< 2 Chronicles 17 >

1 And Jehoshaphat his son reigned in his stead, and strengthened himself against Israel.
Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake na akajiimarisha dhidi ya Israeli.
2 And he placed forces in all the fortified cities of Judah, and set garrisons in the land of Judah, and in the cities of Ephraim, which Asa his father had taken.
Akaweka jeshi katika miji yote ya Yuda yenye ngome na kuweka askari walinzi katika Yuda na katika miji ya Efraimu ile ambayo baba yake Asa alikuwa ameiteka.
3 And the LORD was with Jehoshaphat, because he walked in the first ways of his father David, and sought not to Baalim;
Bwana Mungu alikuwa na Yehoshafati kwa sababu katika miaka yake ya mwanzoni alienenda katika njia za Daudi baba yake. Hakutafuta Mabaali
4 But sought to the [LORD] God of his father, and walked in his commandments, and not after the doings of Israel.
bali alimtafuta Mungu wa baba yake na kuzifuata amri zake badala ya kufuata desturi za watu wa Israeli.
5 Therefore the LORD established the kingdom in his hand: and all Judah brought to Jehoshaphat presents; and he had riches and honor in abundance.
Kwa hiyo Bwana akauimarisha ufalme chini ya uongozi wake, nao Yuda wote wakamletea Yehoshafati zawadi, hivyo akawa na utajiri mwingi na heshima.
6 And his heart was lifted up in the ways of the LORD: moreover he took away the high places and groves out of Judah.
Moyo wake ukawa hodari katika njia za Bwana na zaidi ya yote, akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na nguzo za Maashera katika Yuda.
7 Also in the third year of his reign he sent to his princes, [even] to Ben-hail, and to Obadiah, and to Zechariah, and to Nethaneel, and to Michaiah, to teach in the cities of Judah.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa akatuma maafisa wake ambao ni: Ben-Haili, Obadia, Zekaria, Nethaneli na Mikaya ili kufundisha katika miji ya Yuda.
8 And with them [he sent] Levites, [even] Shemaiah, and Nethaniah, and Zebadiah, and Asahel, and Shemiramoth, and Jehonathan, and Adonijah, and Tobijah, and Tob-adonijah, Levites; and with them Elishama and Jehoram, priests.
Pamoja nao walikuwepo Walawi fulani nao ni: Shemaya, Nethania, Zebadia, Asaheli, Shemiramothi, Yehonathani, Adoniya, Tobia, Tob-Adonia, pamoja nao walikuwepo makuhani Elishama na Yehoramu.
9 And they taught in Judah, and [had] the book of the law of the LORD with them, and went about throughout all the cities of Judah, and taught the people.
Wakafundisha Yuda yote, wakiwa wamechukua Kitabu cha Sheria ya Bwana wakazunguka miji yote ya Yuda na kufundisha watu.
10 And the fear of the LORD fell upon all the kingdoms of the lands that [were] around Judah, so that they made no war against Jehoshaphat.
Hofu ya Bwana ikawa juu ya falme zote za nchi zilizozunguka Yuda, hivyo hawakufanya vita na Yehoshafati.
11 Also [some] of the Philistines brought Jehoshaphat presents, and tribute silver; and the Arabians brought him flocks, seven thousand and seven hundred rams, and seven thousand and seven hundred he-goats.
Baadhi ya Wafilisti wakamletea Yehoshafati zawadi na fedha kama ushuru, nao Waarabu wakamletea mifugo: kondoo dume 7,700 na mbuzi 7,700.
12 And Jehoshaphat became exceedingly great; and he built in Judah castles, and cities of store.
Yehoshafati akaendelea kupata nguvu zaidi na zaidi, akajenga ngome na miji ya hazina katika Yuda
13 And he had much business in the cities of Judah: and the men of war, mighty men of valor, [were] in Jerusalem.
na akawa na wingi mkubwa wa vitu katika miji ya Yuda. Pia aliweka askari wa vita wenye uzoefu huko Yerusalemu.
14 And these [are] the numbers of them according to the house of their fathers: of Judah, the captains of thousands; Adnah the chief, and with him mighty men of valor three hundred thousand.
Wakaandikishwa katika jamaa zao kama ifuatavyo: Kutoka Yuda, majemadari wa vikosi vya elfu: Jemadari Adna akiwa na askari wa vita 300,000;
15 And next to him [was] Jehohanan the captain, and with him two hundred and eighty thousand.
aliyefuata ni jemadari Yehohanani, akiwa na askari 280,000 walio tayari kwa vita;
16 And next to him [was] Amasiah the son of Zichri, who willingly offered himself to the LORD; and with him two hundred thousand mighty men of valor.
aliyefuata ni Amasia mwana wa Zikri, ambaye alijitolea kwa ajili ya kazi ya Bwana, akiwa na askari 200,000.
17 And of Benjamin; Eliada a mighty man of valor, and with him armed men with bow and shield two hundred thousand.
Kutoka Benyamini: Eliada, askari shujaa akiwa na watu 200,000 wenye silaha za nyuta na ngao;
18 And next to him [was] Jehozabad, and with him a hundred and eighty thousand ready prepared for the war.
aliyefuata ni Yehozabadi, akiwa na askari 180,000 wenye silaha za vita.
19 These waited on the king, besides [those] whom the king put in the fortified cities throughout all Judah.
Hawa ndio waliomtumikia mfalme, mbali na wale mfalme aliweka katika miji yenye ngome huko Yuda yote.

< 2 Chronicles 17 >