< John 11 >
1 And ther was a sijk man, Lazarus of Bethanye, of the castel of Marie and Martha, hise sistris.
Basi mtu mmoja jina lake Lazaro alikuwa mgonjwa. Yeye alikuwa akiishi Bethania kijiji cha Maria na Martha dada zake.
2 And it was Marye, which anoyntide the Lord with oynement, and wipte hise feet with hir heeris, whos brother Lazarus was sijk.
Huyu Maria, ambaye Lazaro kaka yake alikuwa mgonjwa, ndiye yule ambaye alimpaka Bwana mafuta na kuifuta miguu yake kwa nywele zake.
3 Therfor hise sistris senten to hym, and seide, Lord, lo! he whom thou louest, is sijk.
Hivyo hawa dada wawili walituma ujumbe kwa Yesu kumwambia, “Bwana, yule umpendaye ni mgonjwa.”
4 And Jhesus herde, and seide to hem, This syknesse is not to the deth, but for the glorie of God, that mannus sone be glorified bi hym.
Lakini Yesu aliposikia hayo, akasema, “Ugonjwa huu hautaleta mauti bali umetokea ili kudhihirisha utukufu wa Mungu, ili Mwana wa Mungu apate kutukuzwa kutokana na ugonjwa huu.”
5 And Jhesus louyde Martha, and hir sistir Marie, and Lazarus.
Pamoja na hivyo, ingawa Yesu aliwapenda Martha, Maria na Lazaro ndugu yao,
6 Therfor whanne Jhesus herde, that he was sijk, thanne he dwellide in the same place twei daies.
baada ya kusikia kwamba Lazaro ni mgonjwa, aliendelea kukawia huko alikokuwa kwa siku mbili zaidi.
7 And after these thingis he seide to hise disciplis, Go we eft in to Judee.
Ndipo akawaambia wanafunzi wake, “Haya, turudi Uyahudi.”
8 The disciplis seien to hym, Maister, now the Jewis souyten for to stoone thee, and eft goist thou thidir?
Wanafunzi wake wakamwambia, “Rabi, Wayahudi walikuwa wanataka kukupiga mawe, nawe unataka kurudi huko?”
9 Jhesus answerde, Whether ther ben not twelue ouris of the dai? If ony man wandre in the dai, he hirtith not, for he seeth the liyt of this world.
Yesu akawajibu, “Si kuna saa kumi na mbili za mchana katika siku moja? Wala watembeao mchana hawawezi kujikwaa kwa maana wanaona nuru ya ulimwengu huu.
10 But if he wandre in the niyt, he stomblith, for liyt is not in him.
Lakini wale watembeao usiku hujikwaa kwa sababu hakuna nuru ndani yao.”
11 He seith these thingis, and aftir these thingis he seith to hem, Lazarus, oure freend, slepith, but Y go to reise hym fro sleep.
Baada ya kusema haya, Yesu akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini naenda kumwamsha.”
12 Therfor hise disciplis seiden, Lord, if he slepith, he schal be saaf.
Wanafunzi wakamwambia, “Bwana, kama amelala usingizi ataamka.”
13 But Jhesus hadde seid of his deth; but thei gessiden, that he seide of slepyng of sleep.
Hata hivyo, Yesu alikuwa anazungumzia kuwa Lazaro amekufa, lakini wanafunzi wake hawakuelewa, walidhani kwamba anasema Lazaro amelala usingizi tu.
14 Thanne therfor Jhesus seide to hem opynli, Lazarus is deed;
Kwa hiyo Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa.
15 and Y haue ioye for you, that ye bileue, for Y was not there; but go we to hym.
Hata hivyo nafurahi kwa kuwa sikuwepo huko kabla ya Lazaro kufa, ili mpate kuamini. Lakini sasa twendeni kwake.”
16 Therfor Thomas, that is seid Didymus, seide to euen disciplis, Go we also, that we dien with hym.
Tomaso aliyeitwa Pacha akawaambia wanafunzi wenzake, “Sisi nasi twendeni tukafe pamoja naye.”
17 And so Jhesus cam, and foond hym hauynge thanne foure daies in the graue.
Yesu alipowasili huko alikuta Lazaro amekuwa kaburini siku nne.
18 And Bethany was bisidis Jerusalem, as it were fiftene furlongis.
Basi Bethania ulikuwa karibu na Yerusalemu umbali wa karibu maili mbili,
19 And many of the Jewis camen to Mary and Martha, to coumforte hem of her brothir.
na Wayahudi wengi walikuwa wamekuja kuwafariji Martha na Maria kwa ajili ya kufiwa na ndugu yao.
20 Therfor as Martha herde, that Jhesu cam, sche ran to hym; but Mary sat at home.
Martha aliposikia kwamba Yesu anakuja, alitoka kwenda kumlaki, ila Maria alibaki nyumbani.
