< 1 Corinthians 14 >
1 Sue ye charite, loue ye spiritual thingis, but more that ye prophecien.
Fuateni upendo na kutaka sana karama za roho, hasa karama ya unabii.
2 And he that spekith in tunge, spekith not to men, but to God; for no man herith. But the spirit spekith mysteries.
Kwa maana mtu yeyote anayesema kwa lugha, hasemi na wanadamu bali anasema na Mungu. Kwa kuwa hakuna mtu yeyote anayemwelewa, kwani anasema mambo ya siri kwa roho.
3 For he that prophecieth, spekith to men to edificacioun, and monestyng, and coumfortyng.
Lakini anayetoa unabii anasema na watu akiwajenga, kuwatia moyo na kuwafariji.
4 He that spekith in tunge, edifieth hym silf; but he that prophecieth, edifieth the chirche of God.
Anenaye kwa lugha hujijenga mwenyewe, bali atoaye unabii hulijenga kanisa.
5 And Y wole, that alle ye speke in tungis, but more that ye prophecie. For he that prophecieth, is more than he that spekith in langagis; but perauenture he expoune, that the chirche take edificacioun.
Ningependa kila mmoja wenu anene kwa lugha lakini ningependa zaidi nyote mtoe unabii. Kwa kuwa yeye atoaye unabii ni mkuu kuliko anenaye kwa lugha, isipokuwa atafsiri, ili kanisa lipate kujengwa.
6 But now, britheren, if Y come to you, and speke in langagis, what schal Y profite to you, but if Y speke to you ethir in reuelacioun, ethir in science, ethir in prophecie, ether in techyng?
Sasa ndugu zangu, kama nikija kwenu nikasema kwa lugha mpya nitawafaidia nini kama sikuwaletea ufunuo au neno la maarifa au unabii au mafundisho?
7 For tho thingis that ben withouten soule, and yyueth voices, ethir pipe, ether harpe, but tho yyuen distinccioun of sownyngis, hou schal it be knowun that is sungun, ether that that is trumpid?
Hata vitu visivyo na uhai vitoapo sauti, kama vile filimbi au kinubi, mtu atajuaje ni wimbo gani unaoimbwa kusipokuwa na tofauti ya upigaji?
8 For if a trumpe yyue an vncerteyn soune, who schal make hym silf redi to batel?
Tena kama tarumbeta haitoi sauti inayoeleweka, ni nani atakayejiandaa kwa ajili ya vita?
9 So but ye yyuen an opyn word bi tunge, hou schal that that is seid be knowun? For ye schulen be spekynge in veyn.
Vivyo hivyo na ninyi, kama mkinena maneno yasiyoeleweka katika akili, mtu atajuaje mnalosema? Kwa maana mtakuwa mnasema hewani tu.
10 There ben many kyndis of langagis in this world, and no thing is with outen vois.
Bila shaka ziko sauti nyingi ulimwenguni, wala hakuna isiyo na maana.
11 But if Y knowe not the vertu of a vois, Y schal be to hym, to whom Y schal speke, a barbarik; and he that spekith to me, schal be a barbarik.
Basi kama sielewi maana ya hiyo sauti, nitakuwa mgeni kwa yule msemaji, naye atakuwa mgeni kwangu.
12 So ye, for ye ben loueris of spiritis, seke ye that ye be plenteuouse to edificacioun of the chirche.
Vivyo hivyo na ninyi. Kwa kuwa mnatamani kuwa na karama za rohoni, jitahidini kuzidi sana katika karama kwa ajili ya kulijenga kanisa.
13 And therfor he that spekith in langage, preie, that he expowne.
Kwa sababu hii, yeye anenaye kwa lugha na aombe kwamba apate kutafsiri kile anachonena.
14 For if Y preye in tunge, my spirit preieth; myn vndurstondyng is with outen fruyt.
Kwa maana nikiomba kwa lugha, roho yangu inaomba, lakini akili yangu haina matunda.
15 What thanne? Y schal preye in spirit, Y schal preye in mynde; Y schal seie salm, in spirit, Y schal seie salm also in mynde.
Nifanyeje basi? Nitaomba kwa roho, na pia nitaomba kwa akili yangu. Nitaimba kwa roho na nitaimba kwa akili yangu pia.
16 For if thou blessist in spirit, who fillith the place of an ydiot, hou schal he seie Amen on thi blessyng, for he woot not, what thou seist?
Ikiwa unabariki kwa roho, mtu mwingine atakayejikuta miongoni mwa hao wasiojua, atawezaje kusema “Amen” katika kushukuru kwako, wakati haelewi unachosema?
17 For thou doist wel thankyngis, but an othir man is not edefied.
Mnaweza kuwa mnatoa shukrani kweli, sawa, lakini huyo mtu mwingine hajengeki.
18 Y thanke my God, for Y speke in the langage of alle you;
Namshukuru Mungu kwamba mimi nanena kwa lugha kuliko ninyi nyote.
19 but in the chirche Y wole speke fyue wordis in my wit, that also Y teche othere men, than ten thousynde of wordis in tunge.
Lakini ndani ya kanisa ni afadhali niseme maneno matano ya kueleweka ili niwafundishe wengine kuliko kusema maneno 10,000 kwa lugha.
