< Jérémie 7 >

1 La parole qui fut adressée à Jérémie de la part de Yahweh, en ces termes:
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
2 « Tiens-toi à la porte de la maison de Yahweh, et là prononce cette parole et dis: Ecoutez la parole de Yahweh, vous tous, hommes de Juda, qui entrez par ces portes pour adorer Yahweh.
“Simama kwenye lango la nyumba ya Bwana, na huko upige mbiu ya ujumbe huu: “‘Sikieni neno la Bwana, enyi watu wote wa Yuda mliokuja kupitia malango haya ili kumwabudu Bwana.
3 Ainsi parle Yahweh des armées, le Dieu d’Israël: Améliorez vos voies et vos œuvres, et je vous ferai habiter dans ce lieu.
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Tengenezeni njia zenu na matendo yenu, nami nitawaacha mkae mahali hapa.
4 Ne vous fiez pas aux paroles de mensonge de ceux qui disent: « C’est ici le temple de Yahweh, le temple de Yahweh, le temple de Yahweh! »
Msitumainie maneno ya udanganyifu na kusema, “Hili ni Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana, Hekalu la Bwana!”
5 Mais si vous améliorez vos voies et vos œuvres, si vous rendez fidèlement la justice entre un homme et son prochain;
Kama kweli mkibadili njia zenu na matendo yenu, mkatendeana haki kila mmoja na mwenzake,
6 Si vous n’opprimez pas l’étranger, l’orphelin et la veuve, si vous ne répandez pas en ce lieu le sang innocent, et si vous n’allez pas près d’autres dieux, pour votre malheur:
kama msipomwonea mgeni, yatima wala mjane, na kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa, nanyi kama msipofuata miungu mingine kwa madhara yenu wenyewe,
7 Alors je vous ferai habiter dans ce lieu, au pays que j’ai donné à vos pères, depuis les temps anciens et pour jamais.
ndipo nitawaacha mkae mahali hapa, katika nchi niliyowapa baba zenu milele na milele.
8 Mais voici que vous vous fiez à des paroles de mensonge, qui ne vous servent de rien!
Lakini tazama, mnatumainia maneno ya udanganyifu yasiyo na maana.
9 Quoi! voler, tuer, commettre l’adultère, jurer faussement, encenser Baal et aller après d’autres dieux que, vous ne connaissez pas!...
“‘Je, mtaiba na kuua, mtazini na kuapa kwa uongo, na kufukiza uvumba kwa Baali, na kufuata miungu mingine ambayo hamkuijua,
10 Et vous venez, vous vous présentez devant moi, dans cette maison sur laquelle mon nom est invoqué, et vous dites: « Nous échapperons! » Et c’est afin de commettre toutes ces abominations!
kisha mje na kusimama mbele yangu katika nyumba hii inayoitwa kwa Jina langu, mkisema, “Tuko salama.” Salama kwa kufanya mambo haya yote ya kuchukiza?
11 Est-ce donc à vos yeux une caverne de brigands, que cette maison sur laquelle mon nom est invoqué? Moi aussi, je l’ai vu, — oracle de Yahweh.
Je, nyumba hii, iitwayo kwa Jina langu, imekuwa pango la wanyangʼanyi kwenu? Lakini nimekuwa nikiona yanayotendeka! asema Bwana.
12 Allez donc à ma demeure qui était à Silo, où j’avais fait autrefois habiter mon nom, et voyez comment je l’ai traitée, à cause de la méchanceté de mon peuple d’Israël.
“‘Nendeni sasa mahali pangu palipokuwa huko Shilo, mahali ambapo nilipafanya pa kwanza kuwa makao ya Jina langu, nanyi mwone lile nililopafanyia kwa ajili ya uovu wa watu wangu Israeli.
