< 1 Peter 1 >

1 Peter an apostle of Jesus Christ to the strangers who are dispersed through Pontus, Galatia, Cappadocia,
Mimi Petro, mtume wa Yesu Kristo nawaandikia ninyi wateule wa Mungu Baba, ambao mmetawanyika na mnaishi kama wakimbizi huko Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithunia.
2 Asia, and Bithynia, chosen according to the fore-knowledge of God, through sanctification of the Spirit, unto obedience, and to the sprinkling of the blood of Jesus Christ, ---may grace and peace be multiplied unto you.
Mungu Baba aliwateua ninyi kufuatana na kusudi lake, na mmefanywa watakatifu na Roho, mpate kumtii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Nawatakieni neema na amani tele.
3 Blessed be the God and Father of our Lord Jesus Christ, who according to his abundant mercy hath regenerated us to a lively hope, by the resurrection of Jesus Christ from the dead,
Asifiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kuu alitufanya tuzaliwe upya kwa kumfufua Yesu kutoka wafu. Ametujalia tumaini lenye uzima,
4 to an inheritance incorruptible, undefiled, and unfading, reserved in heaven for you,
na hivyo tunatazamia kupata baraka zile ambazo Mungu aliwawekea watu wake. Mungu amewawekeeni baraka hizo mbinguni ambako haziwezi kuoza au kuharibika au kufifia.
5 who are kept by the power of God through faith unto salvation ready to be revealed in the last time.
Hizo zitakuwa zenu ninyi ambao kwa imani mnalindwa salama kwa nguvu ya Mungu kwa ajili ya wokovu ambao uko tayari kufunuliwa mwishoni mwa nyakati.
6 In which ye rejoice, tho' now for a little while, if need be, ye are grieved through various trials.
Furahini kuhusu jambo hilo, ijapokuwa sasa, kwa kitambo kidogo, itawabidi kuhuzunika kwa sababu ya majaribio mbalimbali mnayoteseka.
7 That the proof of your faith, which is much more precious than of gold, (that perisheth, though tried by fire) may be found unto praise, and honor, and glory, when Jesus Christ shall be revealed:
Shabaha yake ni kuthibitisha imani yenu. Hata dhahabu yenyewe ambayo huharibika, hujaribiwa kwa moto; hali kadhalika na imani yenu ambayo ni ya thamani zaidi kuliko dhahabu, ni lazima ijaribiwe ipate kuwa thabiti. Hapo mtapokea sifa na utukufu na heshima Siku ile Yesu Kristo atakapofunuliwa.
8 whom having not seen ye love; in whom, though now ye see Him not, yet believing ye rejoice with joy ineffable and full of glory; receiving the end of your faith,
Ninyi mnampenda ingawaje hamjamwona, na mnamwamini ingawa hamumwoni sasa. Hivyo, mnafurahi kwa furaha tukufu isiyoelezeka,
9 even the salvation of your souls:
kwa sababu mnapokea wokovu wa roho zenu ambao ni lengo la imani yenu.
10 concerning which salvation the prophets, who prophesied of the grace to be conferred on you, enquired and diligently sought after it:
Manabii walipeleleza kwa makini na kufanya uchunguzi juu ya wokovu huo, wakabashiri juu ya neema hiyo ambayo ninyi mngepewa.
11 searching what, or what manner of time the Spirit of Christ in them did declare in testifying beforehand the sufferings that were to come upon Christ, and the glories following them:
Walijaribu kujua nyakati na mazingira ya tukio hilo, yaani wakati alioudokezea Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao, akibashiri juu ya mateso yatakayompata Kristo na utukufu utakaofuata.
12 to whom it was revealed, that it was not to themselves, but to us they ministered these things, which are now declared unto you by them that have preached the gospel unto you, through the holy Spirit sent down from heaven; which things the angels desire to look into.