20 Britheren, nyle ye be maad children in wittis, but in malice be ye children; but in wittis be ye parfit.
Ndugu zangu, msiwe kama watoto katika kufikiri kwenu, afadhali kuhusu uovu mwe kama watoto wachanga, lakini katika kufikiri kwenu, mwe watu wazima.
21 For in the lawe it is writun, That in othere tungis and othere lippis Y schal speke to this puple, and nether so thei schulen here me, seith the Lord.
Katika Sheria imeandikwa kwamba: “Kupitia kwa watu wenye lugha ngʼeni na kupitia midomo ya wageni, nitasema na watu hawa, lakini hata hivyo hawatanisikiliza,” asema Bwana.
22 Therfor langagis ben in to tokene, not to feithful men, but to men out of the feith; but prophecies ben not to men out of the feith, but to feithful men.
Basi kunena kwa lugha ni ishara, si kwa watu waaminio, bali kwa wasioamini, wakati unabii si kwa ajili ya wasioamini, bali kwa ajili ya waaminio.
23 Therfor if alle the chirche come togidere in to oon, and alle men speken in tungis, if idiotis, ether men out of the feith, entren, whether thei schulen not seie, What ben ye woode?
Kwa hiyo kama kanisa lote likikutana na kila mmoja akanena kwa lugha, kisha wakaingia wageni wasioelewa wasioamini, je, hawatasema kwamba wote mna wazimu?
24 But if alle men prophecien, if ony vnfeithful man or idiot entre, he is conuyct of alle, he is wiseli demyd of alle.
Lakini kama mtu asiyeamini au asiyeelewa akiingia wakati kila mtu anatoa unabii, ataaminishwa na watu wote kuwa yeye ni mwenye dhambi na kuhukumiwa na wote,
25 For the hid thingis of his herte ben knowun, and so he schal falle doun on the face, and schal worschipe God, and schewe verili that God is in you.
nazo siri za moyo wake zitawekwa wazi. Kwa hiyo ataanguka chini na kumwabudu Mungu akikiri, “Kweli Mungu yuko katikati yenu!”
26 What thanne, britheren? Whanne ye comen togidere, ech of you hath a salm, he hath techyng, he hath apocalips, he hath tunge, he hath expownyng; alle thingis be thei don to edificacioun.
Basi tuseme nini ndugu zangu? Mnapokutana pamoja, kila mmoja ana wimbo, au neno la mafundisho, au ufunuo, lugha mpya au atatafsiri. Mambo yote yatendeke kwa ajili ya kulijenga kanisa.
27 Whether a man spekith in tunge, bi twei men, ethir thre at the moste, and bi partis, that oon interprete.
Kama mtu yeyote akinena kwa lugha, basi waseme watu wawili au watatu si zaidi, mmoja baada ya mwingine na lazima awepo mtu wa kutafsiri.
28 But if there be not an interpretour, be he stille in the chirche, and speke he to hym silf and to God.
Lakini kama hakuna mtu wa kutafsiri, hao watu na wanyamaze kimya kanisani na wanene na nafsi zao wenyewe na Mungu.
29 Prophetis tweine or thre seie, and othere wiseli deme.
Manabii wawili au watatu wanene na wengine wapime yale yasemwayo.
30 But if ony thing be schewid to a sittere, the formere be stille.
Kama mtu yeyote aliyeketi karibu, akipata ufunuo, basi yule wa kwanza na anyamaze.
31 For ye moun `prophecie alle, ech bi hym silf, that alle men lerne, and alle moneste.
Kwa maana wote mnaweza kutoa unabii, mmoja baada ya mwingine, ili kila mtu apate kufundishwa na kutiwa moyo.
32 And the spiritis of prophetis ben suget to prophetis;
Roho za manabii huwatii manabii.
33 for whi God is not of discencioun, but of pees; as in alle chirchis of hooli men `Y teche.
Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko bali ni Mungu wa amani. Kama ilivyo katika makusanyiko yote ya watakatifu,
34 Wymmen in chirchis be stille; for it is not suffrid to hem to speke, but to be suget, as the lawe seith.
wanawake wanapaswa kuwa kimya kanisani. Hawaruhusiwi kusema, bali wanyenyekee kama sheria isemavyo.
35 But if thei wolen ony thing lerne, `at home axe thei her hosebondis; for it is foule thing to a womman to speke in chirche.
Kama wakitaka kuuliza kuhusu jambo lolote, wawaulize waume zao nyumbani. Kwa maana ni aibu kwa mwanamke kuzungumza kanisani.
36 Whether `of you the word of God cam forth, or to you aloone it cam?
Je, neno la Mungu lilianzia kwenu? Au ni ninyi tu ambao neno la Mungu limewafikia?
37 If ony man is seyn to be a prophete, or spiritual, knowe he tho thingis that Y write to you, for tho ben the comaundementis of the Lord.
Kama mtu yeyote akidhani kwamba yeye ni nabii, au ana karama za rohoni, basi na akubali kwamba haya ninayoandika ni maagizo kutoka kwa Bwana.
38 And if ony man vnknowith, he schal be vnknowun.
Kama mtu akipuuza jambo hili yeye mwenyewe atapuuzwa.
39 `Therfor, britheren, loue ye to prophecie, and nyle ye forbede to speke in tungis.
Kwa hiyo ndugu zangu, takeni sana kutoa unabii na msikataze watu kusema kwa lugha.
40 But be alle thingis don onestli, and bi due ordre in you.
Lakini kila kitu kitendeke kwa heshima na kwa utaratibu.