13 Et maintenant, puisque vous avez fait toutes ces actions, — oracle de Yahweh, et que je vous ai parlé, vous parlant dès le matin, et vous n’avez pas écouté, et que je vous ai appelés, et vous n’avez pas répondu,
Mlipokuwa mnafanya yote haya, asema Bwana, nilisema nanyi tena na tena, lakini hamkusikiliza; niliwaita, lakini hamkujibu.
14 je ferai de cette maison, sur laquelle mon nom a été invoqué, dans laquelle vous mettez votre confiance, et de ce lieu que j’ai donné à vous et à vos pères, ce que j’ai fait de Silo;
Kwa hiyo, nililolifanyia Shilo, nitalifanya sasa kwa nyumba hii iitwayo kwa Jina langu, Hekalu mnalolitumainia, mahali nilipowapa ninyi na baba zenu.
15 et je vous rejetterai de devant moi, comme j’ai rejeté tous vos frères, toute la race d’Ephraïm.
Nitawafukuza mbele yangu, kama nilivyowafanyia ndugu zenu, watu wa Efraimu.’
16 Et toi, n’intercède pas en faveur de ce peuple; n’élève pour lui ni plainte ni prière, et n’insiste pas auprès de moi, car je ne t’écouterai pas.
“Kwa hiyo usiombe kwa ajili ya watu hawa, wala usinililie, na usifanye maombi kwa ajili yao; usinisihi, kwa sababu sitakusikiliza.
17 Ne vois-tu pas, ce qu’ils font dans les villes de Juda, et dans les rues de Jérusalem?
Je, huyaoni hayo wanayoyatenda katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu?
18 Les fils ramassent du bois, les pères allument le feu, les femmes pétrissent de la pâte pour faire des gâteaux à la reine du ciel, et répandre des libations à d’autres dieux, afin de m’offenser.
Watoto wanakusanya kuni, baba zao wanawasha moto, na wanawake wanakanda unga na kuoka mikate kwa ajili ya Malkia wa Mbinguni. Wanamimina sadaka za vinywaji kwa miungu mingine ili kunikasirisha.
19 Est-ce moi qu’ils offensent, — oracle de Yahweh, n’est-ce pas eux-mêmes, à la honte de leur visage?
Lakini je, mimi ndiye wanayenikasirisha? asema Bwana. Je, hawajiumizi wenyewe na kujiaibisha?
20 C’est pourquoi ainsi parle le Seigneur Yahweh: Voici que ma colère et ma fureur vont se répandre sur ce lieu, sur les hommes et sur les bêtes, sur l’arbre des champs et sur le fruit du sol; elle brûlera et ne s’éteindra point.
“‘Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenyezi: Hasira yangu na ghadhabu yangu itamwagwa mahali hapa, juu ya mwanadamu na mnyama, juu ya miti ya shambani na juu ya matunda ya ardhini, nayo itaungua pasipo kuzimwa.
21 Ainsi parle Yahweh des armées, Dieu d’Israël: Ajoutez vos holocaustes à vos sacrifices, et mangez-en la chair;
“‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Endeleeni, ongezeni sadaka zenu za kuteketezwa juu ya dhabihu zenu nyingine, mle nyama hiyo wenyewe!
22 car je n’ai pas parlé à vos pères ni ne leur ai rien prescrit, le jour où je les ai fait sortir du pays d’Égypte, en matière d’holocaustes et de sacrifices.
Kwa kuwa nilipowaleta baba zenu kutoka Misri na kusema nao, sikuwapa amri kuhusu sadaka za kuteketezwa na dhabihu tu,
23 Mais quant au commandement que je leur ai donné, je leur ai dit: Ecoutez ma voix, et je serai votre Dieu, et vous serez mon peuple; marchez dans toutes les voies que je vous prescrirai, afin que vous soyez heureux.
lakini niliwapa amri hii nikisema: Nitiini mimi, nami nitakuwa Mungu wenu nanyi mtakuwa watu wangu. Enendeni katika njia zote ninazowaamuru ili mpate kufanikiwa.
