< Genesis 13 >

1 Therfore Abram stiede fro Egipt, he, and his wijf, and alle thingis that he hadde; and Loth stiede with hym, to the south coost.
Kwa hiyo Abram akaondoka akatoka Misri na akaenda Negebu, Yeye, mke wake, na vyote alivyokuwa navyo. Lutu pia akaenda pamoja naye.
2 Forsothe he was ful riche in possessyoun of siluer and of gold.
Na sasa Abram alikuwa tajiri wa mifugo, fedha na dhahabu.
3 And he turnede ayen bi the weye in which he cam fro the south in to Bethel, `til to the place, in which bifore he hadde sett tabernacle, bitwixe Bethel and Hay,
Aliendelea na safari yake kutoka Negebu hadi Betheli, mahali ambapo hema yake ilikuwa tangu mwanzo, kati ya Betheli na mji wa Ai.
4 in the place of the auter which he made bifore, and inwardli clepide there the name of the Lord.
Akaenda mahali ambapo madhabahu ilikuwa imejengwa mwanzoni. Hapa akaliitia jina la Yahwe.
5 But also flockis of scheep, and droues of oxun, and tabernaclis weren to Loth, that was with Abram;
aliyekuwa anasafiri na Abram, alikuwa pia na ngo'mbe, makundi ya mifugo, na mahema.
6 and the lond miyte not take hem, that thei schulden dwelle togidre, for the catel of hem was myche, and thei miyten not dwelle in comyn.
Nchi haikuwatosha wote kukaa pamoja karibu kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana, kiasi kwamba hawakuweza kukaa pamoja.
7 Wherfor also strijf was maad bitwixe the keperis of flockis of Abram and of Loth. Forsothe Chananei and Feresei dwelliden in that lond in that tyme.
Pia, kulikuwa na ugomvi kati ya wachunga wanyama wa Abram na wachunga wanyama wa Lutu. Wakanaani pamoja na Waperizi walikuwa wakiishi katika nchi ile wakati huo.
8 Therfor Abram seide to Loth, Y biseche, that no strijf be bitwixe me and thee, and bitwixe my scheepherdis and thi scheepherdis; for we ben britheren.
Kwa hiyo Abram akamwambia Lutu, “Pasiwe na ugomvi kati yako na mimi, na kati ya wachunga wanyama wako na wachunga wanyama wangu; licha ya hayo sisi ni familia.
9 Lo! al the lond is bifore thee, Y biseche, departe thou fro me; if thou go to the left side, Y schal holde the riyt side; if thou chese the riyt side, Y schal go to the left side.
Je nchi hii yote haiko mbele yako? Nenda na ujitenge na mi. Ikiwa utakwenda kushoto, mimi nitakwenda kulia. au ikiwa utakwenda kulia, mimi nitakwenda kushoto.”
10 And so Loth reiside hise iyen, and seiy aboute al the cuntrei of Jordan, which was al moistid, bifor that the Lord distriede Sodom and Gomorre, as paradis of the Lord, and as Egipt, as men comen in to Segor.
Kwa hiyo Lutu akatazama, na akaona kuwa nchi yote tambarare ya Yorodani ilikuwa na maji kila mahali hadi Zoari, kama vile bustani ya Yahwe, na kama nchi ya Misri. Hii ilikuwa ni kabla Yahwe hajaiangamiza Sodoma na Gomora.
11 And Loth chees to him the cuntre aboute Jordan, and departide fro the eest; and thei weren departid ech fro his brother.
Kwa hiyo Lutu akajichagulia yeye mwenyewe nchi tambarare ya Yorodani na akasafiri mashariki, na ndugu hawa wakatengana wao kwa wao.
12 Abram dwellide in the lond of Chanaan; sotheli Loth dwellide in townes aboute Jordan, and wonide in Sodom.
Abram akaishi katika nchi ya Kanaani, na Lutu akaishi katika miji ya tambarare. Akatandaza hema zake hadi Sodoma.
13 Forsothe men of Sodom weren ful wickid, and synneris greetly bifore the Lord.
Na sasa watu wa Sodoma walikuwa waovu na wenye dhambi nyingi dhidi ya Yahwe.
14 And the Lord seide to Abram, aftir that Loth was departid fro him, Reise thin iyen forth riyt, and se fro the place in which thou art now, to the north and south, to the eest and west;
Yahwe akamwambia Abram baada ya Lutu kuondoka kwake, “Angalia kuanzia mahali ulipo simama hadi kaskazini, kusini, mashariki, na magharibi.
15 Y schal yyue al the lond which thou seest to thee and to thi seed, til in to with outen ende.
Nchi yote hii uionayo, nitakupatia wewe pamoja na uzao wako milele.
16 And Y schal make thi seed as the dust of erthe; if ony man may noumbre the dust of erthe, also he schal mowe noumbre thi seed.
Nitawafanya uzao wako kuwa wengi kama mavumbi ya nchi, kiasi kwamba kama kuna mtu anaweza kuhesabu mavumbi ya nchi, ndipo na uzao wako pia utahesabika.
17 Therfor rise thou, and passe thorou the lond in his lengthe and breede, for Y schal yyue it to thee.
Inuka, tembea katika urefu na upana wa nchi hii, kwa kuwa nitakupatia.”
18 Therfor Abram, mouynge his tabernacle, cam and dwellide bisidis the valei of Mambre, which is in Ebron; and he bildide there an auter to the Lord.
Kwa hiyo Abram akachukua hema yake, akaja na kukaa katika mwaloni wa Mamre, ambao uko Hebroni, na pale akajenga Madhabahu ya Yahwe.

< Genesis 13 >