< John 4 >

1 Therefore when the Lord knew, the pharisees had heard that Jesus made and baptized more disciples than John,
Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane.
2 (though Jesus Himself did not baptize, but his disciples, )
(Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.)
3 He left Judea, and departed again into Galilee.
Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya;
4 And as He must pass through the country of Samaria, He came to a Samaritan city called Sichar,
na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.
5 near the piece of ground which Jacob gave to his son Joseph.
Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu.
6 And Jacob's well was there. Now Jesus was tired with his journey, and sat down at the well: and it was about the sixth hour of the day,
Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
7 when a woman of Samaria coming to draw water, Jesus saith unto her, Give me to drink.
Basi, mwanamke mmoja Msamaria akafika kuteka maji. Yesu akamwambia, “Nipatie maji ninywe.”
8 (For his disciples were gone away to the city to buy food.)
(Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
9 But the Samaritan saith unto Him, How is it that thou who art a Jew askest drink of me, who am a Samaritan? for the Jews have no friendly intercourse with the Samaritans.
Lakini huyo mwanamke akamwambia, “Wewe ni Myahudi; mimi ni mwanamke Msamaria! Unawezaje kuniomba maji?” (Wayahudi hawakuwa na ushirikiano na Wasamaria katika matumizi ya vitu.)
10 Jesus answered and said unto her, If thou knewest the gift of God, and who it is that saith unto thee, Give me to drink; thou wouldst have asked of Him, and He would have given thee living water.
Yesu akamjibu, “Kama tu ungalijua zawadi ya Mungu na ni nani anayekwambia: Nipatie maji ninywe, ungalikwisha mwomba, naye angekupa maji yaliyo hai.”
11 The woman saith unto Him, Sir, thou hast nothing to draw with, and the well is deep: whence then hast thou the living water?
Huyo mama akasema, “Mheshimiwa, wewe huna chombo cha kutekea maji, nacho kisima ni kirefu; utapata wapi maji yaliyo hai?
12 Art thou greater than our father Jacob, who gave us the well, and drank of it himself, and his children, and his cattle?
Au, labda wewe wajifanya mkuu kuliko babu yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo yake walikunywa maji ya kisima hiki.”
13 Jesus answered and said unto her, Whosoever drinketh of this water, will thirst again;
Yesu akamjibu, “Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena.
14 but he that drinketh of the water which I shall give him, shall never thirst: but the water, which I shall give him, will be in him a fountain of water springing up unto eternal life. (aiōn g165, aiōnios g166)
Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
15 The woman saith unto Him, Sir, give me this water, that I may not thirst, nor come hither to draw.
Huyo mwanamke akamwambia, “Mheshimiwa, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; nisije tena mpaka hapa kuteka maji.”
16 Jesus saith unto her, Go call thine husband, and come hither.
Yesu akamwambia, “Nenda ukamwite mumeo uje naye hapa.”
17 The woman answered, I have no husband. Jesus saith unto her, Thou hast said right, I have no husband:
Huyo mwanamke akamwambia, “Mimi sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli, kwamba huna mume.
18 for thou hast had five husbands; and he, whom thou now hast, is not thy husband: this thou hast said true.
Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli.”
19 The woman saith unto Him, Sir, I perceive that thou art a prophet.
Huyo Mwanamke akamwambia, “Mheshimiwa, naona ya kuwa wewe u nabii.
20 Our fathers worshipped on this mountain, and ye say that in Jerusalem is the place where men ought to worship.
Babu zetu waliabudu juu ya mlima huu, lakini ninyi mwasema kwamba mahali pa kumwabudu Mungu ni kule Yerusalemu.”
21 Jesus saith unto her, Woman, believe me, the time is coming, when ye shall worship the Father neither on this mountain nor in Jerusalem.
Yesu akamwambia, “Niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba juu ya mlima huu, wala kule Yerusalemu.
22 Ye worship ye know not what; but we worship what we know: for salvation is from the Jews.
Ninyi Wasamaria mnamwabudu yule msiyemjua, lakini sisi tunamjua huyo tunayemwabudu, kwa maana wokovu unatoka kwa Wayahudi.
23 But the time is coming, and now is, when the true worshippers shall worship the Father in spirit and truth: for the Father requireth such worshippers of Him.
Lakini wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wanaoabudu kweli, watamwabudu Baba kwa nguvu ya Roho; watu wanaomwabudu hivyo ndio Baba anaotaka.
24 God is a spirit, and they that worship Him, must worship in spirit and truth.
Mungu ni Roho, na watu wataweza tu kumwabudu kweli kwa nguvu ya Roho wake.”
25 Then saith the woman unto Him, I know that the Messiah, that is to say the Christ, is coming; and when He comes, He will tell us all things.
Huyo mama akamwambia, “Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu.”
26 Jesus saith unto her, I, who am talking to thee, am He.
Yesu akamwambia, “Mimi ninayesema nawe, ndiye.”
27 And upon this came his disciples and wondered that He talked with the woman: (though none of them said, What dost thou seek? or, Why dost thou talk with her?)
Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: “Unataka nini?” au, “Kwa nini unaongea na mwanamke?”
