikubali fidia yoyote ya kuokoa uhai wa muuaji ambaye anastahili kufa. Mtu huyo hakika lazima auawe.
32 Vous n’accepterez point de rançon qui permette à celui qui s’est enfui dans sa ville de refuge de revenir habiter dans son pays avant la mort du grand prêtre.
“‘Usikubali fidia ya mtu yeyote ambaye amekimbilia katika mji wa makimbilio na kumruhusu kurudi kuishi katika nchi yake kabla ya kifo cha kuhani mkuu.
33 Vous ne souillerez point le pays où vous serez, car le sang souille le pays, et il n’y a pour le pays d’expiation pour le sang qui y a été répandu, que par le sang de celui qui l’a répandu.
“‘Msiinajisi nchi mnayoishi. Umwagaji damu hunajisi nchi, na upatanisho hauwezekani kufanyika katika nchi ambayo damu imemwagwa, isipokuwa tu kwa damu ya yule aliyeimwaga damu.
34 Tu ne profaneras point le pays où vous demeurerez, et au milieu duquel j’habite; car je suis Yahweh, qui habite au milieu des enfants d’Israël. »
Msiinajisi nchi mnayoishi, ambayo nami ninakaa, kwa kuwa Mimi, Bwana, ninakaa katikati ya Waisraeli.’”

< Nombres 35 >