< Romans 13 >

1 Every [believer] must be subject to the authorities. [Remember that] God is the only one [who gives officials their] authority. Furthermore, those officials that exist are ones who have been appointed by God {God has appointed}.
Kila mtu anapaswa kuwatii wenye mamlaka katika serikali; maana mamlaka yote hutoka kwa Mungu; nao wenye mamlaka wamewekwa na Mungu.
2 So whoever resists the officials is resisting what God has established. Furthermore, those who resist officials will bring on themselves [from the officials] the punishment [that God considers fitting].
Anayepinga mamlaka ya viongozi anapinga agizo la Mungu; nao wafanyao hivyo wanajiletea hukumu wenyewe,
3 What rulers [do] is not [to cause people who] do good deeds to be afraid. Instead, [what they do is to cause people who do] evil to be afraid. So, if any of you [RHQ] wants to be unafraid of officials, do what is good! [If you(sg) do good], they will commend you [instead of punishing you!]
Maana, watawala hawasababishi hofu kwa watu wema, ila kwa watu wabaya. Basi, wataka usimwogope mtu mwenye mamlaka? Fanya mema naye atakusifu;
4 It is in order to serve God [by doing their work that every official exists], in order that they may benefit each of you. If any of you does what is evil, you [(sg) will rightfully have reason to] be afraid, because the authority that they have to punish people [MTY] is very real [LIT]! The officials exist to serve God. That is, they act as God’s agents as they punish those who do evil.
maana yeye ni mtumishi wa Mungu anayefanya kazi kwa faida yako. Lakini ukifanya mabaya, basi, huna budi kumwogopa, maana anao kweli uwezo wa kutoa adhabu. Yeye ni mtumishi wa Mungu na huitekeleza ghadhabu ya Mungu kwao watendao maovu.
5 So, it is necessary for you [(pl)] to be subject [to officials], not only because they will punish you [MTY] [if you disobey them], but also because you know [that you should be subject to them]
Kwa hiyo ni lazima kuwatii wenye mamlaka, si tu kwa sababu ya kuogopa ghadhabu ya Mungu, bali pia kwa sababu dhamiri inadai hivyo.
6 It is for this reason that you also pay taxes, because the officials are ones who serve God as they continually do their work.
Kwa sababu hiyohiyo ninyi hulipa kodi; maana viongozi hao humtumikia Mungu ikiwa wanatimiza wajibu wao.
7 Give to all [the officials] what you are supposed to give to them! Pay taxes to [those who require that you pay taxes]. Pay duties [on goods to those who require that you pay those] duties. Respect [those who ought to] be respected. Honor [those who ought to] be honored.
Mpeni kila mtu haki yake; mtu wa ushuru, ushuru; wa kodi, kodi; na astahiliye heshima, heshima.
8 Pay all of your debts [when you are supposed to pay them]. The only thing [that is like] a debt that [you] should never stop paying is to love one another. Whoever loves others has fulfilled all that [God requires in] his laws.
Msiwe na deni kwa mtu yeyote, isipokuwa tu deni la kupendana. Ampendaye jirani yake ameitekeleza Sheria.
9 [There are many things that God] commanded [in his laws, such as] do not commit adultery, do not murder [anyone], do not steal, and do not desire anything that belongs to someone else. But the command by which they are all summed up {that includes them all} is this: Each of you must love the people with whom you come in contact, just like you [(sg)] love yourself.
Maana, amri hizi: “Usizini; Usiue; Usitamani;” na nyingine zote, zimo katika amri hii moja: “Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
10 If you love people with whom you come in contact [PRS], you will not do any evil to them [LIT]. So, whoever loves [others] fulfills all that [God’s] laws [require].
Ampendaye jirani yake hamtendei vibaya. Basi, kwa mapendo Sheria yote hutimizwa.
11 [Do] what I have just told you, especially since you know [the significance of] the time [in which we are living. You know that it is] time for you to be [fully alert and active] [MET], [like people who have] awakened from sleeping [MET], because [the time when Christ will finally] deliver us [from this world’s pain/sin and sorrow] is near. That time (is closer than/was not so close) when we first believed [in Christ].
Zaidi ya hayo, ninyi mnajua tumo katika wakati gani: sasa ndio wakati wa kuamka usingizini; naam, wokovu wetu u karibu zaidi sasa kuliko wakati ule tulipoanza kuamini.
12 [Our time to live in this world] [MTY] [is almost ended] [MET], [like] a night that is nearly ended. The time [when Christ will return] [MTY] is near. So we must quit doing wicked deeds [MET] [such as people do] in the darkness, and [we must be doing the things that will help us resist Satan/evil] [MET], [as soldiers who] put on their armor in the daytime [get ready to resist their enemies].
Usiku unakwisha na mchana unakaribia. Basi, tutupilie mbali mambo yote ya giza, tukajitwalie silaha za mwanga.
13 We must behave properly, as though the time [when Christ will return] [MTY] [were already here]. We must not participate in drunken carousing [HEN]. We must not commit any kind of sexual immorality [MTY, DOU]. We must not quarrel. We must not be jealous [of other people].
Mwenendo wetu uwe wa adabu kama inavyostahili wakati wa mchana; tusiwe na ulafi na ulevi, uchafu na uasherati, ugomvi na wivu.
14 On the contrary, you/we should [be like] the Lord Jesus Christ [so that others will see that we belong to him], just as [people] put on [special clothes so that others will see what group they belong to] [MET]. You/We should stop thinking about [doing the things that your/our] self-directed nature desires.
Bwana Yesu Kristo awe vazi lenu; msishughulikie tena tamaa zenu za maumbile na kuziridhisha.

< Romans 13 >