< 1 John 1 >
1 That which was from the beginning, that which we have heard, that which we have seen with our eyes, that which we looked upon, and our hands handled, concerning the word of life,
Tunawajulisha lile lililokuwepo tangu mwanzo, lile tulilosikia, ambalo tumeliona kwa macho yetu, ambalo tumelitazama na kuligusa kwa mikono yetu, kuhusu Neno la uzima.
2 —and the life was manifested, and we have seen it, and bear witness, and announce to you the everlasting life, which was with the Father, and was manifested to us, — (aiōnios )
Uzima huo ulidhihirishwa; nasi tumeuona na kuushuhudia, nasi twawatangazia uzima wa milele, ambao ulikuwa pamoja na Baba, nao ukadhihirishwa kwetu. (aiōnios )
3 that which we have seen and heard we announce to you, that ye also may have fellowship with us; and truly our fellowship is with the Father, and with his Son Jesus Christ.
Twawatangazia lile tuliloliona na kulisikia, ili nanyi mwe na ushirika nasi. Na ushirika wetu hasa ni pamoja na Baba na Mwanawe, Yesu Kristo.
4 And these things we write to you, that your joy may be full.
Tunaandika mambo haya ili furaha yetu ipate kuwa timilifu.
5 And this is the message which we have heard from him, and announce to you, that God is light, and in him is no darkness at all.
Huu ndio ujumbe tuliosikia kutoka kwake na kuwatangazia ninyi: kwamba Mungu ni nuru na ndani yake hamna giza lolote.
6 If we say that we have fellowship with him, and walk in the darkness, we lie, and do not the truth;
Kama tukisema kwamba twashirikiana naye huku tukienenda gizani, twasema uongo, wala hatutendi lililo kweli.
7 but if we walk in the light, as he is in the light, we have fellowship one with another, and the blood of Jesus his Son cleanseth us from all sin.
Lakini tukienenda nuruni, kama yeye alivyo nuruni, twashirikiana sisi kwa sisi na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote.
8 If we say that we have no sin, we deceive ourselves, and the truth is not in us.
Kama tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe wala kweli haimo ndani yetu.
9 If we confess our sins, he is faithful and righteous to forgive us our sins, and to cleanse us from all unrighteousness.
Kama tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki, atatusamehe dhambi zetu na kutusafisha kutoka kwenye udhalimu wote.
10 If we say that we have not sinned, we make him a liar, and his word is not in us.
Kama tukisema hatukutenda dhambi, twamfanya yeye kuwa mwongo na neno lake halimo ndani yetu.