< 1 Peter 4 >

1 Therefore, because Christ suffered physically, you also must think the way that he did [when he was willing to suffer], because those who suffer [because of belonging to Jesus] have stopped sinning [the way they used to sin].
Kwa hiyo, kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni nia iyo hiyo kwa maana mtu aliyekwisha kuteswa katika mwili ameachana na dhambi.
2 As a result, during their remaining time here on earth, they do not do the things that sinful people desire to do, but instead they do the things that God wants them to do.
Kwa hivyo, haishi maisha yake yaliyobaki ya kuishi hapa duniani kwa tamaa mbaya za wanadamu, bali anaishi kwa mapenzi ya Mungu.
3 [I say that to you] because [SAR] you have already spent too much of your time [here on earth] doing what the people who do not know God like to do. In the past you committed all kinds of sexually immoral acts [DOU], you got drunk and then participated in (orgies/wild parties) and carousing/revelry, and you [worshipped] idols, which is very displeasing to God.
Maana wakati uliopita mmekwisha kutumia muda wa kutosha katika maisha yenu mkifanya yale ambayo wapagani hupenda kutenda: wakiishi katika uasherati, tamaa mbaya, ulevi, karamu za ulafi, vileo, ngoma mbaya, na ibada chukizo za sanamu.
4 [Because you used to do those things], [your friends] are surprised that you do not join them any more when they participate in that kind of wild behavior [that] ([is rushing to/will quickly]) [destroy them like] [MET] a flood. As a result, they say evil things about you.
Wao hushangaa kwamba ninyi hamjiingizi pamoja nao katika huo wingi wa maisha ya ufisadi, nao huwatukana ninyi.
5 But [God] is ready to judge the people who are living [now] and the people who have died, and he is the one who will decide whether he approves of what each of them has done.
Lakini itawapasa wao kutoa hesabu mbele zake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa.
6 That is the reason why the message [about Christ] was preached {[people] preached the message [about Christ]} to believers who have now died. [That message was preached to them] in order that even though [sinful] people might judge them [and say that they are guilty], God’s Spirit would [enable them to] live [eternally].
Kwa kuwa hii ndiyo sababu Injili ilihubiriwa hata kwa wale waliokufa, ili wahukumiwe sawasawa na wanadamu wengine katika mwili, lakini katika roho waishi kulingana na Mungu aishivyo.
7 It is almost the time when everything on this earth will come to an end. Therefore, keep thinking sensibly/reasonably and control what you think [DOU], so that you can pray [clearly].
Mwisho wa mambo yote umekaribia. Kwa hiyo kuweni na akili tulivu na kiasi, mkikesha katika kuomba.
8 Most important of all, love each other earnestly/wholeheartedly, because if we love others [PRS], we will just ignore many of the sinful things that [they do to us].
Zaidi ya yote, dumuni katika upendo kwa maana upendo husitiri wingi wa dhambi.
9 Provide food and a place to sleep for those [who come to your community], [and do it] without complaining.
Kuweni wakarimu kila mtu na mwenzake pasipo manungʼuniko.
10 Believers should all use the spiritual gifts that God has given them to serve others. They should manage/use well the various gifts that God has kindly given them.
Kila mmoja na atumie kipawa chochote alichopewa kuwahudumia wengine, kama mawakili waaminifu wa neema mbalimbali za Mungu.
11 Those who speak [to the congregation] should do that as though they are speaking the [very] words of God. Those who do kind things to others should do it with the strength that God gives them, in order that God may be honored by all this {that all this may honor God} as Jesus Christ [enables us to do it. I pray that we will] praise [God] (OR, [Jesus]) and allow him [to rule over us] forever. (May it be so!/Amen!) (aiōn g165)
Yeyote asemaye hana budi kusema kama mtu asemaye maneno ya Mungu mwenyewe. Yeyote ahudumuye hana budi kuhudumu kwa nguvu zile anazopewa na Mungu, ili Mungu apate kutukuzwa katika mambo yote kwa njia ya Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
12 You whom I love, do not be surprised about the painful things that you are suffering [because you belong to Christ]. [Those] things are [testing you as metals are tested by people putting them] in a fire. Do not think that something strange is happening to you.
Wapenzi, msione ajabu kwa yale mateso yanayotukia miongoni mwenu, kana kwamba ni kitu kigeni kinachowapata.
13 Instead, rejoice that you are suffering the same kinds of things that Christ endured. Rejoice when [you suffer], in order that you may also be very glad [DOU] when Christ returns and reveals how glorious/wonderful he is.
Bali furahini kuwa mnashiriki katika mateso ya Kristo, ili mpate kufurahi zaidi wakati utukufu wake utakapofunuliwa.
14 If you are insulted {If [people] insult you} because you believe in Christ [MTY], [God is] pleased with you, because it shows that the Spirit of God, the Spirit who [reveals how] great [God is], lives within you.
Kama mkitukanwa kwa ajili ya jina la Kristo, mmebarikiwa, kwa sababu Roho wa utukufu na wa Mungu anakaa juu yenu.
15 If you suffer, do not let that suffering be the result of your being a murderer or a thief or as a result of doing some other evil thing, or as a result of interfering in someone else’s affairs.
Lakini asiwepo mtu yeyote miongoni mwenu anayeteswa kwa kuwa ni muuaji, au mwizi, au mhalifu wa aina yoyote, au anayejishughulisha na mambo ya watu wengine.
16 But if you suffer because of being a Christian, do not be ashamed about it. Instead, praise God that you are suffering because of belonging to Christ [MTY].
Lakini kama ukiteseka kwa kuwa Mkristo, usihesabu jambo hilo kuwa ni aibu, bali mtukuze Mungu kwa sababu umeitwa kwa jina hilo.
17 I say that, because it is now time for God to begin judging people, and first he will judge those who belong [MTY] to him. Since he will judge us believers first, think about the terrible things that will happen to [RHQ] those who do not obey the good message that comes from him!
Kwa maana wakati umewadia wa hukumu kuanzia katika nyumba ya Mungu. Basi kama ikianzia kwetu sisi, mwisho wa hao wasiotii Injili ya Mungu utakuwaje?
18 [That will be as it] is written in the Scriptures, [Many] righteous people [will have to suffer] many [difficult trials before going to heaven]. So ungodly and sinful people will surely have to suffer [much severe punishment from God]!
Basi, “Ikiwa ni vigumu kwa mwenye haki kuokoka, itakuwaje kwa mtu asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?”
19 Therefore, those who suffer because of its being God’s will that they suffer [because of being Christians] should commit themselves to God, the one who created them and the one who always does what he promises to do. And they should continue to do what is right.
Kwa hiyo, wale wanaoteswa kulingana na mapenzi ya Mungu, wajikabidhi kwa Muumba wao aliye mwaminifu, huku wakizidi kutenda mema.

< 1 Peter 4 >