< Luke 18 >
1 And He spake also a parable to them, to shew that men ought always to pray, and not to faint:
Basi, Yesu aliwasimulia mfano kuonyesha kwamba ni lazima kusali daima bila kukata tamaa.
2 saying, There was a judge in a certain city, who neither feared God, nor regarded man.
Alisema: “Katika mji mmoja kulikuwa na hakimu ambaye hakuwa anamcha Mungu wala kumjali binadamu.
3 And there was a widow in that city, who came to him, saying, Do me justice of my adversary.
Katika mji huohuo, kulikuwa pia na mama mmoja mjane, ambaye alimwendea huyo hakimu mara nyingi akimwomba amtetee apate haki yake kutoka kwa adui yake.
4 And he would not for a time: but afterwards he said within himself, Though I fear not God,
Kwa muda mrefu huyo hakimu hakupenda kumtetea huyo mjane; lakini, mwishowe akajisemea: Ingawa mimi simchi Mungu wala simjali binadamu,
5 nor regard man, yet because this widow gives me trouble, I will do her justice, least by continually coming she weary me out.
lakini kwa vile huyu mjane ananisumbua, nitamtetea; la sivyo ataendelea kufika hapa, na mwisho atanichosha kabisa!”
6 And the Lord said, hear what even the unjust judge saith:
Basi, Bwana akaendelea kusema, “Sikieni jinsi alivyosema huyo hakimu mbaya.
7 and will not God do justice for his elect that cry to Him day and night, though He bear long with them.
Je, ndio kusema Mungu hatawatetea wale aliowachagua, ambao wanamlilia mchana na usiku? Je, atakawia kuwasikiliza?
8 I tell you, He will avenge them speedily. And yet when the Son of man cometh, shall He find faith in the land?
Nawaambieni atawatetea upesi. Hata hivyo, je, kutakuwako na imani duniani wakati Mwana wa Mtu atakapokuja?”
9 And He spake also this parable to some that trusted in themselves as being righteous, and despised others.
Halafu Yesu aliwaambia pia mfano wa wale ambao walijiona kuwa wema na kuwadharau wengine.
10 Two men went up to the temple to pray; the one a pharisee and the other a publican.
“Watu wawili walipanda kwenda Hekaluni kusali: mmoja Mfarisayo, na mwingine mtoza ushuru.
11 The pharisee standing by himself prayed thus, O God, I thank thee that I am not as other men are, rapacious, unjust, adulterous, or even as this publican.
Huyo Mfarisayo akasimama, akasali kimoyomoyo: Ee Mungu, nakushukuru kwa vile mimi si kama watu wengine: walafi, wadanganyifu au wazinzi. Nakushukuru kwamba mimi si kama huyu mtoza ushuru.
12 I fast twice a week, and I give tithes of all that I possess.
Nafunga mara mbili kwa juma, natoa zaka sehemu ya kumi ya pato langu.
13 But the publican standing at a distance did not presume so much as to lift up his eyes to heaven, but smote upon his breast, saying, O God, be merciful to me a sinner.
Lakini yule mtoza ushuru, akiwa amesimama kwa mbali bila hata kuinua macho yake mbinguni, ila tu akijipiga kifua kwa huzuni, alisema: Ee Mungu, unionee huruma mimi mwenye dhambi.
14 I tell you, this man went down to his house justified rather than the other: for whoever exalteth himself shall be abased, but he that humbleth himself shall be exalted.
Nawaambieni, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amesamehewa. Lakini yule mwingine, sivyo. Kwa maana kila anayejikweza atashushwa, na kila anayejishusha atakwezwa.”
15 And they brought to Him infants also, that He might touch them: and his disciples seeing it rebuked them.
Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono yake. Wanafunzi walipowaona, wakawazuia kwa maneno makali.
16 But Jesus called them to Him and said, Suffer little children to come unto me, and forbid them not: for of such is the kingdom of God.
Lakini Yesu akawaita kwake akisema: “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu kama hawa.
17 Verily I tell you, Whosoever shall not receive the kingdom of God as a little child shall by no means enter into it.
Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hataingia katika Ufalme huo.”
18 And a certain ruler asked Him, saying, Good master, what shall I do to inherit eternal life? (aiōnios )
Kiongozi mmoja, Myahudi, alimwuliza Yesu, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niweze kuupata uzima wa milele?” (aiōnios )
19 And Jesus said unto him, Why callest thou me good? there is none good but one, that is God.
Yesu akamwambia, “Mbona waniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
20 Thou knowest the commandments, Do not commit adultery, Do not kill, Do not steal, Do not bear false witness, Honour thy father and thy mother.
