< 2 Kings 2 >

1 When Yahweh was about to take [the prophet] Elijah up to heaven in a (whirlwind/twisting wind), Elijah and [his fellow prophet] Elisha were traveling [south] from Gilgal [town].
Wakati Bwana alipokuwa karibu kumchukua Eliya mbinguni kwa upepo wa kisulisuli, Eliya na Elisha walikuwa njiani wakitoka Gilgali.
2 Elijah said to Elisha, “Stay here, because Yahweh has told [only] me to go to Bethel [town].” But Elisha replied, “Just as certainly as Yahweh lives and you live, I will not leave you!” So they went down [together] to Bethel.
Eliya akamwambia Elisha, “Kaa hapa. Bwana amenituma Betheli.” Lakini Elisha akasema, “Kwa hakika, kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Kwa hiyo wakaenda Betheli pamoja.
3 A group of prophets came to Elisha [and Elijah before they entered the town], and they asked Elisha, “Do you know that Yahweh is going to take your master/boss [Elijah] away from you today?” Elisha answered, “Certainly I know that, but don’t talk about it!” [IDM]
Wana wa manabii waliokuwako huko Betheli wakamjia Elisha na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?” Elisha akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.”
4 Then Elijah said to Elisha, “Stay here, because Yahweh has told [only] me to go to Jericho.” But Elisha replied [again], “Just as certainly as Yahweh lives and you live, I will not leave you!” So they went [together] to Jericho [city].
Kisha Eliya akamwambia, “Baki hapa, Elisha. Bwana amenituma Yeriko.” Naye akajibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wakaenda Yeriko.
5 [As they neared] Jericho, a group of prophets who were from there came to Elisha and said to him, “Do you know that Yahweh is going to take your master/boss [Elijah] away from you today?” He answered again, “Certainly I know that, but don’t talk about it!” [IDM]
Wana wa manabii waliokuwako huko Yeriko wakamwendea Elisha na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?” Akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.”
6 Then Elijah said to Elisha, “Stay here, because Yahweh has told [only] me to go to the Jordan [River].” But [again] Elisha replied, “As certainly as Yahweh lives and you live, I will not leave you!” So they continued walking together.
Kisha Eliya akamwambia, “Kaa hapa. Bwana amenituma kwenda Yordani.” Naye akamjibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wote wawili wakaendelea pamoja.
7 Fifty men from a group of prophets [who were from Jericho] also went, but they watched from a distance as Elijah and Elisha stopped at the edge of the Jordan [River].
Wana hamsini wa manabii wakaenda na kusimama kwa mbali, kuelekea mahali ambapo Eliya na Elisha walikuwa wamesimama kando ya Mto Yordani.
8 Then Elijah rolled up his cloak and struck the water with it. A path opened up for them through the river, and they walked across [as though they were] on dry ground.
Eliya akachukua vazi lake, akalisokota na kupiga nalo maji. Maji yakagawanyika upande wa kuume na upande wa kushoto, nao wawili wakavuka pakavu.
9 When they came to the other side, Elijah said to Elisha, “What do you want me to do for you before (I am taken away/Yahweh takes me away)?” Elisha replied, “I want to receive twice as much of your power [as you have had, ] (OR enable me to very powerfully continue your ministry).”
Walipokwisha kuvuka, Eliya akamwambia Elisha, “Niambie, nikufanyie nini kabla sijaondolewa kutoka kwako?” Elisha akajibu, “Naomba nirithi sehemu maradufu ya roho yako.”
10 Elijah replied, “You have asked for something which is difficult [for me to cause to happen]. But, if you see me when (I am taken from you/Yahweh takes me from you), you will get what you are requesting. But if you do not see me, then you will not get it.”
Eliya akasema, “Umeomba jambo gumu. Lakini kama utaniona wakati ninapoondolewa kutoka kwako litakuwa lako. La sivyo, hautalipata.”
11 As they were walking and talking, suddenly a chariot that had fire [surrounding it], pulled by horses which also had fire [surrounding them], appeared. [The chariot driver] drove the chariot between Elijah and Elisha and separated them. Then Elijah was taken up to heaven in a (whirlwind/twisting wind).
Walipokuwa wakitembea pamoja na kuzungumza, ghafula gari la moto na farasi wa moto vilitokea na kuwatenganisha wao wawili, naye Eliya akapanda mbinguni katika upepo wa kisulisuli.
12 Elisha saw it. He cried out, “My father/master! My father/master! The chariots of us Israeli people and their drivers [have taken my master away]!” [They disappeared into the sky, ] and Elisha never saw Elijah again. Then Elisha tore his own robe into two pieces [to show that he was sad].
Elisha aliona hili, naye akapaza sauti, “Baba yangu! Baba yangu! Magari ya Israeli na wapanda farasi wake!” Naye Elisha hakumwona tena. Kisha akazishika nguo zake mwenyewe na kuzirarua.