Mungu aliwafunulia kwamba wakati walipokuwa wanasema juu ya hayo mambo ambayo ninyi mmekwisha sikia sasa kutoka kwa wale wajumbe waliowatangazieni Habari Njema kwa nguvu ya Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni, hiyo kazi yao haikuwa kwa faida yao wenyewe, bali kwa ajili yenu. Hayo ndiyo mambo ambayo hata malaika wangependa kuyafahamu.
13 Wherefore girding up the loins of your mind, be sober, and stedfastly hope for the grace to be conferred upon you at the appearing of Jesus Christ;
Kwa hiyo, basi, muwe tayari kabisa kwa nia, na kukesha. Wekeni tumaini lenu lote katika baraka ile mtakayopewa wakati Yesu Kristo atakapoonekana!
14 as children of obedience, not conforming yourselves to the former lusts in your ignorance:
Kama watoto wa Mungu wenye utii, msikubali kamwe kufuata tena tamaa mbaya mlizokuwa nazo wakati mlipokuwa wajinga.
15 but as He who hath called you is holy, be ye also holy in all your conversation: since it is written,
Bali mnapaswa kuwa watakatifu katika mwenendo wenu wote, kama vile yule aliyewaiteni ni mtakatifu.
16 Be ye holy, for I am holy.
Maandiko yasema: “Muwe watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”
17 And if ye call upon the Father, who without respect of persons judgeth according to every man's work, pass the time of your sojourning here in fear:
Mnapomtaja Mungu ninyi humwita Baba. Basi, jueni kwamba yeye humhukumu kila mmoja kadiri ya matendo yake, bila ubaguzi. Hivyo tumieni wakati wenu uliowabakia hapa ugenini katika kumcha Mungu.
18 knowing that ye were redeemed from your vain conversation learned by tradition from your fathers, not with corruptible things, as silver and gold;
Maana mnajua kwamba ninyi mlikombolewa katika mwenendo wenu usiofaa ambao mliupokea kutoka kwa wazee wenu, si kwa vitu vyenye kuharibika: kwa fedha na dhahabu;
19 but with the precious blood of Christ as of a lamb without blemish and without spot:
bali mlikombolewa kwa damu tukufu ya Kristo, ambaye alikuwa kama mwana kondoo asiye na dosari wala doa.
20 who was indeed appointed before the foundation of the world, but manifested in these last times, for your sakes,
Yeye alikuwa ameteuliwa na Mungu kabla ya ulimwengu kuumbwa, akafunuliwa siku hizi za mwisho kwa ajili yenu.
21 who through Him trust in God that raised Him from the dead, and gave Him glory, that your faith and hope might be fixed in God.
Kwa njia yake, ninyi mnamwamini Mungu aliyemfufua kutoka wafu na kumpa utukufu; na hivyo imani na matumaini yenu yako kwa Mungu.
22 Having therefore purified your souls by obedience to the truth, through the Spirit, to brotherly love unfeigned, love one another with a pure heart fervently:
Maadamu sasa, kwa kuutii ukweli, ninyi mmezitakasa roho zenu na kuwapenda wenzenu bila unafiki, basi, pendaneni kwa moyo wote.
23 being regenerated not of corruptible seed, but of incorruptible, by the word of God which liveth and abideth for ever. (aiōn g165)
Maana kwa njia ya neno hai la Mungu, ninyi mmezaliwa upya, si kama watoto wa baba awezaye kufa, bali baba asiyekufa milele. (aiōn g165)
24 For all flesh is as grass, and all the glory of man as the flower of grass: the grass withereth, and the flower thereof falleth away;
Kama Maandiko yasemavyo: “Kila binadamu ni kama nyasi, na utukufu wake wote ni kama maua ya porini. Nyasi hunyauka na maua huanguka.
25 but the word of the Lord abideth for ever. And this is the word which is preached to you in the gospel. (aiōn g165)
Lakini neno la Bwana hudumu milele.” Neno hilo ni hiyo Habari Njema iliyohubiriwa kwenu. (aiōn g165)

< 1 Peter 1 >