Unazijua amri: Usizini; usiue; usiibe; usitoe ushahidi wa uongo; waheshimu baba yako na mama yako.”
21 And he said, all these have I kept from my youth.
Yeye akasema, “Hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu.”
22 But when Jesus heard these things He said unto him, Thou yet wantest one thing, Sell all that thou hast, and distribute to the poor, and thou shalt have treasure in heaven: and come, follow me.
Yesu aliposikia hayo akamwambia, “Unatakiwa bado kufanya kitu kimoja: uza kila ulicho nacho, wagawie maskini, na hivyo utakuwa na hazina yako mbinguni; halafu njoo unifuate.”
23 But when he heard this, he was very sorrowful; for he was very rich.
Lakini huyo mtu aliposikia hayo, alihuzunika sana kwa sababu alikuwa tajiri sana.
24 And when Jesus saw that he was very sorrowful, He said, How difficultly shall they that have riches enter into the kingdom of God?
Yesu alipoona akihuzunika hivyo, akasema, “Jinsi gani ilivyo vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!
25 For it is easier for a camel to go through the eye of a needle, than for a rich man to enter into the kingdom of God.
Naam, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
26 And they that heard it said, Who then can be saved?
Wale watu waliposikia hayo, wakasema, “Nani basi, atakayeokolewa?”
27 But He answered, Things impossible with men are possible with God.
Yesu akajibu, “Yasiyowezekana kwa binadamu, yanawezekana kwa Mungu.”
28 Then said Peter, Behold, we have quitted all, and followed Thee.
Naye Petro akamwuliza, “Na sisi je? Tumeacha vitu vyote tukakufuata!”
29 And He said unto them, Verily I tell you, there is no one that hath left house, or parents, or brethren, or wife, or children, for the sake of the kingdom of God,
Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, mtu yeyote aliyeacha nyumba au mke au kaka au wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,
30 who shall not receive manifold more even in this life, and in the world to come life everlasting. (aiōn , aiōnios )
atapokea mengi zaidi wakati huu wa sasa, na kupokea uzima wa milele wakati ujao.” (aiōn , aiōnios )
31 And He took the twelve with Him and said to them, Behold, we are going up to Jerusalem, and all things written by the prophets concerning the Son of man shall be accomplished.
Yesu aliwachukua kando wale kumi na wawili, akawaambia, “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu na huko kila kitu kilichoandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Mtu kitakamilishwa.
32 For He shall be delivered to the Gentiles, and insulted, and abused, and spit upon, and they will scourge Him, and put Him to death:
Kwa maana atakabidhiwa kwa watu wa mataifa nao watamtendea vibaya na kumtemea mate.
33 and the third day He shall rise again.
Watampiga mijeledi, watamuua; lakini siku ya tatu atafufuka.”
34 But they understood none of these things; and this matter was hid from them, so that they knew not the things which were spoken.
Lakini wao hawakuelewa hata kidogo jambo hilo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.
35 And as he was near to Jericho, a certain blind man sat by the way-side begging.
Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.
36 And hearing a multitude passing by, he asked what it meant.
Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, “Kuna nini?”
37 And they told him, Jesus of Nazareth is coming by.
Wakamwambia, “Yesu wa Nazareti anapita.”
38 And he cried out, saying, Jesus, thou son of David, have compassion on me.
Naye akapaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
39 And they, that went before, rebuked him, that he might hold his peace, but he cried out the more, O Son of David, have pity on me.
Wale watu waliotangulia wakamkemea wakimwambia anyamaze; lakini yeye akazidi kupaza sauti: “Mwana wa Daudi, nihurumie;”
40 So Jesus stopt, and ordered him to be brought to Him: and when he was come near,
Yesu alisimama, akaamuru wamlete mbele yake. Yule kipofu alipofika karibu, Yesu akamwuliza,
41 He asked him, saying, What wouldst thou that I should do for thee? And he said, Lord, that I may recover my sight.
“Unataka nikufanyie nini?” Naye akamjibu, “Bwana, naomba nipate kuona tena.”
42 And Jesus said unto him, Receive thy sight: thy faith hath saved thee.
Yesu akamwambia, “Ona! Imani yako imekuponya.”
43 And immediately he received his sight, and followed Him, glorifying God: and all the people, when they saw it, gave praise unto God.
Na mara yule aliyekuwa kipofu akapata kuona, akamfuata Yesu akimtukuza Mungu. Watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.