28 therefore the woman left her water-pot, and went away into the city,
Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu,
29 and saith to the people, Come, see a man who hath told me all that ever I did; is not this the Christ?
“Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?”
30 They therefore went out of the city, and came to Him.
Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu.
31 In the mean time his disciples addressed Him, saying, Master, eat.
Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: “Mwalimu, ule chakula.”
32 But He said unto them, I have food to eat, which ye know not of.
Lakini Yesu akawaambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.”
33 Therefore the disciples said one to another, Hath any one brought Him aught to eat?
Wanafunzi wake wakaulizana, “Je, kuna mtu aliyemletea chakula?”
34 Jesus saith unto them, My food is to do the will of Him that sent me, and to finish his work.
Yesu akawaambia, “Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.
35 Do not ye say, it is yet four months, and then cometh harvest? Behold, lift up your eyes, and see the fields, they are already white for harvest.
Ninyi mwasema: Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika! Lakini mimi nawaambieni, yatazameni mashamba; mazao yako tayari kuvunwa.
36 And he that reapeth receiveth wages, and gathereth the fruit together unto life eternal: that both he that soweth and he that reapeth may rejoice together; (aiōnios g166)
Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja. (aiōnios g166)
37 for herein the saying is verified, that one soweth, and another reapeth,
Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: Mmoja hupanda na mwingine huvuna.
38 in as much as I have sent you to reap that on which ye have not laboured: others have laboured, and ye are entered into their labors.
Mimi nimewatuma mkavune mavuno ambayo hamkuyatolea jasho, wengine walifanya kazi, lakini ninyi mnafaidika kutokana na jasho lao.”
39 And many of the Samaritans of that city believed on Him, because of what the woman said, testifying, He told me all that ever I did.
Wasamaria wengi wa kijiji kile waliamini kwa sababu ya maneno aliyosema huyo mama: “Ameniambia mambo yote niliyofanya.”
40 Therefore when the Samaritans came to Him, they desired Him to stay with them: and He staid there two days.
Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili.
41 And many more believed on account of his own discourse:
Watu wengi zaidi walimwamini kwa sababu ya ujumbe wake.
42 and said to the woman, Now we believe, not because of what thou hast spoken; for we ourselves have heard Him, and know that this is indeed the Christ, the Saviour of the world.
Wakamwambia yule mama, “Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu.”
43 And after two days he departed thence, and went into Cana of Galilee.
Baada ya siku mbili Yesu aliondoka hapo, akaenda Galilaya.
44 For Jesus himself had testified that a prophet hath no honor in his own country.
Maana Yesu mwenyewe alisema waziwazi kwamba, “Nabii hapati heshima katika nchi yake.”
45 And when He was come into Galilee, the Galileans received Him, having seen all that he did in Jerusalem at the feast: for they also went to the feast.
Basi, alipofika Galilaya, Wagalilaya wengi walimkaribisha. Maana nao pia walikuwa kwenye sikukuu ya Pasaka, wakayaona mambo yote Yesu aliyotenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu hiyo.
46 Therefore Jesus came again into Cana of Galilee, where He had made the water wine.
Yesu alifika tena huko mjini Kana, mkoani Galilaya, mahali alipogeuza maji kuwa divai. Kulikuwa na ofisa mmoja aliyekuwa na mtoto mgonjwa huko Kafarnaumu.
47 And there was a certain nobleman, whose son was sick at Capernaum: who, when he heard that Jesus was come out of Judea into Galilee, went to Him, and intreated Him, that he would come down and heal his son; for he was at the point of death.
Basi, huyo ofisa aliposikia kuwa Yesu alikuwa ametoka Yudea na kufika Galilaya, alimwendea akamwomba aende kumponya mtoto wake aliyekuwa mgonjwa mahututi.
48 Jesus therefore said unto him, Except ye see signs and wonders ye will not believe.
Yesu akamwambia, “Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!”
49 The nobleman saith unto Him, Lord, come down before my child die.
Huyo ofisa akamwambia, “Mheshimiwa, tafadhali twende kabla mwanangu hajafa.”
50 Jesus saith unto him, Go, thy son is well. And the man believed what Jesus said unto him, and went his way.
Yesu akamwambia, “Nenda tu, mwanao yu mzima.” Huyo mtu akaamini maneno ya Yesu, akaenda zake.
51 And as he was now going down, his servants met him and told him, saying, Thy son is well.
Alipokuwa bado njiani, watumishi wake walikutana naye, wakamwambia kwamba mwanawe alikuwa mzima.
52 He inquired therefore of them the hour in which he grew better: and they said unto him, Yesterday at the seventh hour the fever left him.
Naye akawauliza saa mtoto alipopata nafuu; nao wakamwambia, “Jana saa saba mchana, homa ilimwacha.”
53 So the father knew that it was in that same hour, in which Jesus said to him, Thy son is well. And he and his whole family believed.
Huyo baba akakumbuka kwamba ilikuwa ni saa ileile ambapo Yesu alimwambia: “Mwanao yu mzima.” Basi, yeye akaamini pamoja na jamaa yake yote.
54 This is the second miracle that Jesus wrought, upon coming out of Judea into Galilee.
Hii ilikuwa ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipokuwa anatoka Yudea kwenda Galilaya.

< John 4 >