< Judges 12 >

1 And the men of Ephraim assembled, and went northward, and said to Jephthah, Why didst thou pass over to fight against the children of Ammon, and didst not call us to go with thee; we will burn thy house upon thee with fire.
Watu wa Efraimu wakaita majeshi yao, wakavuka kwenda Zafoni, wakamwambia Yefta, “Kwa nini mmekwenda kupigana na Waamoni bila kutuita ili twende pamoja nawe? Basi tutaichoma moto nyumba yako, pamoja nawe ukiwa ndani yake.”
2 And Jephthah said to them, I and my people were at great strife with the children of Ammon; and when I called you, ye delivered me not out of their hands.
Yefta akajibu, “Mimi na watu wangu tulikuwa na ugomvi mkubwa na Waamoni, hata ingawa niliwaita hamkuniokoa katika mkono wao.
3 And when I saw that ye delivered [me] not, I put my life in my hands, and passed over against the children of Ammon, and the LORD delivered them into my hand: why then have ye come up to me this day, to fight against me?
Nilipoona kuwa hamkunipa msaada nikauhatarisha uhai wangu na nikavuka kupigana na Waamoni. Naye Bwana akanipatia ushindi dhidi yao. Sasa kwa nini mnanijia leo ili kupigana nami?”
4 Then Jephthah collected all the men of Gilead, and fought with Ephraim: and the men of Gilead smote Ephraim, because they said, Ye Gileadites [are] fugitives of Ephraim among the Ephraimites, [and] among the Manassites.
Ndipo Yefta akakusanya watu wa Gileadi pamoja na kupigana na Efraimu. Wagileadi wakawashinda Efraimu, kwa kuwa Waefraimu walisema, “Ninyi Wagileadi ni watoro mliotoroka toka Efraimu na Manase.”
5 And the Gileadites took the passages of Jordan before the Ephraimites: and it was [so], that when those Ephraimites who had escaped, said, Let me go over; that the men of Gilead said to him, [Art] thou an Ephraimite? If he said, No;
Wagileadi wakaviteka vivuko vya Yordani dhidi ya hao Waefraimu, kisha ilikuwa yeyote yule aliyenusurika katika Efraimu aliposema, “Niache nivuke,” hao watu wa Gileadi walimuuliza, “Je wewe ni Mwefraimu?” Kama alijibu “Hapana,”
6 Then said they to him, Say now Shibboleth: and he said Sibboleth: for he could not frame to pronounce [it] right. Then they took him, and slew him at the passages of Jordan. And there fell at that time of the Ephraimites forty and two thousand.
walimwambia, “Sawa, sema ‘Shibolethi.’” Iwapo alitamka, “Sibolethi,” kwa sababu hakuweza kutamka hilo neno sawasawa, walimkamata na kumuua hapo kwenye vivuko vya Yordani. Waefraimu 42,000 waliuawa wakati huo.
7 And Jephthah judged Israel six years: then died Jephthah the Gileadite, and was buried in [one of] the cities of Gilead.
Yefta akawa mwamuzi wa Waisraeli kwa muda wa miaka sita. Basi Yefta akafa, akazikwa katika mmojawapo wa miji ya Gileadi.
8 And after him Ibzan of Beth-lehem judged Israel.
Baada yake, Ibzani wa Bethlehemu akawa mwamuzi wa Israeli.
9 And he had thirty sons and thirty daughters [whom] he sent abroad, and took in thirty daughters from abroad for his sons: and he judged Israel seven years.
Alikuwa na wana thelathini na binti thelathini. Akawaoza binti zake kwa watu wengine nje ya ukoo wake, na kuwatwalia wanawe wanawake thelathini toka nje ya ukoo wake. Ibzani akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka saba.
10 Then died Ibzan, and was buried at Beth-lehem.
Ibzani akafa, akazikwa huko Bethlehemu.
11 And after him Elon, a Zebulonite, judged Israel, and he judged Israel ten years.
Baada yake Eloni, Mzabuloni, akawa mwamuzi wa Israeli, naye akawaamua kwa muda wa miaka kumi.
12 And Elon the Zebulonite died, and was buried in Ajalon in the country of Zebulun.
Kisha Eloni akafa, akazikwa katika Aiyaloni, katika nchi ya Zabuloni.
13 And after him Abdon the son of Hillel, a Pirathonite, judged Israel.
Baada yake, Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akawa mwamuzi wa Israeli.
14 And he had forty sons and thirty nephews, that rode on seventy ass colts: and he judged Israel eight years.
Naye akazaa wana arobaini na wana wa wanawe thelathini waliopanda punda sabini. Akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka minane.
15 And Abdon the son of Hillel the Pirathonite died, and was buried in Pirathon in the land of Ephraim, in the mount of the Amalekites.
Ndipo Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akafa, naye akazikwa huko Pirathoni katika Efraimu, katika nchi ya vilima ya Waamaleki.

< Judges 12 >