< Exodus 26 >
1 “Moreover you shall make the tabernacle with ten curtains of fine twined linen, and blue, and purple, and scarlet, with cherubim. You shall make them with the work of a skillful workman.
“Tengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi atatarizi makerubi kwenye mapazia hayo.
2 The length of each curtain shall be twenty-eight cubits, and the width of each curtain four cubits: all the curtains shall have one measure.
Mapazia yote yatatoshana kwa ukubwa: kila moja litakuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
3 Five curtains shall be coupled together to one another, and the other five curtains shall be coupled to one another.
Unganisha mapazia matano pamoja; fanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
4 You shall make loops of blue on the edge of the one curtain from the edge in the coupling, and you shall do likewise on the edge of the curtain that is outermost in the second coupling.
Tengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, na ufanye vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
5 You shall make fifty loops in the one curtain, and you shall make fifty loops in the edge of the curtain that is in the second coupling. The loops shall be opposite one another.
Fanya vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vielekeane.
6 You shall make fifty clasps of gold, and couple the curtains to one another with the clasps. The tabernacle shall be a unit.
Kisha tengeneza vifungo hamsini vya dhahabu ili vitumike kufunga na kuunganisha mapazia pamoja kufanya Hema liwe kitu kimoja.
7 “You shall make curtains of goats’ hair for a covering over the tabernacle. You shall make eleven curtains.
“Tengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
8 The length of each curtain shall be thirty cubits, and the width of each curtain four cubits: the eleven curtains shall have one measure.
Mapazia hayo kumi na moja yatakuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
9 You shall couple five curtains by themselves, and six curtains by themselves, and shall double over the sixth curtain in the forefront of the tent.
Unganisha hayo mapazia matano yawe fungu moja, na hayo mengine sita yawe fungu lingine. Kunja hilo pazia la sita mara mbili mbele ya maskani.
10 You shall make fifty loops on the edge of the one curtain that is outermost in the coupling, and fifty loops on the edge of the curtain which is outermost in the second coupling.
Tengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
11 You shall make fifty clasps of bronze, and put the clasps into the loops, and couple the tent together, that it may be one.
Kisha tengeneza vifungo hamsini vya shaba, uviingize katika vile vitanzi ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
12 The overhanging part that remains of the curtains of the tent—the half curtain that remains—shall hang over the back of the tabernacle.
Kuhusu kile kipande cha ziada cha pazia la Hema, nusu ya hilo pazia lililobaki litaningʼinizwa upande wa nyuma wa Hema.
13 The cubit on the one side and the cubit on the other side, of that which remains in the length of the curtains of the tent, shall hang over the sides of the tabernacle on this side and on that side, to cover it.
Mapazia ya hema yatakuwa na urefu wa dhiraa moja zaidi pande zote, sehemu itakayobaki itaningʼinia pande zote za Hema ili kuifunika.
14 You shall make a covering for the tent of rams’ skins dyed red, and a covering of sea cow hides above.
Tengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
15 “You shall make the boards for the tabernacle of acacia wood, standing upright.
“Tengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
16 Ten cubits shall be the length of a board, and one and a half cubits the width of each board.
Kila mhimili uwe na urefu wa dhiraa kumi na upana wa dhiraa moja na nusu,
17 There shall be two tenons in each board, joined to one another: thus you shall make for all the boards of the tabernacle.
zikiwa na ndimi mbili zilizo sambamba kila mmoja na mwingine. Tengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
18 You shall make twenty boards for the tabernacle, for the south side southward.
Tengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
19 You shall make forty sockets of silver under the twenty boards; two sockets under one board for its two tenons, and two sockets under another board for its two tenons.
kisha tengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
20 For the second side of the tabernacle, on the north side, twenty boards,
Kuhusu upande wa kaskazini wa maskani, tengeneza mihimili ishirini
21 and their forty sockets of silver; two sockets under one board, and two sockets under another board.
na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
22 For the far side of the tabernacle westward you shall make six boards.
Kisha tengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
23 You shall make two boards for the corners of the tabernacle in the far side.
na pia utengeneze mihimili miwili ya pembe za upande ulio mbali.
24 They shall be double beneath, and in the same way they shall be whole to its top to one ring: thus shall it be for them both; they shall be for the two corners.
Katika pembe hizi mbili ni lazima mihimili yake iwe miwili kuanzia chini mpaka juu, na iingizwe kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili itafanana.
25 There shall be eight boards, and their sockets of silver, sixteen sockets; two sockets under one board, and two sockets under another board.
Kwa hiyo itakuwepo mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
26 “You shall make bars of acacia wood: five for the boards of the one side of the tabernacle,
“Pia tengeneza mataruma ya mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
27 and five bars for the boards of the other side of the tabernacle, and five bars for the boards of the side of the tabernacle, for the far side westward.
matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili ya mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
28 The middle bar in the middle of the boards shall pass through from end to end.
Taruma la katikati litapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
29 You shall overlay the boards with gold, and make their rings of gold for places for the bars. You shall overlay the bars with gold.
Funika hiyo mihimili kwa dhahabu, kisha tengeneza pete za dhahabu ambazo zitashikilia hayo mataruma. Pia funika hayo mataruma kwa dhahabu.
30 You shall set up the tabernacle according to the way that it was shown to you on the mountain.
“Simamisha Hema sawasawa na mfano ulioonyeshwa kule mlimani.
31 “You shall make a veil of blue, and purple, and scarlet, and fine twined linen, with cherubim. It shall be the work of a skillful workman.
“Tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi atirizi makerubi kwenye hilo pazia.
32 You shall hang it on four pillars of acacia overlaid with gold; their hooks shall be of gold, on four sockets of silver.
Litundike kwa kulabu za dhahabu kwenye nguzo nne za mti wa mshita ambazo zimefunikwa kwa dhahabu, zikiwa zimesimamishwa kwenye vitako vinne vya fedha.
33 You shall hang up the veil under the clasps, and shall bring the ark of the covenant in there within the veil. The veil shall separate the holy place from the most holy for you.
Ningʼiniza pazia hilo kwenye vifungo, kisha weka Sanduku la Ushuhuda nyuma ya pazia. Pazia litatenganisha Mahali Patakatifu kutoka Patakatifu pa Patakatifu.
34 You shall put the mercy seat on the ark of the covenant in the most holy place.
Weka kifuniko cha kiti cha rehema juu ya Sanduku la Ushuhuda ndani ya Patakatifu pa Patakatifu.
35 You shall set the table outside the veil, and the lamp stand opposite the table on the side of the tabernacle toward the south. You shall put the table on the north side.
Weka meza nje ya pazia upande wa kaskazini wa Hema, kisha weka kinara cha taa upande wa kusini wa Hema.
36 “You shall make a screen for the door of the Tent, of blue, and purple, and scarlet, and fine twined linen, the work of the embroiderer.
“Kwa ajili ya ingilio la hema, tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
37 You shall make for the screen five pillars of acacia, and overlay them with gold. Their hooks shall be of gold. You shall cast five sockets of bronze for them.
Tengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya hilo pazia, na nguzo tano za mshita zilizofunikwa kwa dhahabu. Kisha mimina vitako vitano vya shaba kwa ajili yake.