< Hosea 4 >
1 Sones of Israel, here ye the word of the Lord, for whi doom is to the Lord with the dwelleris of erthe; for whi trewthe is not, and merci is not, and kunnyng of the Lord is not in erthe.
Sikilizeni neno la Bwana, enyi watu wa Israeli. Bwana ana mashtaka dhidi ya wenyeji wa nchi, kwa sababu hakuna ukweli au uaminifu wa agano, hakuna ujuzi wa Mungu katika nchi.
2 Curs, and leesyng, and manquelling, and thefte, and auowtrie flowiden, and blood touchide blood.
Kuna laana, uongo, mauaji, wizi na uzinzi. Watu wamevunja mipaka yote, na damu inakuja baada ya damu.
3 For this thing the erthe schal mourne, and ech that dwellith in that lond, schal be sijk, in the beeste of the feeld, and in the brid of the eir; but also the fischis of the see schulen be gaderid togidere.
Kwa hiyo nchi inakauka, na kila mtu aliyeishi ndani yake anaangamia; wanyama katika mashamba na ndege angani, hata samaki katika bahari, wanaondolewa.
4 Netheles ech man deme not, and a man be not repreuyd; for thi puple is as thei that ayen seien the prest.
Lakini usiruhusu mtu yeyote kuleta mashtaka; msiruhusu mtu yeyote ahukumu mtu mwingine. Kwa maana ninyi ndio makuhani, ninaowashtaki.
5 And thou schalt falle to dai, and the profete also schal falle with thee; in the niyt Y made thi modir to be stille.
Ninyi makuhani mtajikwaa wakati wa mchana; manabii pia watajikwaa pamoja nanyi usiku, nami nitamwangamiza mama yako.
6 My puple was stille, for it hadde not kunnyng; for thou hast putte awei kunnyng, Y schal putte thee awei, that thou vse not presthod to me; and for thou hast foryete the lawe of thi God, also Y schal foryete thi sones.
Watu wangu wanaharibiwa kwa sababu ya ukosefu wa maarifa. Kwa sababu makuhani wamekataa maarifa, nami nitawakataa msiwe makuhani kwangu. Kwa sababu umesahau sheria yangu, ingawa mimi ni Mungu wako, nami pia nitasahau watoto wako.
7 Bi the multitude of hem, so thei synneden ayens me. Y schal chaunge the glorie of hem in to schenschipe.
Makuhani wengi waliongezeka, zaidi walifanya dhambi dhidi yangu. Walibadilisha heshima zao kwa aibu.
8 Thei schulen ete the synnes of my puple, and thei schulen reise the soulis of hem to the wickidnesse of hem.
Wanajilisha dhambi ya watu wangu; wao ni wenye tamaa zaidi ya uovu wao.
9 And it schal be, as the puple so the prest; and Y schal visite on hym the weies of hym, and Y schal yelde to him the thouytis of hym.
Itakuwa sawa kwa watu kama kwa makuhani: nitawaadhibu wote kwa matendo yao; Nitawalipa kwa matendo yao.
10 And thei schulen ete, and thei schulen not be fillid; thei diden fornicacioun, and ceessiden not, for thei forsoken the Lord in not kepynge.
Watakula lakini hawatashiba; watafanya uzinzi lakini hawataongezeka, kwa sababu wamekwenda mbali na Bwana.
11 Fornycacioun, and wiyn, and drunkenesse doen awei the herte.
Wanapenda uasherati, divai, na divai mpya, ambayo imechukua uelewa wao.
12 My puple axide in his tre, and the staf therof telde to it; for the spirit of fornicacioun disseyuede hem, and thei diden fornicacioun fro her God.
Watu wangu hutaka shauri kwa sanamu zao za mbao, na fimbo zao za kutembelea huwapa unabii. Kwa maana mawazo ya uasherati yamewadanganya, na wamefanya kama makahaba badala ya kuwa mwaminifu kwa Mungu wao.
13 On the heedis of mounteyns thei maden sacrifice, and on the litil hillis thei brenten encense vndur an ook, and a popeler, and terebynte, for the schadewe therof was good. Therfor youre douytris schulen do fornicacioun, and youre wyues schulen be auoutressis.
Wanatoa sadaka juu ya milima na kuteketeza uvumba kwenye milima, chini ya mialoni, milibua na miela, kwa sababu kivuli ni nzuri. Basi binti zenu hufanya uasherati, na binti zenu wanazini.
14 Y schal not visite on youre douytris, whanne thei don fornicacioun, and on youre wyues, whanne thei doon auowtrie; for thei lyuyden with hooris, and maden sacrifice with men turned in to wymmens condiciouns. And the puple that vndirstondith not, schal be betun.
Mimi siwaadhibu binti zako wakati wanachagua kutenda uasherati, wala binti zako wakati wazini. Kwa maana wanaume pia wanajitoa kwa makahaba, na hutoa dhabihu ili waweze kufanya vitendo vya uasherati na makahaba. Hivyo watu wasiofahamu wataangamizwa.
15 If thou, Israel, doist fornicacioun, nameli Juda trespasse not; and nyle ye entre in to Galgala, and stie ye not in to Bethauen, nether swere ye, The Lord lyueth.
Ingawa wewe, Israeli, umefanya uzinzi, lakini Yuda asiwe na hatia. Ninyi msiende Gilgali; msiende hadi Beth Aven. Wala msiape, “Aishivyo Bwana.”
16 For as a wielde cow Israel bowide awei; now the Lord schal fede hem as a lomb in broodnesse.
Kwa maana Israeli amefanya ukaidi, kama ndama mkaidi. Je! Bwana anaweza kuwaleta kwenye malisho kama kondoo mahali penye nafasi?
17 Effraym is the partener of idols, leeue thou him;
Efraimu alijiunga na sanamu; mwache peke yake.
18 the feeste of hem is departid. Bi fornicacioun thei diden fornicacioun, the defenders therof louyden to brynge schenschipe.
Hata wakati kileo chao kimeondoka wakaendelea kufanya uzinzi; watawala wake hupenda sana aibu yao.
19 The spirit boond hym in hise wyngis, and thei schulen be schent of her sacrifices.
Upepo utamfunga kwa mabawa yake; nao wataona aibu kwa sababu ya dhabihu zao.