21 Therfor Martha seide to Jhesu, Lord, if thou haddist be here, my brother hadde not be deed.
Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.
22 But now Y woot, that what euere thingis thou schalt axe of God, God schal yyue to thee.
Lakini sasa ninajua kuwa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
23 Jhesus seith to hir, Thi brother schal rise ayen.
Yesu akamwambia, “Ndugu yako atafufuka.”
24 Martha seith to hym, Y woot, that he schal rise ayen in the ayen risyng in the laste dai.
Martha akamjibu, “Ninajua ya kuwa atafufuka wakati wa ufufuo wa wafu siku ya mwisho.”
25 Jhesus seith to hir, Y am ayen risyng and lijf; he that bileueth in me, yhe, thouy he be deed, he schal lyue;
Yesu akamwambia, “Mimi ndiye huo ufufuo na uzima. Yeye aniaminiye mimi, hata akifa atakuwa anaishi
26 and ech that lyueth, and bileueth in me, schal not die with outen ende. Bileuest thou this thing? (aiōn )
na yeyote aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je, unasadiki haya?” (aiōn )
27 Sche seith to hym, Yhe, Lord, Y haue bileued, that thou art Crist, the sone of the lyuynge God, that hast come in to this world.
Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana, ninaamini ya kuwa wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yeye ajaye ulimwenguni.”
28 And whanne sche hadde seid this thing, sche wente, and clepide Marie, hir sistir, in silence, and seide, The maister cometh, and clepith thee.
Baada ya kusema haya Martha alikwenda, akamwita Maria dada yake faraghani na kumwambia, “Mwalimu yuko hapa anakuita.”
29 Sche, as sche herd, aroos anoon, and cam to hym.
Maria aliposikia hivyo, akaondoka upesi akaenda mpaka alipokuwa Yesu.
30 And Jhesus cam not yit `in to the castel, but he was yit in that place, where Martha hadde comun ayens hym.
Yesu alikuwa hajaingia kijijini, bali alikuwa bado yuko mahali pale alipokutana na Martha.
31 Therfor the Jewis that weren with hir in the hous, and coumfortiden hir, whanne thei sayn Marie, that sche roos swithe, and wente out, thei sueden hir, and seiden, For sche goith to the graue, to wepe there.
Wale Wayahudi waliokuwa pamoja na Maria nyumbani wakimfariji walipoona ameondoka haraka na kutoka nje, walimfuata wakidhani ya kwamba alikuwa anakwenda kule kaburini kulilia huko.
32 But whanne Marie was comun where Jhesus was, sche seynge hym felde doun to his feet, and seide to hym, Lord, if thou haddist be here, my brother hadde not be deed.
Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa, alipiga magoti miguuni Pake na kusema, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.”
33 And therfor whanne Jhesu saiy hir wepyng, and the Jewis wepynge that weren with hir, he `made noise in spirit, and troblide hym silf,
Yesu alipomwona Maria akilia na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye pia wakilia, Yesu alisikia uchungu moyoni, akafadhaika sana.
34 and seide, Where han ye leid hym? Thei seien to hym, Lord, come, and se.
Akauliza, “Mmemweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo upaone.”
35 And Jhesus wepte. Therfor the Jewis seiden,
Yesu akalia machozi.
36 Lo! hou he louede hym.
Ndipo Wayahudi wakasema, “Tazama jinsi alivyompenda Lazaro!”
37 And summe of hem seiden, Whethir this man that openyde the iyen of the borun blynde man, myyte not make that this schulde not die?
Lakini wengine wakasema, “Je, yule aliyefungua macho ya kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife?”
38 Therfor Jhesus eft makynge noise in hym silf, cam to the graue. And there was a denne, and a stoon was leid theronne.
Yesu kwa mara nyingine akiwa amefadhaika sana, akafika penye kaburi. Hilo kaburi lilikuwa pango ambalo jiwe lilikuwa limewekwa kwenye ingilio lake.
39 And Jhesus seith, Take ye awey the stoon. Martha, the sistir of hym that was deed, seith to hym, Lord, he stynkith now, for he hath leye foure daies.
Yesu akasema, “Liondoeni hilo jiwe.” Martha ndugu yake yule aliyekuwa amekufa akasema, “Lakini Bwana, wakati huu atakuwa ananuka kwani amekwisha kuwa kaburini siku nne.”
40 Jhesus seith to hir, Haue Y not seid to thee, that if thou bileuest, thou schalt se the glorie of God?
Yesu akamwambia, “Sikukuambia kwamba kama ukiamini utauona utukufu wa Mungu?”
41 Therfor thei token awei the stoon. And Jhesus lifte vp hise iyen, and seide, Fadir, Y do thankyngis to thee, for thou hast herd me; and Y wiste,
Kwa hiyo wakaliondoa lile jiwe kutoka kaburini. Yesu akainua macho yake juu akasema, “Baba, ninakushukuru kwa kuwa wanisikia.