13 Elijah’s cloak [had fallen off when he was taken away, so] Elisha picked it up and returned to the bank of the Jordan [River].
Akaliokota lile vazi lililoanguka kutoka kwa Eliya, kisha akarudi na kusimama ukingoni mwa Yordani.
14 He [rolled up the cloak and] struck the water with it, and cried out, “Will Yahweh, the God who [enabled] Elijah [to perform miracles, enable me to do similar things]?” Then the water separated, and a path opened up for him, and Elisha went across.
Ndipo akalichukua lile vazi ambalo lilikuwa limeanguka kutoka kwa Eliya, naye akayapiga yale maji nalo. Akauliza, “Yuko wapi sasa Bwana, Mungu wa Eliya?” Elisha alipoyapiga maji, yakagawanyika kulia na kushoto, naye akavuka.
15 When the group of prophets from Jericho saw what happened, they exclaimed, “Elisha now has the power that Elijah had!” [MTY] They walked over to him and bowed down in front of him.
Wale wana wa manabii kutoka Yeriko waliokuwa wakitazama wakasema, “Roho wa Eliya inamkalia Elisha.” Nao wakaenda kumlaki na kusujudu hadi nchi mbele yake.
16 [One of] them said, “Sir, if you permit us, 50 of our strongest men will go and search for your master [on the other side of the river]. Perhaps the Spirit of Yahweh has left him on some mountain or in some valley.” Elisha replied, “No, do not send them.”
Wakasema, “Tazama, sisi watumishi wako tunao watu hamsini wenye uwezo. Waruhusu waende kumtafuta bwana wako. Labda Roho wa Bwana amemtwaa na kumweka katika mlima fulani au bonde fulani.” Elisha akajibu, “Hapana, msiwatume.”
17 But they kept insisting. Finally he was tired of saying “No,” and he said, “Okay, send them.” So 50 men searched for three days, but they did not find Elijah.
Lakini wakasisitiza, mpaka akaona aibu kuwakatalia. Hivyo akasema, “Watumeni.” Nao wakawatuma watu hamsini, wakamtafuta kwa siku tatu, lakini hawakumpata.
18 They returned to Jericho, and Elisha was still there. He said to them, “I told you that you should not go, [because you would not find him]!” [RHQ]
Walipomrudia Elisha, ambaye alikuwa akingojea huko Yeriko, akawaambia, “Je, sikuwaambia msiende?”
19 Then the leaders of [Jericho] city came to talk with Elisha. One of them said, “Our master, we have a problem. You can see that this is a very nice place [to live in]. But the water is bad, and as a result, crops will not grow on the land.”
Watu wa mji wakamwambia Elisha, “Tazama, bwana wetu, mahali mji huu ulipojengwa ni pazuri, kama bwana wangu aonavyo, lakini maji yake ni mabaya, na nchi haizai.”
20 Elisha said to them, “Put some salt in a new bowl and bring the bowl to me.” So they brought it to him.
Akasema, “Nileteeni bakuli mpya, mweke chumvi ndani yake.” Kwa hiyo wakamletea.
21 Then he went out to the spring [from which the people in the town got water]. He threw the salt into the spring. Then he said, “This is what Yahweh says: ‘I have made this water good/pure. No longer will anyone die, from having drunk this water, and now crops will be able to grow.’” [LIT]
Kisha akaenda kwenye chemchemi na kuitupa ile chumvi ndani yake, akisema, “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nimeyaponya maji haya. Kamwe hayatasababisha mauti tena wala kutozaa.’”
22 And the water became pure, just as Elisha said it would be. Since that time it has always remained pure.
Nayo yale maji yakaponywa mpaka leo, sawasawa na neno la Elisha alilokuwa amesema.
23 Elisha left Jericho and went up to Bethel. As he was walking along the road, a group of young boys from Bethel [saw him and] started to make fun of him. They continued shouting, “Go away, you bald-headed man!”
Kutoka huko Elisha akakwea kwenda Betheli. Ikawa alipokuwa akitembea barabarani, baadhi ya vijana wakatoka mjini na kumfanyia mzaha. Wakasema, “Paa, wewe mwenye upaa! Paa, wewe mwenye upaa!”
24 Elisha turned around and looked/glared at them. He asked Yahweh to (curse them/do something bad to them). Immediately two bears came out of the woods and mauled forty-two of them.
Akageuka, akawatazama na kuwalaani kwa Jina la Bwana. Kisha dubu wawili wa kike wakatokea mwituni na kuwararua vijana arobaini na wawili miongoni mwao.
25 Elisha left Bethel and went to Carmel Mountain, and after that he returned to Samaria [city].
Naye akaondoka huko, akaenda Mlima Karmeli, na kutoka huko akarudi Samaria.

< 2 Kings 2 >