< Acts 3 >

1 Now Peter and John were going up to the temple together at the hour of prayer, which is the ninth hour.
Siku moja, saa tisa alasiri, Petro na Yohane walikuwa wanakwenda Hekaluni, wakati wa sala.
2 And a certain man who had been lame from his birth was carried along; whom they laid every day at the gate of the temple, which is called Beautiful, to ask alms of those that were going into the temple:
Na pale karibu na mlango wa Hekalu uitwao “Mlango Mzuri”, palikuwa na mtu mmoja, kiwete tangu kuzaliwa. Watu walimbeba huyo mtu kila siku na kumweka hapo ili aombe chochote kwa wale waliokuwa wakiingia Hekaluni.
3 who seeing Peter and John about to go into the temple, asked alms of them.
Alipowaona Petro na Yohane wakiingia Hekaluni, aliwaomba wampe chochote.
4 But Peter, and John, looking earnestly at him said, Look on us.
Petro na Yohane walimkodolea macho, naye Petro akamwambia, “Tutazame!”
5 And he fixed his eyes upon them, expecting to receive something from them.
Naye akawageukia, akitazamia kupata kitu kutoka kwao.
6 But Peter said, Silver and gold I have not; but what I have I give thee: In the name of Jesus Christ of Nazareth, rise up and walk.
Kisha Petro akamwambia, “Sina fedha wala dhahabu lakini kile nilicho nacho nitakupa. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, tembea!”
7 And taking him by the right hand, he raised him up: and immediately his feet and ancles were strengthened:
Halafu, akamshika mkono wa kulia, akamwinua. Papo hapo miguu na magoti yake yakapata nguvu.
8 and leaping up he stood firm, and walked; and entered with them into the temple, walking, and leaping, and praising God.
Akaruka, akasimama na kuanza kutembea. Halafu akaingia pamoja nao Hekaluni, akitembea na kurukaruka huku akimtukuza Mungu.
9 And all the people saw him walking and praising God:
Watu wote waliokuwa hapo walimwona akitembea na kumsifu Mungu.
10 and knew that it was he who sat to ask for alms at the Beautiful gate of the temple: and they were filled with astonishment and extasy at what had befallen him.
Walipomtambua kuwa ndiye yule aliyekuwa anaombaomba karibu na ule “Mlango Mzuri” wa Hekalu, wakashangaa mno hata wasiweze kuelewa yaliyompata.
11 And as the lame man that was healed had hold of Peter and John, all the people being astonished ran together to them to the porch called Solomon's porch.
Watu wote, wakiwa na mshangao mkubwa wakaanza kukimbilia mahali palipoitwa “Ukumbi wa Solomoni,” ambapo yule mtu alikuwa bado anaandamana na Petro na Yohane.
12 And Peter seeing this said to the people, Men of Israel, why marvel ye at this, or why look ye so earnestly on us, as if by our own power or piety we had made this man able to walk?
Basi, Petro alipowaona watu hao akawaambia, “Wananchi wa Israeli, kwa nini mnashangazwa na jambo hili? Mbona mnatukodolea macho kana kwamba ni kwa nguvu zetu au utakatifu wetu sisi wenyewe tumemfanya mtu huyu aweze kutembea?
13 The God of Abraham and of Isaac and of Jacob, the God of our fathers hath glorified his son Jesus, whom ye delivered up, and denied before Pilate, when he determined to release Him.
Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa baba zetu amemtukuza Yesu mtumishi wake. Yeye ndiye yuleyule mliyemtia mikononi mwa wakuu na kumkataa mbele ya Pilato hata baada ya Pilato kuamua kumwacha huru.
14 But ye refused the holy and righteous One, and desired a murderer to be granted unto you:
Alikuwa mtakatifu na mwema; lakini ninyi mlimkataa, mkataka mtu mwingine aliyekuwa muuaji afunguliwe.
15 and put to death the prince of life; whom God hath raised from the dead, of which we are witnesses.
Basi, mlimuua yule ambaye ni chanzo cha uzima. Lakini Mungu alimfufua, na sisi ni mashahidi wa tukio hilo.
16 And through faith in his name, hath strengthened this man, whom ye see and know: his name, I say, and saith in Him, hath wrought this perfect cure before you all.
Jina la Yesu na imani katika jina hilo ndivyo vilivyompa nguvu mtu huyu mnayemwona na kumfahamu. Imani kwa Yesu ndiyo iliyomponya kabisa mtu huyu kama mnavyoona nyote.
17 And now, brethren, I know that ye did it through ignorance, as did also your rulers:
“Sasa ndugu zangu, nafahamu kwamba ninyi na wakuu wenu mlitenda hayo kwa sababu ya kutojua kwenu.
18 but thus hath God accomplished those things which He had foretold by the mouth of all his prophets, that Christ should suffer.
Lakini ndivyo Mungu alivyotimiza yale aliyotangaza zamani kwa njia ya manabii wote, kwamba ilikuwa lazima Kristo wake ateseke.
19 Repent therefore and be converted, that your sins may be blotted out: that seasons of refreshing may come upon you from the presence of the Lord;
Basi, tubuni mkamrudie Mungu ili afute dhambi zenu.
20 and He may send Jesus Christ, who was before preached unto you:
Fanyeni hivyo ili Bwana awape nyakati za kuburudika rohoni na kuwaletea yule Kristo aliyemteua ambaye ndiye Yesu.
21 whom heaven must indeed receive till the times of settling all things, of which God hath spoken by the mouth of all his holy prophets from the beginning. (aiōn g165)
Ni lazima yeye abaki huko mbinguni mpaka utakapofika wakati wa kurekebishwa vitu vyote, kama Mungu alivyosema kwa njia ya manabii wake watakatifu wa tangu zamani. (aiōn g165)
22 For Moses said unto the fathers, the Lord your God will raise up a prophet unto you, of your brethren, like me, Him shall ye hear in all things whatever He shall say unto you;
Kwa maana Mose alisema, Bwana Mungu wenu atawapelekeeni nabii kama mimi kutoka kati yenu ninyi wenyewe.
23 and every soul, who will not hearken to that prophet, shall be destroyed from among the people: yea and all the prophets from Samuel,
Yeyote yule ambaye hatamsikiliza nabii huyo atatengwa mbali na watu wa Mungu na kuangamizwa.
24 and those that followed, as many as have prophesied, have also foretold these days.
Manabii wote, kuanzia Samweli na wale waliomfuata, walitangaza habari za mambo haya ambayo yamekuwa yakitendeka siku hizi.
25 Now ye are the children of the prophets, and of the covenant, which God made with our fathers, saying to Abraham, "And in thy seed shall all the families of the earth be blessed:"
Ahadi zile Mungu alizotoa kwa njia ya manabii ni kwa ajili yenu; na mnashiriki lile agano Mungu alilofanya na babu zenu, kama alivyomwambia Abrahamu: Kwa njia ya wazawa wako, jamaa zote za dunia zitabarikiwa.
26 and to you first God having raised up his son Jesus, sent Him to bless you; in your turning away every one of you from your iniquities.
Basi, ilikuwa kwa ajili yenu kwanza kwamba Mungu alimfufua mtumishi wake, alimtuma awabariki kwa kumfanya kila mmoja wenu aachane kabisa na maovu yake.”

< Acts 3 >