42 that thou euermore herist me, but for the puple that stondith aboute, Y seide, that thei bileue, that thou hast sent me.
Ninajua ya kuwa wewe hunisikia siku zote, lakini nimesema haya kwa ajili ya umati huu uliosimama hapa, ili wapate kuamini ya kuwa wewe umenituma.”
43 Whanne he hadde seid these thingis, he criede with a greet vois, Lazarus, come thou forth.
Baada ya kusema haya, Yesu akapaza sauti yake akaita, “Lazaro, njoo huku!”
44 And anoon he that was deed, cam out, boundun the hondis and feet with boondis, and his face boundun with a sudarie. And Jhesus seith to hem, Vnbynde ye hym, and suffre ye hym to go forth.
Yule aliyekuwa amekufa akatoka nje, mikono yake na miguu yake ikiwa imeviringishiwa vitambaa vya kitani na leso usoni pake. Yesu akawaambia, “Mfungueni, mwacheni aende zake.”
45 Therfor many of the Jewis that camen to Marie and Martha, and seyn what thingis Jhesus dide, bileueden in hym.
Hivyo Wayahudi wengi waliokuwa wamekuja kumfariji Maria, walipoona yale Yesu aliyoyatenda wakamwamini.
46 But summe of hem wente to the Farisees, and seiden to hem, what thingis Jhesus `hadde don.
Lakini baadhi yao wakaenda kwa Mafarisayo na kuwaambia mambo Yesu aliyoyafanya.
47 Therfor the bischopis and the Farisees gadriden a counsel ayens Jhesu, and seiden, What do we? for this man doith many myraclis.
Kwa hiyo viongozi wa makuhani na Mafarisayo wakaita mkutano wa baraza. Wakaulizana, “Tufanyeje? Huyu mtu anafanya ishara nyingi.
48 If we leeue hym thus, alle men schulen bileue in hym; and Romayns schulen come, and schulen take our place and oure folk.
Kama tukimwacha aendelee hivi, kila mtu atamwamini, nao Warumi watakuja na kupaharibu mahali petu patakatifu na taifa letu.”
49 But oon of hem, Cayfas bi name, whanne he was bischop of that yeer, seide to hem,
Mmoja wao aliyeitwa Kayafa, ambaye alikuwa kuhani mkuu mwaka huo, akasema, “Ninyi hamjui kitu chochote!
50 Ye witen nothing, ne thenken, that it spedith to you, that o man die for the puple, and that al the folc perische not.
Hamjui kwamba ni afadhali mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa lote liangamie?”
51 But he seide not this thing of hym silf, but whanne he was bischop of that yeer, he prophesiede, that Jhesu was to die for the folc,
Hakusema haya kutokana na mawazo yake mwenyewe bali kama kuhani mkuu mwaka huo, alitabiri kuwa Yesu angelikufa kwa ajili ya taifa la Wayahudi,
52 and not oneli for the folc, but that he schulde gadere in to oon the sones of God that weren scaterid.
wala si kwa ajili ya taifa hilo pekee, bali pia kwa ajili ya watoto wa Mungu waliotawanyika, ili kuwaleta pamoja na kuwafanya wawe wamoja.
53 Therfor fro that day thei souyten for to sle hym.
Hivyo tangu siku hiyo wakawa wanafanya mipango ili wamuue Yesu.
54 Therfor Jhesus walkide not thanne opynli among the Jewis; but he wente in to a cuntre bisidis desert, in to a citee, that is seid Effren, and there he dwellide with hise disciplis.
Kwa hiyo Yesu akawa hatembei hadharani miongoni mwa Wayahudi, bali alijitenga akaenda sehemu iliyo karibu na jangwa kwenye kijiji kiitwacho Efraimu. Akakaa huko na wanafunzi wake.
55 And the pask of the Jewis was niy, and many of the cuntrey wenten vp to Jerusalem bifor the pask, to halewe hem silf.
Basi Pasaka ya Wayahudi ilipokuwa imekaribia, watu wengi walitoka vijijini wakaenda Yerusalemu kabla ya Pasaka ili wakajitakase.
56 Therfor thei souyten Jhesu, and spaken togidere, stondynge in the temple, What gessen ye, for he cometh not to the feeste day?
Watu wakawa wanamtafuta Yesu, nao waliposimama kwenye eneo la Hekalu waliulizana, Je, mtu huyu hatakuja kamwe kwenye Sikukuu?
57 For the bischopis and Farisees hadden youun a maundement, that if ony man knowe where he is, that he schewe, that thei take hym.
Viongozi wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kuwa yeyote atakayejua mahali Yesu aliko, lazima atoe taarifa ili wapate kumkamata.