24 Mais ils n’ont pas écouté, et ils n’ont pas prêté l’oreille et ils ont marché selon leurs conseils, selon l’endurcissement de leur mauvais cœur; ils sont allés en arrière, et non en avant.
Lakini hawakusikiliza wala kujali. Badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Walirudi nyuma badala ya kusonga mbele.
25 Depuis le jour où vos pères sont sortis de la terre d’Égypte jusqu’à ce jour, je vous ai envoyé tous mes serviteurs les prophètes, les envoyant chaque jour dès le matin;
Tangu wakati ule baba zenu walipotoka Misri hadi sasa, siku baada ya siku, tena na tena nimewatumia watumishi wangu manabii.
26 mais ils ne m’ont pas écouté, ils n’ont pas prêté l’oreille; ils ont raidi leur cou, ils ont fait pis que leurs pères.
Lakini hawakunisikiliza wala hawakujali. Walikuwa na shingo ngumu na kufanya maovu kuliko baba zao.’
27 Tu leur diras toutes ces choses, ils ne t’écouteront pas; tu les appelleras, ils ne te répondront pas.
“Utakapowaambia haya yote, hawatakusikiliza; utakapowaita, hawatajibu.
28 Alors tu leur diras: C’est la nation qui n’a pas écouté la voix de Yahweh, son Dieu, et qui n’a pas accepté l’instruction; la fidélité a péri; elle a disparu de sa bouche.
Kwa hiyo waambie, ‘Hili ni taifa ambalo halimtii Bwana, Mungu wao, wala kukubali maonyo. Kweli imekufa, imetoweka midomoni mwao.
29 Rase ta chevelure, et jette-la; et entonne sur les hauteurs un chant de deuil, car Yahweh a pris en dédain et rejeté la race objet de sa colère.
Nyoeni nywele zenu na kuzitupa, ombolezeni katika miinuko iliyo kame, kwa kuwa Bwana amekikataa na kukiacha kizazi hiki kilichomkasirisha.
30 Car les fils de Juda ont fait ce qui est mal à mes yeux, — oracle de Yahweh; ils ont placé leurs abominations dans la maison sur laquelle mon nom a été invoqué, afin de la souiller;
“‘Watu wa Yuda wamefanya maovu machoni pangu, asema Bwana. Wameziweka sanamu zao za machukizo ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu, na wameitia unajisi.
31 et ils ont construit les hauts lieux de Topheth dans la vallée du fils de Hinnom, pour brûler au feu leurs fils et leurs filles, ce que je n’avais pas commandé, et ce qui ne m’était pas venu à la pensée.
Wamejenga mahali pa juu pa kuabudia sanamu pa Tofethi kwenye Bonde la Ben-Hinomu ili kuwateketeza wana wao na binti zao kwenye moto, kitu ambacho sikuamuru, wala hakikuingia akilini mwangu.
32 C’est pourquoi voici que des jours viennent, — oracle de Yahweh, où l’on ne dira plus « Topheth, » ni « Vallée du fils de Hinnom », mais « Vallée du massacre », et où l’on enterrera à Topheth, faute de place.
Kwa hiyo mjihadhari, siku zinakuja, asema Bwana, wakati watu watakapokuwa hawapaiti Tofethi au Bonde la Ben-Hinomu, lakini watapaita Bonde la Machinjo, kwa sababu watawazika wafu huko Tofethi mpaka pasiwe tena nafasi.
33 Et les cadavres de ce peuple seront la pâture des oiseaux du ciel et des bêtes de la terre, sans qu’il y ait personne pour les chasser.
Ndipo mizoga ya watu hawa itakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwafukuza.
34 Et je ferai cesser, dans les villes de Juda et dans les rues de Jérusalem, les cris de réjouissance et les cris d’allégresse, le chant de l’époux et le chant de l’épouse, car le pays sera devenu un désert.
Nitazikomesha sauti za shangwe na furaha, na sauti za bwana arusi na bibi arusi katikati ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu, kwa sababu nchi itakuwa ukiwa.

< Jérémie 7 >