< Hosea 6 >

1 Come, and let us return to the LORD: for he hath torn, and he will heal us; he hath smitten, and he will bind us up.
“Njooni, tumrudie Bwana. Ameturarua vipande vipande lakini atatuponya; ametujeruhi lakini atatufunga majeraha yetu.
2 After two days will he revive us: in the third day will he raise us up, and we shall live in his sight.
Baada ya siku mbili atatufufua; katika siku ya tatu atatuinua, ili tuweze kuishi mbele zake.
3 Then shall we know, [if] we follow on to know the LORD: his going forth is prepared as the morning; and he will come to us as the rain, as the latter [and] former rain to the earth.
Tumkubali Bwana, tukaze kumkubali yeye. Kutokea kwake ni hakika kama vile kuchomoza kwa jua; atatujia kama mvua za masika, kama vile mvua za vuli ziinyweshavyo nchi.”
4 O Ephraim, what shall I do to thee? O Judah, what shall I do to thee? for your goodness [is] as the morning cloud, and as the early dew it goeth away.
“Nifanye nini nawe, Efraimu? Nifanye nini nawe, Yuda? Upendo wako ni kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao.
5 Therefore have I hewed [them] by the prophets; I have slain them by the words of my mouth: and thy judgments [are as] the light [that] goeth forth.
Kwa hiyo ninawakata ninyi vipande vipande kwa kutumia manabii wangu; nimewaua ninyi kwa maneno ya kinywa changu, hukumu zangu zinawaka kama umeme juu yenu.
6 For I desired mercy, and not sacrifice: and the knowledge of God more than burnt-offerings.
Kwa maana nataka rehema, wala si dhabihu, kumkubali Mungu zaidi kuliko sadaka za kuteketezwa.
7 But they like men have transgressed the covenant: there have they dealt treacherously against me.
Wamevunja Agano kama Adamu: huko hawakuwa waaminifu kwangu.
8 Gilead [is] a city of them that work iniquity, [and is] polluted with blood.
Gileadi ni mji wenye watu waovu, umetiwa madoa kwa nyayo za damu.
9 And as troops of robbers wait for a man, [so] the company of priests murder in the way by consent: for they commit lewdness.
Kama wanyangʼanyi wamviziavyo mtu, ndivyo magenge ya makuhani wafanyavyo; wanaulia watu kwenye njia iendayo Shekemu, wakifanya uhalifu wa aibu.
10 I have seen a horrible thing in the house of Israel: there [is] the prostitution of Ephraim, Israel is defiled.
Nimeona jambo la kutisha katika nyumba ya Israeli. Huko Efraimu amejitolea kwa ukahaba na Israeli amenajisika.
11 Also, O Judah, he hath set a harvest for thee, when I returned the captivity of my people.
“Pia kwa ajili yako, Yuda, mavuno yameamriwa. “Wakati wowote ningerejesha neema ya watu wangu,

< Hosea 6 >